STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Mwenyekiti CCK yawapuuza wanaokiwabeza chama chao

Constantine Akitanda (kulia) alipokuwa akipokea hati ya usajili wa chama chake toka kwa aliyekuwa msajili wa vyama nchini, John Tendwa
MWENYEKITI wa Chama cha Kijamii (CCK), Constantine Akitanda, amewapuuza wanaokibeza chama chake kwa maamuzi yao ya kufanya ziara mikoani kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu na manufaa ya kupatikana Katiba Mpya.
Aidha, chama hicho, kimesisitiza kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) ndiyo adui yao namba moja, hivyo katu hakiwezi kukubali kuwa kibaraka katika kuwasafishia njia ya kuendelea kukaa madarakani zaidi kama baadhi ya watu wasiokitakia mema chama hicho wanavyodai.
Akizungumza kwa njia ya simu jana akiwa safarini, Akitanda, alisema CCK na chama mshirika cha NRA wameamua kufanya ziara hiyo mikoani kutoa elimu juu ya upotoshaji unaofanywa na baadhi ya wanasiasa kuhusiana na Katiba Mpya.
Alisema ziara hiyo wanaifanya kwa nguvu zao wenyewe kama njia ya kuonyesha ukomavu wao na kiu kubwa ya kuwazindua wananchi ambao wamekuwa 'kizani' kuhusu mchakato huo wa Katiba.
"Wale wanaotubeza wanafanya hivyo kwa sababu wana wivu na hawatujui vyema, CCK kama taasisi ina mipango na mikakati yake na inajiendesha kwa kujitegemea bila msaada wa yeyote kama baadhi ya vyama vinavyofanya," alisema.
Alisema dai kwamba wanafanya ziara hiyo mikoani kwa ufadhili wa CCM ili kuvuruga mambo ambayo Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umekuwa ukihubiri kuhusu mchakato mzima wa katiba, ni upuuzi.
"Tulishatangaza tangu awali kuwa, adui yetu namba moja ni CCM, sasa iweje adui huyo aje awe mfadhili wetu inaingia akilini kweli, watu waache mtazamo hasi kwa vyama vinavyotofautina na vingine," alisema.
Alisema chama hicho kipo tayari kutofautiana na chama chochote katika suala zima la upotoshaji wa Katiba Mpya kwani Rasimu ya Katiba Mpya kwani ina mambo mengi ya msingi yanayowagusa wananchi moja kwa moja kuliko suala la mfumo na muundo wa serikali.

"Vyama vidogo vimekuwa vikionekana mamluki vinapotofautiana na vyama vikuu, ila ukweli vyama vyote vina nafasi sawa mbele ya Msajili wa Vyama na Watanzania na tunachokifanya ni sahihi," alisema.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Akitanda na Mwenyekiti wa NRA, Rashid Mtuta walitangaza nia yao ya kuzungumza baadhi ya mikoa ili kutoa elimu kuhusu masuala ya Katiba kilichopokelewa kwa hisia tofauti na baadhi ya vyama vya siasa.

No comments:

Post a Comment