STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Afrika majanga! Nigeria, Algeria zafurushwa Brazil



Andre Schuller akiifungia Ujerumani bao la kuongoza
WAAFRIKA hawana chao tena kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Brazil baada ya usiku wa jana timu pekee mbili zilizokuwa zimesalia kwenye michuano hiyo kung'olewa na timu za Ulaya.
Super Eagles ya Nigeria ilianza kuaga mapema na kuendeleza mzimu wa kushindwa kuvuka hatua ya 16 katika fainali zake zote ilizocheza kwa kukubali kipigio cha mabao 2-0 toka kwa Ufaransa, huku baadaye Mbweha wa Algeria walikufa kiume kwa kulazwa mabao 2-1 katika muda wa nyongeza baada ya kukomaa kwa dakika 90 bila kufungana na Ujerumani.
Katika mechi ya Nigeria na Ufaransa iliyoanza mapema, Nigeria ilishindwa kuonyesha soka kama ilivyoumana na Argentina na kuruhusu Ufaransa kuwatawala na kujipatia mabao yake kupitia ya Paul Pogba na jingine la kujifunga la beki Joseph Yobo na kuhitimisha mbio zao kwenye fainali hizo zinazoingia hatua ya Robo Fainali.
Pogba anbayekipiga Juventus alifunga bao lake katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa Garrincha, Brasilia, katika dakika ya 79 kwa njia ya kichwa na dakika mbili baadaye Yobio alijhifunga bao katika harakati za kuiokoa mpira wa krosi na kuwafanya Tai hao wa Kijani kurejea nyumbani kama ilivyokuwa kwaIvory Coast, Cameroon na Ghana zilizoaga mapema na kukwama kutimiza ndoto za kutinga Robo Fainali kwa mara ya kwanza.
Katika mechi iliyiofuatailiyiochezwa Uwanja wa Beira-Rio mjini Porto Alegre, dakika 90 za mchezo kati ya Ujerumani na Algeria zilishuhudia timu hizio zikiwa nguvu sawa kwa kutofunaga na kuiongezewa dakika 30 zilizokuwa mwiba kwa Waafrika baada ya Andre Schurrle kufunga bao dakika mbili tangu kuanza kwa muda huo kabla ya Mesut Ozil kuiongeza la pili dakika ya 119.
Hata hivyo Algeria walioonyesha soka la ushindani katika michuano hiyo tofauti na walivyokuwa wakichukuliwa awali walipata bao la kufutia machozi kwenye dakika za ziada kabla ya mchezo kumalizika kupitia kwa Abdelmoumene Djabou.
Kwa matokeo hayo ni kwamba Ujerumani na Ufaransa watakutana kwenye mechi ya Robo Fainali huku timu za Afrika zikirudi nyumbani kishujaa hata hivyo.

No comments:

Post a Comment