STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Lionel Messi kuendeleza makali yake Brazil

Lionel Messi
BAADA ya Neymar na Thomas Muiller kushindwa kuongeza bao lolote katika hatua ya 16 Bora ya Fainali za Kombe la Dunia na kusaliwa na mabao yao manne manne, nyota wa Argentina Lionel Messi ana nafasi ya kuwakacha wenzao hao wa kuwania Kiatu cha Dhahabu' iwapo atafunga leo na kumfikia kinara wa mabao wa sasa katika fainali hizo James Rodriguez mwenye mabao matano.
Rodriguez wa Colombia alifikisha idadi hiyo ya mabao baada ya kufunga mabao mawili wakati akiivusha nchi yake hadi Robo Fainali mbele ya timu ya Uruguay iliyokosa huduma za Luis Suarez aliuyefungiwa na FIFA kwa kosa la kumng'ata Giorgio Chiellini wa Italia.
Messi ambaye amefunga katika mechi zote zilizopita nchi yake leo itakuwa ikikabiliana na Uswisi katika mechi ya kuamua hatma ya timu ipi ya kuungana na Brazil, Uholanzi, Colombia, Ufaransa na Ujerumani katika Robo Fainali zitakazoanza Ijumaa.
Nyota huyo anayekipiga Barcelona katika fainali za mwaka huu ameonekana moto wa kuotea mbali kiasi cha kubashiriwa kuwa Mchezaji Bora na hata kunyakua kiatu cha Dhahabu kama ataendelea kutupia mabao kambani akichuana na wakali wenzake.
Nahodha huyo wa Argentina anategemewa kuendelea kuwatesa mabeki wakati wakikabiliana na Uswisi ambao kupitia kocha wake, Ottmar Hitzfeld ameahidi kutumia 'kijiji' kumkaba ili asiwaletee madhara kama alivyowafanyia timu hiyo katika fainali hizo za Brazil.
Nyota wenzake wa Brazil , Neymar na Muiller wa Ujerumani walishindwa kufunga bao lolote katika mechi zao za 16 Bora na kuendelea kusaliwa na mabao yao manne kama aliyonayo Messi na kuachwa kwa idadi ya bao moja na Rodriguez ambaye ameonekana ni mbadala halisi ya Radamel Falcao aliyezikosa fainali hizo kwa kuwa majeruhi.
Mbali na mechi ya Argentina na Uswisi pia leo kutakuwa na pambano jingine la kumalizia ratiba ya 16 Bora kati ya Ubelgiji dhidi ya Marekani.
ORODHA YA WAFUNGAJI:
5-James Rodriguez (Colombia)
4- Lionel Messi (Argentina)
    Thomas Muiller (Ujerumani)
    Neymar (Brazil)
3- Karim Benzema (Ufaransa)
    Arjen Robben (Uholanzi)
    Robin van Persie (Uholanzi)
    Xherdar Shaqiri (Uswisi)
    Enner Valencia (Ecuador)
2- Andre Ayew (Ghana)
    Wilfried Bony (Ivory Coast)
   Tim Cahill (Australia)
   Clint Dempsey (Marekani)
   Memphis Depay (Uholanzi)
   Asamoah Gyan (Ghana)

No comments:

Post a Comment