STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 6, 2018

Rostand anatunguliwa na kipa mwenzake

YANGA wanafungwa bao la nne kwa mkwaju wa penalti iliyopigwa na Zammamouche na kuifanya USM kutoka na ushindi mnono wa mabao 4-0. Pambano limeisha mara baada ya mkwaju huo.

Waarabu wanapata penalti

USM wanapata penalti baada ya Dante kucheza faulo ndani ya lango lake.

Zimeongezwa dakika mbili

ZIMEONGEZWA dakika mbili kabla ya pambano la Yanga na USM Alger kumalizika na matokeo bado ni 3-0.

Dante ameumia

BEKI na nahodha wa mchezo wa leo, Dante ameumia na anapatiwa matokeo. Bado dakika mbili mpira kumalizika. Yanga wapo nyuma mabao 3-0. Yohana Mkomola pia kaingia kuchukua nafasi ya Yusuf Mhilu aliyeshindwa kabisa kufurukuta.

Pato anaingia kumpokea Makapu

YANGA imefanya mabadiliko kwa kumtoa Juma Said 'Makapu' na kuingia Pato Ngonyani. USM Alger wamebanwa kwa sasa, lakini bado wanaongoza kwa mabao 3-0.

Darfalou alimwa kadi naye

Oussumana darfalou naye anapewa kadi ya njano kwa kumchezea Abdallah Shaibu Ninja anayekaba hadi kivuli. Dakika ya 70. Mabao bado 3-0.

Juma Mahadhi apewa kadi

JUMA Mahadhi anakuwa mchezaji wa kwanza kupewa kadi ya njano katika mchezo huu, Matokeo bado 3-0.

Rafael anatoka Abdul anaingia

Juma Abdul
YANGA imefanya mabadiliko ya kumtoa Rafael Daud na kumuingiza Juma Abdul ikiwa ni mbinu ya benchi la ufundi la Yanga kuimarisha ulinzi baada ya kuona wasipokuwa makini watapigwa nyingi.
Dakika ya 65' USM 3 Yanga 0

Yanga inapigwa la tatu


MAMBO yanazidi kuwa magumu kwa Yanga baada ya wenyeji kuandika bao la tatu, kutokana na uzembe wa mabeki na kipa Rostand na Abderrahmane Meziane anauweka kimiani mpira ikiwa ni dakika ya 54.
USM Alger 3 Yanga )

Hassan Kessy anaupiga mwingi

BEKI Hassan Kessy ndiye pekee anayeonekana kujitoa uwanjani akihakaka kila mahali.

Waarabu wameanza uhuni wao

MMOJA wa wachezaji wa USM Alger anafanya uhuni wa kupiga mpira na kumgandishia mguu beki Dante na kumfanya apatiwe matibabu. Hata hivyo Dante anaendelea. Matokeo bado 2-0.

Mopira umeanza

Dakika 45 za pili zimeanza, na Yanga wanafika langoni mwa USM Alger. Matokeo bado 2-0.

Timu zinarudi uwanjani

TIMU za Yanga na USM Alger zinarudi uwanjani kuanza kipindi cha pili.

Takwimu za nusu ya kwanza

USM Alger                        Yanga
2              Goals                 0

9              Shots                 3
3              Shots on Target   1
73%         Possession         27%
0              Yellow Card         0
0              Red Card             0
1              Offsides               2
7              Corners               1   

Ni mapumziko sasa

Pambano la Yanga na USM Alger limemaliza dakika 45 na wachezaji wanaenda mapumziko kupewa mawaidha kabla ya kurudi uwanjani kwa kipindi cha pili. USM wapo mbele kwa mabao 2-0.
Wenyeji wameposses mpira kwa asilimia 73 kwa 27 za Yanga.

Imeongezwa dakika moja ya nyongeza

Imeongezwa dakika moja kabla ya mapumziko, Yanga bado ipo nyuma kwa mabao 2-0

Yanga wanakosa bao

Shuti la Mwashiuya linaokolewa na kipa na kuinyima Yanga bao. Bao 2-0

Pengo la Tshishimbi, Chirwa, Ajibu laonekana


Bado dakika tano kabla ya mapumziko, lakini Yanga bado inahaha kurejesha mabao waliyotanguliwa na wenyeji wao, huku mapengo ya nyota watano waliobaki jijini Dar es Salaam yakionekana wazi.
Nyota hao waliokosekana kwenye mchezo huo unaoendelea mjini Algiers ni Papy Kabamba Tshishimbi, Obrey Chirwa, Kelvin Yondani, Ibrahim Ajibu na Thabani Kamusoko.

Mambo bado magumu

Pambano la Yanga na USM Alger bado linaendelea na Yanga wanapigwa bao la pili baada ya kona ya wenyeji kusindikizwa wavuni na Farouk Chafai dakika ya 33 kipa Rostand akifanya makosa yale yale na kufungwa bao rahisi. Mpira wa Chafai unamaliziwa kimiani na Pius Buswita.
USM Alger 2 Yanga 0

Yanga inapata kona ya kwanza

Yanga wanapata kona baada ya shambulizi lao kuokolewa na mabeki, wakati Geofrey Mwashiuya akijiandaa kufunga. Hata hivyo haijazaa matunda. Dk 26

Uwanja umeelemea kwa Yanga

DK 25 Yanga bado wanakimbizwa, licha ya kujitahidi kurudisha mashambulizi, lakini ni kama uwanja umeelemea upande mmoja.
Bao matokeo ni 1-0 wenyeji wapo mbele.

Yanga chupuchupu tena

Yanga chupuchupu wapigwe bao la pili, makosa ya Andrew Vincent 'Dante' na kipa Rostand ambaye amekuwa akitoka ovyo langoni mwake bila hesabu makini.
Dk 23

Yanga wanakoswa koswa

WAWAKILISHI wa Tanzania Yanga, bado wanashambuliwa na USM Alger, huku ikionekana upande wa kushoto unaolindwa na Gadiel Michael ukiwa uchochoro wa mashambulizi mengi ya wenyeji.
Dakika ya 21

Dakika ya 15 mambo bado

Matokeo bado ni 1-0 wenyeji wakiwa mbele, huku nyota wa Yanga wakionekana kuzidiwa na wenyeji.

Yanga yatanguliwa bao la mapema

DAKIKA ya Nne tu, Yanga wamesharuhusu bao la kuongoza la Waarabu wa USM Alger baada ya mabeki na kipa Youthe Rostand kushindwa kuokoa krosi pasi iliyoungwa na Oussama Darfalou
USM Alger 1 Yanga 0.

