STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Kisiga afunikwa na Kisiga Mchangani

Na Adam Fungamwango
KIUNGO mshambuliaji wa Mtibwa Sugar Shaaban Kisiga, juzi alikutana na mchezaji mwingine kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwananyamala anayetumia jina lake ambaye alimfunika vilivyo.
Shaaban Kisiga huyo 'feki' alikuwa anaichezea timu Morning Star ya Msasani, huku Kisiga mwenyewe akiwa anaichezea Morning Star ya Kiwalani.
Hata kwenye fomu za majina kwa waamuzi, pamoja na timu zote mbili kuwa na majina yanayofanana, lakini pia ilikuwa na majina yanayofanana, kila timu ikiwa na Shaaban Kisiga.
Ina maana kukawa na Kisiga halisi yaani 'original' na mwingine 'feki'.
Katika mchezo huo uliochezeswa na waamuzi wa kike watupu, Mwanahamisi Matiku, Germina Simon na Neuru Mushi, Kisiga 'feki' alionekana kumfunika Kisiga halisi kiasi cha kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa bao 1-0 kwenye mechi ya robo fainali ya kwanza ya Wadau Cup.
Bao la Morning Star ya Msasani dhidi ya Morning Star ya Kiwalani lilifungwa na Oscar Magari katika dakika ya 52, baada ya pande safi kutoka kwa Kisiga 'feki'.
Mabeki wa Morning Star ya Msasani walikuwa na kazi moja tu, kuhakikisha kuwa Kisiga 'original' ambaye alicheza nafasi ya ushambuliaji haleti madhara na kweli walifanikiwa.
Timu hizo mbili zitarudiana wiki ijayo kwenye mechi ya robo fainali ya pili itakayochezwa kwenye uwanja huo huo wa shule ya msingi Mwananyamala.

No comments:

Post a Comment