STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 3, 2014

Stars yapigwa 4 Botswana kujiuliza kwa Lesotho

TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) juzi ilikubali kichapo cha mabao 4-2 kutoka kwa wenyeji wao timu ya Botswana katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika jijini Gaborone.
Mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa wa Gaborone, ilishuhudiwa hadi mapumziko Stars ilikuwa nyuma kwa mabao 3-0 licha kuonekana timu zote zikishambuliana kwa zamu.
Mabao ya Stars katika mchezo huo wa kirafiki yalifungwa na wachezaji wa klabu ya Azam, Khamis Mcha 'Vialli' na John Bocco 'Adebayor' kwa njia ya penalti.
Kikosi hichio cha kocha Mart Nooij kitashuka dimbani tena siku ya Jumamosi kupepetana na Lesothio katika pambano jingine la kirafiki la kimataifa kabla ya siku inayofuata kurejea nyumbani kujiwinda na mechi yao ya kuwania kufuzu hatua ya makundi ya kucheza Fainali za Kombe la Afrika za mwakani.
Taifa Stars imeweka kambi ugenini kwa ajili ya kujiandaa na mechi yake ya kusaka tiketi ya kucheza fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Msumbiji itakayofanyika Julai 20 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Stars ambayo ilisonga mbele katika mashindano hayo baada ya kuifunga Zimbabwe mabao 3-2 na kama itafanikiwa kuing'oa Msumbiji katika mechi zao itaangukia kundi moja na timu za Zambia, Cape Verde na Niger ili kuwania kucheza fainali hizo za Afrika zitakazofanyika nchini Morocco.

No comments:

Post a Comment