Hiki ndicho kikosi cha Yanga kitakachoanza dhidi ya USM Alger


Yanga yarahisishiwa kazi Kombe la Shirikisho Afrika

Yanga SC ambao muda mchache ujao watalianzisha kwa USM Alger katika mechi yao ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika.
KIGALI, RWANDA
WAKATI Yanga ikijiandaa usiku huu kuvaana na USM Alger mjini Algiers, Algeria, wapinzani wao katika kundi hilo, Rayon Sports ya Rwanda na Gor Mahia ya Kenya wameshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1 mjini Kigali, Rwanda.
Katika pambano hilo klililochezwa Uwanja wa Nyamirambo, wageni Gor Mahia ndio waliokuwa wa kwanza kuandika bao dakika ya 10 likifungwa na Mnyarwanda Meddie Kagere kabla ya wenyeji kuchomoa kupitia Eric Rutanga dakika ya 24.
Matokeo hayo yametioa nafuu kwa Yanga katika mbio zao za kuwania kutinga robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kundi lao, lakini ikitegemeana na matokeo yake ya usiku huu nchini Algeria.
Baada ya mchezo wao wa usiku huu, Yanga itarudi nyumbani kuisubiri Rayon katika mechi yao ya pili, wakati Gor Mahia itakuwa mjini Nairobi kuipokea USM Alger mechi zikichezwa Mei 16.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, ASEC Mimosas iliwatambia Aduana Stars ya Ghana kwa bao 1-0 mjini Abidjan, Ivory Coast, Berkane ya Morocco nayo ilishinda 1-0 dhidi ya Al Hilal Omdurman ya Sudan na Enyimba ikiwa nyumba Nigeria iliwatmbia Djoliba ya Mali kwa mabao 2-0.

Simba hii ya Lechantre tema mate chini, Okwi motoooo!

Kikosi cha Simba wanaelekea kubeba taji lao la 19 la Ligi Kuu Bara msimu huu
Emmanuel Okwi

NA RAHMA WHITEWAMESHINDIKANA. Ndio, hakuna tena wa kuizuia Simba kwani vinara hao wa Ligi Kuu Bara wamebakisha mchezo mmoja tu kabla ya kutangazwa mabingwa wa msimu huu baada ya jioni ya leo kuwatandika Ndanda FC ya Mtwara kwa bao 1-0.
Katika mchezo huo mkali uliochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam Simba iliandika bao lake kupitia kwa nyota wake, Emmanuel Okwi lililomfanya afikishe bao la 20 na kuipa Simba alama tatu muhimu wakitimiza pointi 65 baada ya mechi 27.
Kama wataenda kuitandika Singida United kwenye Uwanja wao wa nyumbani wa Namfa, Singida basi watawavua rasmi watani zao Yanga taji la Ligi Kuu baada ya Vijana wa Jangwani kulishikilia kwa misimu mitatu mfululizo.
Simba ikishinda Jumamosi ijayo dhidi ya Singida, itawafanya wafikishe alama 68 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote akiwamo Yanga ambayo imesaliwa na michezo minne mkononi huku ikiwa na alama 48 tu. Yanga ikishinda mechi zote ina uwezo wa kufikisha pointi 66 tu. Azam waliokuwa wakitarajiwa kuiletea kauzibe Simba yenye jioni a leo imekubali kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Chama la Wana na kuifanya isaliwe na alama zao 49 ikisaliwa na mechi tatu ambazo kama itashinda zote itawapa nafasi ya kufikisha pointi 58 tu ambazo zimeshapitwa na Simba kitambo.
Katika mchezo wa leo Simba ililianza pambano kwa kasi na kufanya mashambulizi mfululizo langoni mwa Ndanda, lakini umakini mdogo wa washambuliaji wao uliwanyima bao mpaka dakika ya 44 Okwi alipowapa furaha mashabiki wa Msimbazi.
Okwi alipokea pasi ndefu ya Shomary Kapombe aliyekuwa katikati ya uwanja na kukimbia na mpira akifukuzwa na mabeki watatu wa Ndanda waliokuwa wakidhani atatoa pasi kabla ya kuhamisha mpira kutoka mguu wa kulia na kuuweka kushoto na kufumua shuti kali lililomshinda kipa Daniel Makonga.
Bao hilo limemfanya Okwi afikishe bao la 20 msimu huu na kuzidi kumsogeza kwenye nafasi ya kunyakua Kiatu cha Dhahabu, huku pia akiwinda kuvunja rekodi za Amissi Tambwe aliyefunga mabao 21 misimu miwili iliyopita yakiwa mabao mengi kwa nyota wa kigeni katika Ligi Kuu Bara.
Hata hivyo Okwi atapaswa katika mechi tatu zilizosalia za timu yake afunge mabao sita ili angalau kufikia rekodi ya muda mrefu ya straika wa zamani wa Simba, Yanga na Taifa Stars, Mohammed Hussein 'Mmachinga' ya kufunga mabao mengi katika msimu mmoja.
Machinga alifunga mabao 26 katika Ligi Kuu enzi za Ligi Daraja la Kwanza katikati ya 1990 na imedumu kwa zaidi ya miaka 20 bila kuvunjwa, japo Abdallah Juma aliyewahi kutamba Mtibwa Sugar kukaribia kuivunja kwa kufunga mabao 25 msimu wa 2006.
Kipigo hicho cha leo kimeifanya Ndanda kujiweka katika mbaya zaidi ya kusalia katika Ligi Kuu kwa msimu ujao kwani imebaki nafasi ya 15 ikiwa na alama 23, moja zaidi ya timu inayioburuza mkia, Njombe Mji ambayo jana ilitandikwa mabao 4-0 na Singida.

Mkwera kamkalisha mtu kwa KO katika masumbwi


Picha tofauti zikionyesha Idd Mkwera bukta nyeusi akimnyoosha Ramadhani Shauri kabla ya mpinzani wake huyo kuokolewa na mwamuzi aliyemshika mkono, baada ya kuinuka alipolambishwa sakafu na pambano lao kumalizika raundi ya 9 kwa KO. Mkwera akishinda.
NA RAHIM JUNIOR
HANA hamu. Ndivyo unavyoweza kusema kwa Bondia Ramadhani Shauri kumkuta ya kumkuta baada ya kupigwa KO ya raundi ya 9 na Idd Mkwera katika pambano lao lililokuwa la raundi 10 lililofanyika juzi kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Katika pambano hilo mabondia wote walionekana kukamiana na kutupiana masumbwi kwa kupokezana kabla ya Mkwera kumzidi ujanja mpinzani wake katika raundi za sita, saba na nane kabla ya raundi ya tisa, Shauri kukata pumzi kwa kulamba sakafu.

