STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 1, 2014

City yauanza mwaka kileleni, ila...!

Fernandinho low strike puts Manchester City ahead against Swansea City.
USHINDI wa mabao 3-2 iliyopata klabu ya Manchester City dhidi ya wenyeji wao Swansea City imeiwezesha timu hiyo kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England jioni hii ikiengua Arsenal iliyopo uwanjani kwa sasa ikiumana na Cardiff City.
City itakuwa kileleni kusubiri kuona kama itaendelea kusalia au itarejea nafasi ya pili kutegemea matokeo ya Arsenal waliopo nyumbani kwao uwanja wa Emirates.
Fernandinho ndiye aliyeanza kuiandikia City bao la kuongoza dakika ya 14 kabla ya Wilfried Bony kurejesha sekunde chache kabla ya mapumziko akimaliza kazi ya Guzman.
Kipindi cha pili kilianza kwa City kuongeza bao la pili kupitia kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast, Yaya Toure katika dakika ya 58  kabla ya Kolarov kuongeza bao jingine la tatu katika dakika ya 66 na kuipa nafuu City ugenini.
Hata hivyo  wenyeji walichomoa bao moja baada ya Bony kufunga bao jingine dakika ya 90 ambalo hata hivyo halikuisaidia Swansea kupona na kipigo kwa wageni wao ambao kwa ushindi huo wamefikisha pointi 44.

No comments:

Post a Comment