STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Taifa Stars uso kwa uso na Botswana kirafiki leo Gaborone

Kikosi cha Taifa Stars
KIKOSI cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars jioni ya leo inatarajiwa kushuka kwenye dimba la Taifa la Botwana mjini Gaborone kuumana na wenyeji wao Botswana katika pambano la kirafiki la kimataifa.
Pambano hilo ni maalum kwa Stars kwa ajili ya kujiwinda na mchezo wao wa kuwania kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Afrika hatua ya makundi dhidi ya Msumbiji mechi itakayopigwa wiki tatu zijazo.
Stars inayonolewa na kocha Mart Nooij, ipo Botswana tangu wiki iliyopita ikijifua na itashuka dimbani leo mjini Gaborone bila winga wake nyota Mrisho Ngassa aliyekuwa ameenda Afrika Kusini kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Free State Stars, p-ia itakosa huduma za nyota wake wengine kama Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza TP Mazembe.
Hata hivyo bado ina kikosi bora kabisa ambacho kitaweza kutoa upinzani kwa wenyeji ambao wanakutana nao kwa mara ya kwanza tangu walipokutana mara ya mwisho mwaka 2012 katika pambano la kirafiki la kimataiafa lililoisha kwa sare ya 3-3 nchini humo.
Taarifa kutoka Botwana zinasema kuwa wachezaji wote wapo fiti tayari kwa mechi hiyo na baada ya hapo itashuka tena dimbani Ijumaa ya Julai 11 kuumana na Lesotho katika mchezo mwingine wa kirafiki wa kimataifa kabla ya kurejea nyumbani kuwasubiri Mamba wa Msumbiji.
Stars ambayo haijashiriki Fainali hizo za Afrika tangu ilipofanya hivyo mara ya kwanza na mwisho mwaka 1980 itarudiana na Mamba Agosti 2 mjini Maputo kama itafanikiwa kuvuka hatua hiyo itaingia kwenye kundi moja na timu za Zambia, Cape Verde na Niger kuwania kufuzu fainali zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

No comments:

Post a Comment