Baada ya kuhesabiwa vya kutosha, mwamuzi wa pambano hilo aliamua kumaliza mchezo kutokana na Shauri kuonekana wazi amesalimu amri na asingeweza kuendelea kupokea makonde na Mkwera.
Mara baada ya pambano hilo Mkwera anayenolewa na Kocha Rajab Mhamila 'Super D' alisema licha ya kupewa mkataba wa pambano hilo ndani ya siku 16, lakini alijifua vema na ndio maana ameibuka na ushindi huku akimsifia mpinzani wake kuwa sugu kwani alipaswa kupigwa KO mapema.
Mbali na pigano hilo pia kulikuwa na michezo mingine ambapo Amani Bariki  alijikuta akipoteza kwa pointi mbele ya Haidar Mchanjo, huku Said Chino  alimchapa kwa pointi Hamza Mchanjo na James Kibazange alimpiga K.O ya raundi ya 3 Karimu Ramadhan.
Katika michezo hiyo mvua ilikatisha uhondo kwani mashabiki walijitokeza kiasi chake, lakini waliofika walipata burudani ya aina yake kutokana kwa mabondia waliopigana.

Sunday, April 29, 2018

HIZI NDIZO REKODI ZA MECHI 99 ZA WATANI TANGU 1965










RAHIM JUNIOR
SIMBA na Yanga leo zinatarajiwa kuvaana kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam katika pambano la marudiano la Ligi Kuu Bara msimu huu.
Kumekuwa na mkanganyiko mkubwa juu ya ukweli kuhusu timu hizi kongwe zimekutana mara ngapi katika mechi za Ligi Kuu Bara tangu ligi hiyo ilipoasisiwa mwaka 1965.
MICHARAZO MITUPU, limeamua kukata mzizi wa fitina kwa kuwawekea rekodi halisi ya mechi hizo kuthibitisha kuwa leo Jumapili ya Aprili 29, 2018 linapigwa pambano la 100 kwa klabu hizo.
Nani atakayeibuka na ushindi kwenye Uwanja wa Taifa? Hiyo ni baada ya kumalizika kwa dakika 90 za mchezo huo utakaochezwa na Mwamuzi Emmanuel Mwandembwa.

Rekodi zenyewe hizi hapa chini...titirika nayo...!

1) JUNI 7, 1965 (Monday)
Yanga 1-0 Sunderland (Simba)
MFUNGAJI: Mawazo Shomvi dk. 15).

2) JUNI 3,  1966 (Friday)
Yanga 3-2 Sunderland (Simba)
WAFUNGAJI:
Yanga: Abdulrahman Lukongo dk. 54, Andrew Tematema dk 67, Emmanuel Makaidi dk. 83. Sunderland: Mustafa Choteka dk 24, Haji Lesso dk. 86.

3) NOVEMBA 26, 1966 (Saturday)
Sunderland 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Mustafa Choteka dk. 44.

4) MACHI 30, 1968 (Saturday)
Yanga 1-0 Sunderland
MFUNGAJI: Kitwana Manara dk. 28.

5) JUNI 1, 1968 (Saturday)
Yanga 5-0 Sunderland
WAFUNGAJI:
Maulid Dilunga dk. 18 (penalti), Dilunga dk. 43, Salehe Zimbwe dk. 54, Zimbwe dk. 89, Kitwana Manara dk. 86.

6) MACHI 3, 1969 (Monday)
Yanga v Sunderland
(Yanga ilipewa pointi za chee na ushindi wa mabao 2-0, baada ya Sunderland kugoma kuingia uwanjani).

7) JUNI 4, 1972 (Sunday)
Yanga 1-1 Sunderland
WAFUNGAJI:
Yanga: Kitwana Manara dk. 19,
Sunderland: Willy Mwaijibe dk. 11.

8) JUNI 18, 1972 (Sunday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Leonard Chitete.

9) JUNI 23,  1973 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Haidari Abeid 'Muchacho' dk. 68.

10) AGOSTI 10, 1974 (Saturday)
Yanga 2-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Gibson Sembuli dk. 87, Sunday Manara dk. 97.
Simba: Adam Sabu dk. 16.
(Mechi ya kihistoria iliyochezwa Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza).

11) JULAI 19, 1977 (Tuesday)
Simba 6-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Abdallah Kibadeni dk. 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73, Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

12) OKTOBA 7, 1979(Sunday)
Simba 3-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Nico Njohole dk. 3, Mohammed Bakari 'Tall' dk. 38, Abbas Dilunga dk.72. Yanga: Rashidi Hanzuruni dk. 4.

13) OKTOBA 4, 1980 (Saturday)
Simba 3-0 Yanga
WAFUNGAJI: Abdallah Mwinyimkuu dk. 29, Thuwein Ally dk. 82, Nico Njohole dk. 83.

14) SEPTEMBA 5, 1981 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Juma Hassan Mkambi dk. 42

15) APRILI 29, 1982 (Thursday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Rashid Hanzuruni dk 2.

16) SEPTEMBA 18, 1982(Saturday)
Yanga 3-0 Simba
WAFUNGAJI:
Omar Hussein dk. 2 na 85, Makumbi Juma dk. 62.

17) FEBRUARI 10, 1983 (Thursday)
Yanga 0-0 Simba.

18) APRILI 16, 1983 (Saturday)
Yanga 3-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Charles Mkwasa dk. 21, Makumbi Juma dk. 38, Omar Hussein dk. 84, Simba; Kihwelu Mussa dk. 14.

19) SEPTEMBA 10, 1983 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Lila Shomari alijifunga dk. 72, Ahmed Amasha dk. 89.

20) SEPTEMBA 25, 1983 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk. 75,
Simba: Sunday Juma dk. 72.

21) MACHI 10, 1984 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 72.
Simba: Idd Pazi kwa penalti dk 20.

22) JULAI 14, 1984 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 39.
Simba: Zamoyoni Mogella dk. 17

23) MEI 19, 1985 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 6
Simba: Mohammed Bob Chopa dk. 30.

24) AGOSTI 10, 1985 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba

25) MACHI 15, 1986 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 44
Simba: John Hassan Douglas dk. 20.

26) AGOSTI 23, 1986 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila dk. 9, Malota Soma dk. 51
Yanga: Omar Hussein dk. 5.

27) JUNI 27, 1987 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Edgar 'Fongo' Mwafongo dk. 36.

28) AGOSTI 15, 1987 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Abeid Mziba dk. 14.

