STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Masai anasikilizia Yero Masai

Yero Subhai! Gilliard Severine 'Masai Nyota Mbofu latika pozi
MCHEKESHAJI mahiri nchini, Gilliad Severine 'Masai Nyota Mbofu' amesema bado hajaamua kufanya nini kwa sasa baada ya kuachana na kampuni ya Al Riyamy akidai anasikilizia kazi yake mpya 'Yero Masai' aliyoachia hivi karibuni.
Akizungumza na MICHARAZO mwishoni wa wiki, Masai alisema bado hajajua aibukie wapi kwa sasa akiendelea na mchakato wake wa kutoa video ya wimbo wake uitwayo 'Masai ya Wapi' alioimba na Christian Bella wa Malaika Band.
"Kwa kweli mpaka sasa sijajua hatma yangu itakuwaje, ila nahangaika kutoa video ya 'Masai ya Wapi' huku nikisikilizia kazi yangu mpya iliyopo hewani kwa sasa iitwayo 'Yero Masai' niliyoimba na Rich Mavoko na Kitokololo", alisema.
Mchekeshaji huyo alitangaza kujiondoa kwenye kampuni ya Al Riyamy inayozalisha filamu  na vichekesho vya kipindi cha Vituko Show na alisema anajiopanga kuibuka kampuni yoyote itakayokuwa ikimhitaji au aendelee kufanya kazi mwenyewe kama msanii huru.

No comments:

Post a Comment