STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Hatimaye Suarez aiomba radhi kwa kosa la kung'ata mtu Brazil

Suarez alipomng'ata Chiellini
MSHAMBULIAJI 'mtukutu' wa Uruguay aliyefungiwa na FIFA kwa kosa la kumng'ata mchezaji mwenzake wa Italia, Luis Suarez amepoza shutuma dhidi yake baada ya  kuomba radhi.
Suarez alimng'ata bega beki wa Azzuri Giorgio Chiellini katika mechi yao ya makundi na kufungiwa na FIFA kwa muda wa miezi minne.
Katika hali isiyo kawaida nyota huyo ameomba radhi usiku wa jana na kuahidi hatorudia kufanya kosa kama hilo, japo inaelezwa Barcelona ilimpa shinikizo la kufanya hivyo ili kuweza kuiwania saini yake.
Siku nne baada ya kufungiwa miezi minne na ameambia FIFA kwamba tukio hilo lilitokea katika mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Italia mjini Natal lilitokana na kushindwa kujizuia.
Mshambuliaji huyo wa Liverpool ameibuka kikamilifu na kujutia kosa lake. Lakini kuomba kwake radihi kunakuja katika wiki ambayo habari zimevuma mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 anatakiwa kwa dau la Pauni Milioni 80 Nou Camp.
Gary Lineker, mshambuliaji wa zamani wa Barcelona, amesema klabu hiyo ya Katalunya imemuambia Suarez bombe msamaha kama wanataka waendelee na jitihada za kumnunua.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwenye ukurasa wake wa Twitter, Suarez amesema: "Baada ya siku kadhaa za kuwa nyumbani na familia yangu, nimepata fursa ya kutuliza jazba na kufikiria haswa kilichotokea katika mechi ya Italia na Uruguay Juni 24, 2014.
"Kutokana na kilichotokea na yote yaliyofuatia baadaye, kiasi cha kuathiri hata kiwango cha timu yangu ya taifa, ukweli ni kwamba mchezaji mwenzangu Giorgio Chiellini ameumizwa na kilichotokea kwa kumng'ata,".
"Kwa hili: Najuta kwa kiasi kikubwa kufanya hivyo. Naomba radhi kwa Giorgio Chiellini na familia ya soka kwa ujumla. nauambia umma kwamba halitatokea tukio kama hili tena,".
Beki wa Juventus, Chiellini ameretweet msamaha wa Suarez katika mtandao wake, baada ya awali kusema adhabu ya kumfungia miezi minne Suarez ni kubwa. 
Chiellini amejibu kwenye akaunti yake ya Tweeter moja kwa moja akisema: "Yote yamesahaulika. Natumai FIFA itakupunguzia adhabu,".

No comments:

Post a Comment