29) APRILI 30, 1988 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Justin Mtekere dk. 28
Simba: Edward Chumila dk. 25.

30) JULAI 23, 1988 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila 21, John Makelele dk. 58
Yanga: Issa Athumani dk. 36.

31) JANUARI 28, 1989 (Saturday)
Yanga 2-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Issa Athumani dk. 4, Abeid Mziba dk. 85
Simba: Malota Soma dk. 30.

32) MEI 21, 1989 (Sunday)
Yanga 0-0 Simba

33) MEI 26, 1990 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Mavumbi Omari dk 6.

34) OKTOBA 20, 1990 (Saturday)
Yanga 3-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk 33, Thomas Kipese dk. 82, Sanifu Lazaro dk. 89
Simba: Edward Chumila dk. 58.

35) MEI 18, 1991 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Said Sued 'Scud' dk.  7.

36) AGOSTI 31, 1991 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Said Sued Scud.

37) OKTOBA 9, 1991 (Wednesday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Athumani China dk. 3, Abubakar Salum 'Sure Boy' dk. 54.

38) NOVEMBA 13, 1991 (Wednesday)
Yanga 2-0 Simba

39) APRILI 12, 1992 (Sunday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Kenneth Mkapa dk. 10.

40) SEPTEMBA 26, 1992 (Saturday)
Simba 2-0 Yanga

41) OKTOBA 27, 1992 (Tuesday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Damian  Kimti.

42) MACHI 27, 1993 (Saturday)
Yanga 2-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Said Mwamba Kizota dk. 47 na 57
Simba: Edward Chumila dk. 75.

43) JULAI 17, 1993 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Dua Said dk. 69.

44) SEPTEMBA 26, 1993 (Sunday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Dua Said dk. 13.

45) NOVEMBA 6, 1993 (Saturday)
Simba 0-0 Yanga

46) FEBRUARI 26, 1994 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
MFUNGAJI: Mohammed Hussein 'Mmachinga' na James Tungaraza 'Boli Zozo'.

47) JULAI 2, 1994 (Saturday)
Simba 4-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi
Yanga: Constantine Kimanda.

48) NOVEMBA 2, 1994 (Wednesday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Madaraka Selemani dk. 71

49) NOVEMBA 21, 1994 (Monday)
Simba 2-0 Yanga
WAFUNGAJI: George Lucas dk. 18, Madaraka Selemani dk. 42.

50) MACHI 18, 1995 (Saturday)
Simba 0-0 Yanga

51) OKTOBA 4, 1995 (Wednesday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Mchunga Bakari dk. 79,
Yanga: Mohammed Hussein 'Mmachinga' dk. 40.

52) FEBRUARI 25, 1996 (Sunday)
Yanga 2-0 Simba

53) SEPTEMBA 21, 1996 (Saturday)
Yanga 0-0 Simba

54) OKTOBA 23, 1996 (Wednesday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk. 46

55) NOVEMBA 9, 1996 (Saturday)
Yanga 4-4 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Edibilly Lunyamila (penalti) dk. 28, Mustafa Hozza alijifunga dk 64, Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Sanifu Lazaro dk. 75.
Simba: Thomas Kipese dk. 7, Ahmed Mwinyimkuu dk. 43, Dua Saidi dk. 60 na 90.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

56) APRILI 26, 1997 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 16
Simba: Abdallah Msamba sekunde ya. 56

57) AGOSTI 31, 1997 (Sunday)
Yanga 0-0 Simba

58) OKTOBA 11, 1997 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 52
Simba: George Masatu dk. 89
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya)

59) NOVEMBA 8, 1997 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Sekilojo Chambua dk. 85
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma)

60) FEBRUARI 21, 1998 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Akida Makunda dk. 46
Simba: Athumani Machepe dk. 88

61) JUNI 7, 1998 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 28
Simba: Abuu Juma (penalti) dk. 32

62) MEI 1, 1999 (Saturday)
Yanga 3-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Idd Moshi dk. 59, Kalimangonga Ongala dk. 64, Salvatory Edward dk. 70
Simba: Juma Amir dk. 12.

63) AGOSTI 29, 1999 (Sunday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Bakari Malima dk. 49, Mohammed Hussein 'Mmachinga' dk 71

64) JUNI 25, 2000 (Sunday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Steven Mapunda dk. 59 na 72
Yanga: Idd Moshi dk. 4.

65) AGOSTI 5, 2000 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)

66) SEPTEMBA 1, 2001 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76

67) SEPTEMBA 30, 2001 (Sunday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Joseph Kaniki dk. 65,
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza)

68) AGOSTI 18, 2002 (Sunday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Madaraka Selemani 65
Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89

69) NOVEMBA 10, 2002 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

70) SEPTEMBA 28, 2003 (Sunday)
Simba 2-2 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55

71) NOVEMBA 2, 2003 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

72) AGOSTI 7, 2004 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
Yanga: Pitchou Kongo dk. 48

73) SEPTEMBA 18, 2004 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82

74) APRILI 17,  2005 (Sunday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
Yanga: Aaron Nyanda dk. 39
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

75) AGOSTI 21, 2005 (Sunday)
Simba 2-0 Yanga
MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

76) MACHI 26, 2006 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga.

77) OKTOBA 29, 2006 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

78) JULAI 8, 2007 (Sunday)
Simba 1-1 Yanga
1-1 (dakika 120)
WAFUNGAJI:
Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
Yanga: Said Maulid (dk. 55).
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo).
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

79) OKTOBA 24, 2007 (Wednesday)
Simba 1-0 Yanga
Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

80) APRILI 27, 2008: (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

81) OKT 26, 2008 (Sunday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

82) APRILI  19, 2009 (Sunday)
Simba 2-2 Yanga
WAFUNGAJI:
SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)
(Matokeo haya yanahusu mechi za Ligi ya Bara na iliyokuwa Ligi ya Muungano pekee)

83) OKTOBA 31, 2009 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

84) APRILI 18, 2010 (Saturday)
Simba 4-3 Yanga
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89

85) OKTOBA 16, 2010 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70

86) MACHI 5, 2011 (Saturday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59.
SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.
(Refa Orden Mbaga alizua tafrani uwanjani, kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidia wake namba moja).

