STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 1, 2014

Ajali! Wa3 wafa, basi la Taqwa lapata ajali Moro

Taarifa zilizofika hivi punde zinasema kuwa basi la Taqwa limegongana na lori na kusababishja ajali ya watu watatu na wengine kujeruhiwa.
Ajali hiyo inadaiwa kutokea eneo la Mikumi, mkoani Morogoro wakati basi hilo likidaiwa kutaka ku-overtake lori na kukutana uso kwa uso na lori jingine na kusababisha vifo vya abiria hao wanawake wakiwa wawili na mwanaume mmoja.
Taarifa zaidi zinaendelea kufuatiwa na mtajulishwa
1388581742264 1388581761327


PIGO! Waziri Mgimwa afariki, Rais Kikwete amlilia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa za kifo cha Waziri wa Fedha, Mheshimiwa William Mgimwa, aliyekuwa pia Mbunge wa Jimbo la Kalenga (Mkoa wa Iringa) kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Rais Kikwete amesema kuwa taifa limempoteza Waziri Mgimwa katika kipindi lilipokuwa linamhitaji zaidi kutokana na mchango wake mkubwa ambao amekuwa akiutoa kupitia nafasi zake za Waziri wa Serikali na mwakilishi wa wananchi wa Jimbo la Kalenga.

Kifo cha Mheshimiwa Mgimwa kimetangazwa mchana wa leo, Jumatano, Januari Mosi, 2014, na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Sefue kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika tangazo lake, Balozi Sefue amesema kuwa Waziri Mgimwa ameaga dunia asubuhi ya leo saa 5:20 (Saa za Afrika ya Kati) katika Hospitali ya Kloof Medi-Clinic , Pretoria, Afrika Kusini ambako amekuwa amelazwa kwa muda sasa.

Balozi Sefue amesema kuwa maandalizi ya kuurudisha nyumbani mwili wa Waziri Mgimwa yanafanywa na Serikali kwa kushirikiana na familia yake na kuwa taarifa zaidi za suala hilo zitatolewa baadaye kwa kadri zinavyopatikana na maandalizi yanavyoendelea.

Katika salamu zake kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda na kwa familia ya Marehemu Mgimwa, Rais Kikwete amesema:  “Sina maneno ya kutosha kuelezea mshtuko na huzuni yangu kubwa kufuatia taarifa za kifo cha Mheshimiwa Mgimwa.

Binafsi nimemtembelea mara mbili kwenye Hospitali alikokuwa amelazwa na mara ya mwisho hali yake ilikuwa imeimarika. Tulizungumza kwa kiasi cha dakika 10 hivi akanielezea nia yake na tamaa yake ya kurejea nyumbani kwa sababu hali yake ilikuwa nzuri.”

Ameongeza Mheshimiwa Rais Kikwete: “Sote tunajua mchango wake katika Serikali. Sote tulitamani kuendelea kuwa naye, lakini haya ni mapenzi ya Mungu.”

“Napenda kutoa pole nyingi na rambirambi zangu za dhati kwa wana-familia wote kwa kuondokewa na mhimili wao. Naungana nanyi katika kuomboleza msiba huo mkubwa. Napenda mjue kuwa msiba huu ni msiba wangu pia. Machungu yenu ni majonzi yangu,” amesema Rais Kikwete.

Rais pia amewatumia rambirambi wananchi wa Jimbo la Kalenga akisema kuwa wamempoteza mwakilishi na mtetezi mahiri wa maslahi yao.

Mgimwa aliyezaliwa January 20, 1950 na kuwa mbunge wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa kupitia chama cha Mapinduzi (CCM)

Dk. Mgimwa alikuwa mkufunzi katika Chuo cha Benki mkoani Mwanza, kabla ya kufanikiwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga, Mkoa wa Iringa, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Arsenal yarejea kileleni, Chelsea, Liver zaua Suarez hakamatiki

Nicklas Bendtner
Nicklas Bendtner akifunga bao la kwanza la Arsenal
Fernando Torres
Torres alipoondoa 'gundu' kwa kuifungia Chelsea bao la kwanza
Daniel Agger scores for Liverpool
Liverpool ilipoisulubu Hully City uwanja wa Anfield

Nicolas Anelka of West Bromwich Albion takes on Michael Williamson (right) and Yohan Cabaye of Newcastle
West Bromwich walipoilaza Newcastle United kwa bao la mkwaju wa penati

