STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Diamond: Asiyekubali kushindwa si mshindani

NYOTA wa nyimbo za 'My Number One' na 'Mdogomdogo', Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz, ameonyesha uungwana kwa kuamua kukubali matokeo ya kushindwa kutwaa tuzo za kimataifa za BET 2014 alizokuwa akiwania na wakali wengine wa Afrika na kushuhudia Mnigeria Davido akimuangusha kwa mara nyingine tena.
Diamond alikuwa akiwania tuzo hiyo kupitia kipengele cha msanii wa kimataifa toka Afrika (Best International Act-Africa) na kujikuta akiangushwa na Davido ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu na Mnigeria huyo aliyemshirikisha katika wimbo wake wa 'My Number One remix' kumbwaga katika tuzo za MTV Africa 2014.
Dakika chache baada ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo hizo zilizofanyika nchini Marekani, Diamond alitupia ujumbe katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii akieleza kukubali matokeo hayo na kuwashukuru wote waliomuunga mkono kwenye tuzo hizo.
"Tusipopenda kukubali matokeo na ushindi wa wenzetu basi daima hatutaweza kuwa washindani...Muhimu ni kujua wapi tulipotoka na wapi tulipo leo, katika nchi zaidi ya 20 zenye wasanii zaidi ya milioni 40 kuchaguliwa Tanzania ni fursa, heshima na hatua kubwa...Cha muhimu ni kuitumia vyema fursa hii na kuhakikisha mwakani tunapiga hatua. Asante sana kwa wote wanaozidi kunisapoti," aliandika.
Katika tuzo hizo Diamond alikuwa akichuana na Davido pamoja na Mafikizolo wa Afrika Kusini, Sarkodie wa Ghana, Tiwa Savage na Toofan wa Togo. Nyota ya Diamond inazidi kung'aa hata hivyo baada ya Mafikizolo kumuomba kufanya naye wimbo.

No comments:

Post a Comment