87) OKTOBA 29, 2011 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75

88) MEI 6, 2012 (Sunday)
Simba 5-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Emmanuel Okwi dk 1 na 65, Patrick Mafisango pen dk 58, Juma Kaseja pen dk 69 na Felix Sunzu pen dk 74

89) OKTOBA 3, 2012 (Wednesday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Simba:Amri Kiemba Dk 4
Yanga:Said Bahanuzi (pen) Dk 65

90) MEI 18, 2013 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Didier Kavumbagu dk 5 na Hamis Kiiza dk 62

91) OKTOBA 20, 2013 (Sunday)
Yanga 3-3 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga:Mrisho Ngassa dk 14 na Hamis Kiiza dk 35 na 45
Simba:Betram Mombeki dk 55, Joseph Owino dk 57 na Gilbert Kazze dk 83

92) APRILI 19, 2014 (Saturday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba:Haruna Chanongo dk 75
Yanga:Simon Msuva dk 86

93) OKTOBA 18, 2014 (Saturday)
Yanga 0-0 Simba

94) MACHI 8, 2015 (Sunday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Emmanuel Okwi Dk 52

95) Septemba 26, 2015 (Saturday)
Simba 0-2 Yanga
WAFUNGAJI: Amissi Tambwe dk 44 na Malimi Busungu dk 76

96) Feb 20, 2016 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Donald Ngoma dk 36 na Amissi Tambwe dk 72

97) Okt 01, 2016 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI: Amissi Tambwe 26',  Shiza Kichuya 82'

98) Feb 25, 2017 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI: Simon Msuva 5' pen; Laudit Mavugo 66' na Shiza Kichuya 81'

99) Okt 28, 2017 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI: Obrey Chirwa 60'; Shiza Kichuya 57'

100) Apr 29, 2018 (Sunday)
Simba   ?? Yanga
 

Msimamo mechi za watani tangu 1965              P     W      D     L       F        A    PTS
YANGA    99    36    34    29    107    95    142
SIMBA     99    29    34    36    95    107    121

Kariakoo Derby, Kichuya ashindwe mwenyewe tu Uwanja wa Taifa

RAHMA WHITE
WAKATI mashabiki wa soka nchini na Afrika Mashariki wakihesabu saa zilizosalia kabla ya kitendawili cha nani mbabe kati ya wapinzani wa jadi wa soka nchini, Simba na Yanga hazijakutana jioni ya leo Jumapili hii katika pambano la Ligi Kuu, winga matata waSimba, Shiza Kichuya yupo katika nafasi nzuri ya kuandikisha rekodi tamu.
Kichuya anayeichezea Simba kwa msimu wa pili sasa tangu alipotua Msimbazi akitokea Mtibwa Sugar na kuifungia jumla ya mabao 19 katika Ligi Kuu, ni kati ya nyota watatu wanaoshikilia rekodi ya kufunga kwenye mechi tatu mfululizo wa watani.
Winga huyo anakula sahani moja na nyota wa zamani wa Simba, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' na straika wa Yanga, Amissi Tambwe, lakini kuwepo kwa mchezo wa Jumapili unampa nafasi mkali huyo kuwapiku wenzake na kuandika rekodi tamu.
Kama Kichuya atafanikiwa kuivuruga tena ngome ya Yanga na kufunga bao, atakuwa ndiye kinara na hivyo kuwapiku Madaraka aliyestaafu soka muda mrefu na Tambwe ambaye msimu huu amekuwa na wakati mgumu kuwa majeruhi wa muda mrefu.
Kichuya aliwafikia Mzee wa Kiminyio na Tambwe kwa mechi tatu zilizopita za watani ikiwamo ile ya kwanza kwanza akiwa na uzi wa Simba iliyopigwa Oktoba 1, 2016 akichomoa bao la Yanga liliwekwa na Tambwe na kusababisha vurugu za mashabiki.
Bao lake la pili alilitupia alipoisaidia Simba kuitungua Yanga katika mechi yao ya Februari 16 mwaka jana wakati Msimbazi wakiitambia Jangwani kwa mabao 2-1. Bao jingine la Simba lililokuwa la ushindi likiwekwa wavuni na Laudit Mavugo.
Katika mechi ya mwisho ya watani hao kukutana Oktoba 28, pia mwaka jana ikiwa mchezo wa duru la kwanza, Kichuya tena alifanya mambo ya kuitanguliza Simba kwa bao la dakika ya 57 kabla ya Obrey Chirwa kuisawazishia Yanga dakika tatu baadaye.
Kwa mazingira yaliyopo kwa winga huyo ni nafasi yake ya kuandika rekodi hiyo mpya kama ambavyo nyota wenzake, John Bocco na Emmanuel Okwi walivyo na kibarua cha kuvunja rekodi ya hat trick ya mechi ya watani inayoshikiliwa na Abdallah Kibadeni.
King Kibadeni aliandikisha rekodi hiyo iliyodumu kwa zaidi ya miaka 40 sasa katika pambano la kihistoria la watani lililopigwa Julai 19, 1977 wakati Simba ikiitambia Yanga kwa mabao 6-0, huku yeye akifunga matatu na mengine mawili yakiwekwa kimiani na Jumanne Hassan 'Masimenti' na beki wa Yanga Selemani Sanga alijifunga.
Pambano hilo la watani ambalo litakuwa la 100 tangu klabu hizo kongwe zianze kukutana katika mechi za Ligi ya Bara, inasubiri kuona rekodi mbalimbali zikivunjwa ikiwamo ya matokeo ya kipigo kikubwa ama sare ya maajabu zilizowahi kuwekwa 1996 na 2003 timu hizo zilipofungana mabao 4-4 na 3-3 mtawalia bila kutarajiwa.

Wednesday, March 21, 2018

CAF yaipa Yanga Wahebeshi Kombe la Shirikisho Afrika

WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya CAf, Yanga imepangwa kuvaana na Wolayta Dicha ya Ethiopia katika mechi za kuwania kutinga makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga itaikaribisha Dicha kati ya Machi 6-8 kabla ya kuwafuata ugenini katika mchezo wa marudiano.
Katika droo iliyofanyika muda mfupi uliopita wababe wa Simba, Al Masry wenyewe wamepangwa kuvaana na Moumana ya Gabon.

Droo ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika mubashara

Yanga walipangwa kuvaana na Wolaita Dicha ya Ethiopia
https://www.pscp.tv/CAF_Online/1yNxakeLkRdGj?t=37m2s

Saturday, January 6, 2018

Cheki Ratiba, Msimamo wa Kombe la Mapinduzi 2018

RAHIM JUNIOR
BAADA ya mechi za jana za makundi ya Kombe la Mapinduzi, cheki ratiba na msimamo wa michuano hiyo inayozidi kushika kasi visiwani Zanzibara na itakayofikia tamati Januari 13 ambapo bingwa wa mwaka huu atafahamika.
Kwa sasa Azam ndio wanaoshikilia taji hilo baada ya kuipokonya Simba katika fainali za mwaka jana. Timu hizo zitakutana tena katika mechi kali itakayopigwa usiku wa leo kwenye Uwanja wa Amaan, Unguja.

