STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 10, 2014

Arsenal yaua, Monaco Juve zapenya 16 Bora Ulaya

Wojciech Szczesny (left) looks on in shock as Arsenal players celebrate Ramsey's stunning strike
Wachezaji wa Arsenal wakishangilia bao lao kwa kumfuta kiatu Aaron Ramsey
Lukas Podolski fires past Galatasaray defender Semih Kaya to give Arsenal an early lead in the Group D clash
Podolski akifunga bao la kwanza la Arsenal
sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid ilitosha kuwavusha Juventus kwenye hatua ya 16 bora.
Wachezaji wa Juventus walifurahia baada ya timu yao kufuzu hatua ya 16 Bora
The Juventus squad couldn't hide their delight at progressing to the knockout stages of the Champions League on Tuesday evening
Hureeee!
Monaco nao walikuwa na furaha yao kama hivi

Bayer Leverkusen went through, but were disappointed at full-time after surrendering top spot to Monaco
Bayer Leverkusen naop wamefuzu 16 Bora
MABAO mawili ya kila mmoja toka kwa Aaron Ramsey na Lucas Podolski yaliiwezesha Arsenal ya Uingereza kupata ushindi mnono ugenini wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji wao Galatasaray ya Uturuki na kujihakikishia nafasi ya pili katika Kundi D la michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Podolski aliiandikia The Gunners bao la kuongoza dakika ya tatu tu tangu kuanza kwa pambano hilo kabla ya Ramsey kuongeza la pili dakika ya 11 na kisha kurudi tena kambani dakika ya 29.
Kipindi cha pili wenyeji walicharuka na kufanikiwa kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na mkongwe Wesley Sneijder kwa mpira wa adhabu ndogo katika dakika ya 87.
Dakika tatu baadaye Ramsey alihitimisha karamu ya mabao kwa kufunga bao la nne na la pili kwake katika mchezo huo na kuifanya Arsenal ikitinga hatua ya 16 Bora nyuma ya Borussia Dortmund ya Ujerumani ambayo ililazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Anderlecht ya Ubelgiji.
Vijana hao wa Arsene Wenger wana hatari ya kukutana na moja ya timu mojawapo kati ya Real Madrid, Atletico Madrid, Barcelona, PSG, Bayern Munich, Porto au Monaco katika hatua ya mtoano.
Bao la Dortmund lilifungwa na Ciro Immobile katika dakika ya 58 kabla ya wageni kuchomoa dakika sita kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia kwa Aleksandar Mitrovic  kwa njia ya kichwa.
Dortmund imeongoza kundi hilo kwa sare hiyo kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, lixcha ya kulinga pointi 13 na Arsenal.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Juventus ikiwa nyumbani ililazmisha suluhu kwa Atletico Madrid na zote mbili kufuzu kwa hatua ya 16 Bora kutoka kundi A, licha ya Olympiakos Pirates kupata ushindi mnono wa mabao 4-2 djhidi ya Malmo ya Sweden.
Nayo timu ya Monaco ya Ufaransa ilifanikiwa kusonga mbele baada ya kuilaza Zenit St Petersburg ya Russia kwa mabao 2-0 na kuongoza kundi C ambalo lilishuhudia Bayer Leverkusen wakifuzu nao licha ya kung'ang'aniwa ugenini na Benfica ya Ureno.

ZILIFUZU 16 BORA
Kundi A: Atletico Madrid na Juventus
Kundi B: Real Madrid na Basle
Kundi C:Monaco na Bayer Leverkusen
Kundi D: Borussia Dortmund na Arsenal

Liverpool yakwama, Real Madrid yaua Ulaya

Steven Gerrard looks forlorn after the final whistle as Liverpool are knocked out of the Champions League by Basle
Nahodha Steven Gerrard haamini kilichoikuta timu yake jana usiku
Basle players celebrate their qualification to the Champions League knockout phases as Bjorn Kuipers blows the final whistle
Basle wakishangilia bao lao lililofungwa na Frei
Croatian defender Dejan Lovren protests as substitute Markovic is shown a straight red card for catching Safari
Nenda nje sitaki uhuni uwanjani
Ronaldo celebrates with Gareth Bale and Javier Hernandez after scoring from the spot against Ludogorets
Ronaldo akipongezwa na wenzake
Medran scored his first Champions League goal for Real Madrid after coming off the bench for the last seven minutes
Medran akifunga bao la nne la Real Madrid
KLABU ya Liverpool imekwama kusonga mbele kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na timu ya Basle, wakati Real Madrid ikipata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Ludogorets katika mechi za Kundi B.
Ushindi huo umeiwezesha Real madrid kuongoza kundi hilo, wakati Liverpool iliyokuwa ikihitaji ushindi ili kusonga mbele imeishia kukamata nafasi ya tatu nyuma ya Basle ambayo sasa inaungana na Real madrid kusonga mbele baada ya sare ya ugenini.
Liverpool wakiwa kwenye uwanja wao wa Anfield walishshtukizwa na wageni wao kwa kufungwa bao katika dakika ya 25 kupitia Fabian Frei na kulazimika kulichomoa katika kipindi cha pili baada ya Lazar Markovic kufunga katika dakika ya 60 na kuongoza msimamo wa kundi B.
Katika pambao jingine la kundi hilo la B, Real Madrid wakiwa nyumbani waliishindilia Lodogorets kwa mabao 4-0, huku Cristiano Ronaldo akifunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penati baada ya Marelonho wa Logorotes kucheza rafu iliyomfanya atolewe nje kwa kadi nyekundu na kumfanya nyota huyo kumfikia gwiji wa zamani wa klabu hiyo Raul Gonzalez kwa idadi ya mabao aliyofunga kwenye michuano hiyo.
Ronaldo alifunga bao hilo katika dakika ya 20 na kumfanya kufikisha jumla ya mabao 72 na kusaliwa mabao mawili kumfikia hasimu wake, Lionel Messi mwenye mabao 74, ambaye usiku wa leo atakuwa dimbani tena kuiwakilisha Barcelona dhidi ya timu ya PSG.
Mabao mengine ya Real Madrid yalifungwa naGareth Bale katika dakika ya 38 kabla ya weatokea benchi Alvaro Arbeloa na Alvaro Medran kufunga mabao mengine katika dakika za 80 na 88.