MABAO ya dakika za lala salama wameiwezesha Arsenal kurejea tena kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England, huku Chelsea ikiendelea kuonyesha makali yake kwa kupata ushindi ugenini dhidi ya Southampton.
Aidha Liverpool nayo imerejesha makali yake baada ya kusimamishwa hivi karibu kwa kupokea vipigo viwili mfululizo baada ya kushinda nyumba mabao 2-0, Luis Suarez akifunga bao lake la 20 katika ligi ya msimu huu.
Nicklas Bendtner aliifungia Arsenal bao dakika ya  88'  na Tim Walcott kuongeza bao la pili dakika za nyongeza za mchezo huo kumalizia kazi ya Jack Walshere iliifanya Arsenal ipumue kwa kuilaza Cardiff City na kurejea tena kileleni ilipokuwa imeshushwa na Manchester City iliyoshinda ugenini jioni hii.
Arsenal imefikisha pointi 45 moja zaidi ya City na kurejesha msimamo wa awali uliokuwapo baada ya timu zote za Top 4 kushinda jioni hii, Chelsea ikiinyoa Southampton mabao 3-0 huku Liverpool ikiwa nyumbani ikiitambia Hull City mabao 2-0.
Katika mechi ya Chelsea mabao yao yalifungwa na  Fernando Torres dakika ya 60 kabla ya William kuongea la pili dakika ya 71 akimalizia kazi ya Oscar.
Oscar aliihakikisha Chelsea inayonolewa na Jose Mourinho ushindi kwa kufunga bao la tatu dakika nane kabla ya kumalizika kwa mchezo huo akimalizia kazi ya Eden Hazard.
Liverpool ilipata ushindi wake nyumbani kupitia kwa Daniel Agger dakika ya 36 na Luis Suarez akafunga bao lake la 20 katika dakika ya 50 na kuipa 'vijogoo' hao wa Anfield ushindi muhimu katika mbio zake za kuwania ubingwa unaoshikiliwa na Manchester United.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizomalizika hivi punde, Crystal Palace ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Norwich City, Fulham iliinyoa West Ham United kwa mabao 2-1 ikiwa nyumbani na     Stoke City iliing'ang'ania Everton na kutoka sare ya  1-1.
Nayo West Bromwich baada ya kufanywa asusa kwa muda mrefu imejitutumua nyumbani kwa kuilaza Newcastle United kwa bao 1-0.
Msimamo wa ligi hiyo unaonyesha Arsenal wapo kileleni ikiwa na pointi 45 ikifuatiwa na Man City yenye pointi 44, kisha Chelsea ikifuatia ikiwa na pointi zake 43 na Livewrpool kurejea kwenye Top 4 kwa kufikisha pointi 39 na Everton ikikamilisha Tano Bora na pointi zake 38.
Pambano la mwisho la ligi hiyo itazikutanisha Manchester United itakayokuwa nyumbani dhidi ya Tottenham ambapo hata zikifungana haziwezi kubadili msimamo wa juu kwani zote zina pointi 34.

City yauanza mwaka kileleni, ila...!

Fernandinho low strike puts Manchester City ahead against Swansea City.
USHINDI wa mabao 3-2 iliyopata klabu ya Manchester City dhidi ya wenyeji wao Swansea City imeiwezesha timu hiyo kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England jioni hii ikiengua Arsenal iliyopo uwanjani kwa sasa ikiumana na Cardiff City.
City itakuwa kileleni kusubiri kuona kama itaendelea kusalia au itarejea nafasi ya pili kutegemea matokeo ya Arsenal waliopo nyumbani kwao uwanja wa Emirates.
Fernandinho ndiye aliyeanza kuiandikia City bao la kuongoza dakika ya 14 kabla ya Wilfried Bony kurejesha sekunde chache kabla ya mapumziko akimaliza kazi ya Guzman.
Kipindi cha pili kilianza kwa City kuongeza bao la pili kupitia kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast, Yaya Toure katika dakika ya 58  kabla ya Kolarov kuongeza bao jingine la tatu katika dakika ya 66 na kuipa nafuu City ugenini.
Hata hivyo  wenyeji walichomoa bao moja baada ya Bony kufunga bao jingine dakika ya 90 ambalo hata hivyo halikuisaidia Swansea kupona na kipigo kwa wageni wao ambao kwa ushindi huo wamefikisha pointi 44.