RATIBA:

Leo Jumamosi
JKU v Singida United
Simba v Azam

Kesho Jumapili

Zimamoto v Yanga

Jumatatu

Simba v URA
Yanga v Singida United

Jumatano, Jan 10, 2018
NUSU FAINALI

Kinara Kundi A v
Mshindi wa Pili Kundi B

Kinara Kundi B v
Mshindi wa Pili Kundi A
Saa 2:15 usiku

Jan 13, 2018
FAINALI

Saa 2:15 usiku

Msimamo:

Kundi A
               P    W    D    L    F    A    Pts
1.Singida  3    3    0    0    9    3    9
2.Yanga    3    3    0    0    5    1    9
3.M'ndege 5    2    0    3    5    7    6
4.Taifa      5    1    1    3    3    7    4
5.JKU       4    1    1    2    2    3    4
6. Z'moto 3    1    0    2    3    4    3

Kundi B
               P    W    D    L    F    A    Pts
1.URA      3    2    1    0    3    1     7
2.Azam    3    2    0    1    6    1    6
3.Simba   2    1    1    0    4    1    4
4.Mwenge4    1    1    2    2    4    4
5.Jamhuri4    0    1    3    2    9    1


Dk Mwakyembe azindua tamthilia zitakazorushwa DStv, Maisha Magic Bongo

Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice-Tanzania, Maharage Chande (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Habari, Utamadunia, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe kabla ya uzinduzi wa tamthilia mbili jana usiku Mlimani City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu, Joyce Fisoo.
MWANDISHI WETU
WASANII wametakiwa kufaidika na kazi zao za sanaa, ambapo Serikali pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, wako tayari kuwasaidia.
Waziri aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Sarafu na Kampuni, ambazo zitaoneshwa na kisimbuzi cha DStv.
Tamthilia hizo zitakuwa zikionekana kupitia chaneli ya Maisha Magic Bongo ili kuwapa burudani zaidi wateja wa DStv.
Mwakyembe alisema kuwa amefurahishwa na kiwango cha hali ya juu kilichooneshwa katika tamthilia hizo mpya, ambazo zote zimebuniwa na kutengenezwa hapa nchini na waigizaji wake, wahariri na waongozaji wote ni Watanzania.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harishon Mwakyembe (katikati) akiwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fisoo (wa pili kulia), Mtendaji Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mwuingereza (kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Maharage Chande (wa pili kushoto) na Mbunge wa Makete Prof. Norman Sigalla King wakifuatilia kwa makini tamthilia mpya za Kitanzania – SARAFU na KAPUNI 
Pia amewaasa wasanii kuhakikisha kuwa wanazingatia maadili ya jamii wakati wote wanapofanya kazi zao za sanaa, kwani sanaa ni kioo cha jamii na kwamba ikitumika vibaya inaweza kuwa na athari mbaya kwa jamii yetu.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice-Tanzania, Maharage Chande alisema Kapuni ni tamthilia iliyojaa vituko na misukosuko, ambavyo ni kivutio kwa watazamaji. Alisema Kapuni imeandaliwa na muandaaji maarufu wa filamu nchini, Leah Mwendamseke na vituko na misukosuko ya mahusiano na usaliti wa kimapenzi.
Tamthilia hizo zitaanza kurushwa hewa kuanzia wiki ijayo katika DStv chaneli 160 – Maisha Magic Bongo.
Tamthilia hiyo imechezwa na waigizaji maarufu akiwemo, Jacqueline Wolper, Gabo, Kajala, Masanja, Jenifer Kyaka (Odama),
Mwanamuziki Quick Rocka, DJ maarufu Rommy Jones na mastaa wengine wengi. 

Wasanii mbalimbali wa tasnia ya filamu hapa nchini wakifuatilia kwa makini tamthilia mpya za Kitanzania – SARAFU na KAPUNI zitakazoonekana katika chanel ya Maisha Magic Bongo kuanzia mwezi huu wakati wa uzinduzi wa tamthilia hizo jana katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Tamthilia hizo zimeigizwa na wasanii maarufu kama Jacquline Wolper, Gabo, Kajala, Mwanamuziki Quick Rocka, Mohammed Funga Funga ( Mzee Jengua), Irene Uwoya, Idris Sultan na wengineo.
Chande aliongeza kusema kuwa tamthilia ya Sarafu iliyoandaliwa na John Samwel Isike, nayo ni maridadi iliyobeba marafiki wawili ambao wanaingia kwenye chuki na uadui mkubwa mpaka kuingiza familia zao kwenye hatari, kisa ni fedha zinazozaa kiburi, dharau na anasa za kupitiliza.
Waigizaji maarufu akiwemo Mohammed Funga Funga ( Mzee Jengua), Mzee Chilo, Elizabeth Michael (Lulu), Hemed Suleiman, Irene Uwoya, Idris Sultan, Yusuph Mlela na mastaa wengineo wamo kwenye tamthilia hiyo.
DStv kupitia chaneli yake mahsusi ya maudhiu ya Kitanzania ya Maisha Magic Bongo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa tasnia ya Sanaa inakua na kuifanya iwe moja ya vyanzo muhimu vya mapato kwa wasanii na hatimaye kuchangia katika uchumi wa nchi yetu.
Chanel ya Maisha Magic Bongo ilianzishawa tarehe 1 Octoba 2015, kwa lengo kuu la kuinua na kukuza vipaji na Sanaa hapa Tanzania na pia kuongeza maudhui ya kitanzania kwa wateja wa DStv.
Kwa kipindi chote hiki Chanel hii imekuwa kwa haraka sana, ambapo kwa sasa ni miongoni mwa Channel zenye watazamaji wengi zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki. Channel hii imekuwa kitovu cha maendeleo ya wasanii hapa nchini, huku mamia ya wasanii wakipata fursa mbalimbali kutokana na kazi zao kurushwa katika channel hii na pia kupata mafuzo na kipato kupitia Sanaa.
Kwa upande wa tasnia ya filamu na uigizaji, Maisha Magic Bongo imeleta mapinduzi makubwa na miongoni mwa filamu zinazotikisa katika soko kwa sasa ni pamoja na Tamthila ya HUBA,ambayo ilipokelewa vizuri sana na Watanzania, pia kuna filamu na vipindi vingine kama MWANTUMU, HARUSI YETU, KITIMTIM ambazo zote zinazidi kuwa maarufu kila uchao.
Kuingizwa kwa tamthilia mpya za Kapuni na Sarafu, nu muendelezo wa mkakati wa Chaneli hii kuongeza maudhui ya kitanzania, na kuwapa watanzania burudani inayoendana na wakati na yenye kuakisi maisha halisi ya kitanzania.
Credit:MLEKANI

Wenger apewa kibano, kisa kumkoromea refa

Kiocha Arsene Wenger akikoromeana na mwamuzi
LONDON, England
MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya Pauni 40,000 kwa kumtolea maneno makali refa kwenye chumba cha kubadilishia nguo baada ya mchezo dhidi ya West Bromwich Jumapili iliyopita.
Kocha huyo alifanya kitendo hicho baada ya kukasirikia kitendo cha mwamuzi huyo Mike Dean kuwazawadia The Baggies penalti ya dakika ya mwisho baada ya mpira uliopigwa na Kieran Gibbs kumfikia mkononi Calum Chambers.
Alimfuata Dean baada ya mechi na kuanza kumtolea maneno ya kulaumu uamuzi wake baada ya Jay Rodriguez kufunga penalti hiyo kuipatia timu yake sare ya 1-1.
Wenger alifunguliwa mashitaka na Chama cha Soka England mapema wiki hii na sasa atakosekana kwenye mechi ya Raundi ya Tatu Kombe la FA dhidi ya Nottingham Forest Jumapili na mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Carabao dhidi ya Chelsea.

Liver, Man Utd watakata, Lukaku, Virgil watupia

Virgil akishangilia bao lake
Lukaku akishiangilia bao akiwa na Lingard
Man United wakipongezana

Liverpool wakipongezana
MANCHESTER, England
MANCHESTER United imeendelea kugawa dozi baada ya usiku wa kuamkia leo kuitungua Derby Count kwa mabao 2-0, huku LIverpool wakiitoa nishai Everton kwa kuichapa mabao 2-1 katika mchezo mwingine mkali wa michuano hiyo.
Romelu Lukaku aliifungia Man United bao la pili dakika ya 90 huku Jesse Lingard akitupia kambani bao la kuongoza dakika ya 84 katika mechi kali iliyopigwa Uwanja wa Old Trafford.
Katika pambao jingine Liverpool ikiwa uwanja wa nyumbani wa Anfield iliitandika wapinzani wao wa jadi Everton kwa mabao 2-1 na kuing'oa kwenye michuano hiyo.
Beki wa Liverpool, Mholanzi Virgil van Dijk akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Wenyeji walitangulia kufunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti kupitia James Milner dakika ya 34 kabla ya Gylfi Sigurosson kuisawazisha Everton katika dakika ya 65 na kwenye dakika ya beki mpya wa Liverpool, Virgil van Dijk alitupia kambani bao la ushindi dakika sita kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Ushindi huo umeifanya Liverpool kuungana na Man United kutinga Raundi ya Nne ya michuano hiyo na leo Jumamosi na kesho Jumapili michezo mingine kibao itapigwa katika mfululizo wa michuano hiyo mikongwe nchini England.

Yanga hiyooo, Simba, Azam mechi ya kisasi

Azam FC itakayovaana na Simba usiku wa leo
Simba watakaokuwa na kibarua mbele ya watetezi wa Mapinduzi, Azam FC

Yanga waliotangulia nusu fainali ya Mapinduzi usiku wa jana
RAHIM JUNIOR
WAKATI Simba usiku huu ikishuka uwanjani katika mechi ya kisasi dhidi ya Azam, watani zao usiku wa kuamkia leo wametangulia nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi wakiungana na Singida United.
Singida inayoongoza Kundi A ikiwa na alama 9 sawa na Yanga ila ikiwa na faida ya mabao ya kufungwa na kufungwa, itashuka tena uwanjani jioni ya leo kuvaana na JKU katika pambano jingine linalotarajiwa kuwa kali itakayochezwa Uwanja wa Amaan mjini Unguja.
Maafande wa JKU wataivaa Singida ikiwa inauguza kidonda cha kutunguliwa bao 1-0 na Yanga katika mechi yao iliyopita na itakuwa ikikamilisha ratiba tu kwani hata kama itaifunga Singida itafikisha pointi 7 ambazo zimeshapitwa na wapinzani wao.
Yanga ilitinga nusu fainali baada ya kuifunga Taifa Jang'ombe kwa mabao 2-0, mabao yaliyowekwa kimiani katika vipindi vyote. La kwanza likifungwa na Ibrahim Ajib dakika chache kabla ya mapumziko na jingine la Yohana Mkomola kwenye dakika ya 60 na kuifanya Yanga kukata tiketi ya kucheza nusu fainali ikiwa na michezo miwili mkononi dhidi ya Zimamoto na Singida United zitakazopigwa kati ya kesho Jumapili na Jumatatu mtawalia.
Hata hivyo Yanga na Singida zikitangulia mapema nusu fainali, wapinzani wao Simba watakuwa na kibarua kizito usiku wa leo kwa kuvaana na Azam katika mechi ya kisasi na inayorejesha kumbukumbu ya fainali ya michuano iliyopita.
Simba ilicharazwa na Azam kwa bao 1-0 katika fainali ya mwaka jana ya michuano hiyo na kuwaacha matajiri hao wa Chamazi wakibeba taji kwa mara ya tatu wakifikia rekodi ya Wekundu wa Msimbazi.
Mchezo wa leo ni vita baada ya Azam jana kulala 1-0 mbele ya URA wanaoongoza kundi lao la B na ushindi pekee ndio utakawanusuru wasiliteme taji hilo la sivyo itawaacha Simba wakiungana na Waganda kucheza hatua hiyo itakayoanza Januari 10.
Simba kupitia Kocha wake, Masudi Djuma imetamba kukata tiketi hiyo kwa sababu imepanga mwaka huu kubeba kila taji baada ya kutemeshwa taji lao la Kombe la FA na timu ya Green Warriors iliyopo Ligi Daraja la Pili (SDL).
Simba ipo nafasi ya tatu nyuma ya URA na Azam ikiwa na alama nne baada ya kupata sare moja na kushinda mchezo mwingine wa mwisho na kama itaichapa Azam, licha ya kulipa kisasi cha mwaka jana, lakini itafuzu nusu fainali.
Watetezi ambao walipoteza mchezo wao wa kwanza msimu huu na kufungwa bao la kwanza katika Mapinduzi tangu mwaka jana walipobeba taji bila kupoteza wala kufungwa bao, imetamba tiketi yao ya nusu fainali wanayo Simba na lazima wawape. Ngoja tuone itakavyokuwa baada ya kipyenga cha mwisho usiku wa leo.

Friday, January 5, 2018

Dk 70 Yanga bado ipo mbele ya kwa mabao 2-0


AJIB anakosa bao la wazi dakika ya 70, matokeo bado ni yale yale, Yanga inaongoza mabao 2-0. Pambano ni kali kwelikweli Uwanja wa Amaan.

Mkomola anaiandikia Yanga bao la pili

Yohana Mkomola
STRAIKA Yohana Mkomola ameiandikia Yanga bao la pili muda mfupi uliopita kutokana na uzembe wa mabeki wa Taifa. Yanga 2 Taifa 0. Dakika ya 63.

Dakika ya 60 matokeo bao 1-0 Yanga inaongoza

Kikosi cha Yanga
PAMBANO la Yanga na Taifa linaendelea kwenye Uwanja wa Amaan, Unguja na mpaka sasa matokeo bado yakiwa ni bao 1-0, Yanga ikiendelea kuongoza.

Simba kazi wanayo kwa Azam

Kocha Masudi Djuma akimkumbatia nahodha msaidizi, Mohammed Hussein 'Tshabalala', huku aliyekuwa Kocha Mkuu Joseph Omog na Mratibu, Abbas Ali wakishuhudia
Wachezaji wa Simba wakijifua mazoezini

RAHIM JUNIOR
HAKUNA namna ila kushinda tu. Ndivyo ambavyo Simba inapaswa kufanya wakati kesho Jumamosi itakaposhuka Uwanja wa Amaan, mjini Unguja kupepetana na Azam katika mechi ya kisasi itakayoamua hatma yao ya kutinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani hapa.
Simba ambayo ilipata ushindi wa kishindo usiku wa jana kwa kuikandika Jamhuri Pemba kwa mabao 3-1, itavaana na Azam usiku wa kesho na timu yoyote ikishinda itajihakikishia nafasi ya kutinga nusu fainali na kusubiri kujua itaungana na nani.
Azam inayotetea taji hilo ililolipata mwaka jana kwa kuichapa Simba kwa baoa 1-0 katika fainali, huo utakuwa ni mchezo wao wa mwisho na kwa sasa ikiwa na alama sita baada ya mechi tatu, kutokana na kupigwa 1-0 jioni ya leo na URA ya Uganda.
Simba yenyewe ipo nafasi ya tatu katika Kundi B ikiwa na alama nne baada ya mechi mbili, huku URA wakiongoza msimamo na pointi zao saba baada ya mechi tatu. Pambano la mwisho la Waganda hao litakuwa ni dhidi ya Simba  litakalopigwa Jumatatu jioni.
Hata hivyo Simba chini ya Kocha, Masudi Djuma imeonyesha kuwa na mabadiliko makubwa kulinganisha na ilipokuwa chini ya Mcameroon, Joseph Omog aliyetimuliwa na kama itacheza kama ilivyocheza mechi yao iliyopita, Azam ni lazima ijipange kwa Vijana hao wa Msimbazi.
Mrundi huyo aliyewapa taji Rayon Sports ya Rwanda, anatarajiwa kuendelea kumtegemea nahodha wake, John Bocco 'Adebayor' kuongoza mashambulizi akisaidiana wa nyota wengine, huku beki kiraka, Asante Kwasi aliyetupia kambani jana katika mechi yake ya kwanza akiwa na uzi wa Simba akitarajiwa kufanya yake.
Kwasi alisajiliwa na Simba hivi karibuni akitokea Lipuli na ameanza kuonyesha makeke yake na kuwafanya mashabiki wa Simba kutabasamu kwa kuamini kuwa timu yao inazidi kunoga, ikiwa siku chache tangu watolewa na kutemeshwa taji la Kombe la FA kwa kufungwa na timu ya Daraja la Pili, Green Warriors.
Azam iliyokuwa haijafungwa bao lolote katika michuano hiyo tangu mwaka jana walipobeba taji bila kupoteza, sio ya kubeza kwanui ukuta wake unaoongozwa na Mghana, Yakubu Mohammed na safu kali ya ushambuliaji chini ya Mghana mwingine, Bernard Arthur na chipukizi Paul Peter na Zayd na Shaaban Idd huenda isikubali kirahisi kupoteza mchezo huo na kutemeshwa taji la michuano hiyo.
Mbali na mchezo huo mapema jioni Singida United itakuwa uwanjani kupepetana na JKU katika mechi nyingine.

Ajibu atupia kambani, Yanga 1-0 Taifa Jang'ombe

RAHIM JUNIOR
IBRAHIM Ajib ameitanguliza Yanga mguu mmoja kwenye nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuifungia bao la kuongoza dakika chache kabla ya kwenda mapumziko akimalizia mpira wa shuti kali ha Yohana Nkomola kuokolewa na kipa wa Jang'ombe.
Kwa sasa pambano hilo lipo mapumziko na kama matokeo yatasalia hivyo, basi Yanga itaifuata Singida United iliyotangulia mapema leo mchana kwa kuilaza Mlandege.
Katika mchezo wa leo unaochezwa Uwanja wa Amaan usiku huu, Yanga imechezesha kikosi cha vijana zaidi, huku wakongwe kama kina Youthe Rostand, Nadir Haroub 'Cannavaro', Amissi Tambwe, Papy Kabamba Tshishimbi wakiwa jukwaani.

Chirwa apigwa stop, Kocha Mbao ala kibano

Obrey Chirwa
Kocha wa Mbao, Etienne Ndayiragije
RAHMA WHITE
MZAMBIA Obrey Chirwa ambaye ameididia klabu ya Yanga kucheza na kutimkia kwao Zambia, amesimamishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuitimulia timu yake kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu.
Chirwa ameasimamiwa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi maarufu kama Kamati ya Saa 72 iliyokutana jana Alhamisi na kujadili mechi mbalimbali za Ligi Kuu (VPL) Daraja la Kwanza (FDL) na Daraja la Pili (SDL).
Soma maamuzi ya kamati hiyo na adhabu zake katika ligi hizo;

LIGI KUU YA VODACOMMechi namba 72 (Mbeya City 0 vs Simba 1).Kamishna wa mechi hiyo Billy Mwilima amepewa Onyo Kali kwa kuruhusu mchezaji Hamisi Msabila wa Mbeya City kucheza mechi bila kuonyesha leseni, hivyo kukiuka Kanuni ya 14(16 na 17) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. 
Mechi namba 81 (Ndanda 1 vs Njombe Mji 1). Klabu ya Ndanda imepigwa faini ya sh 500,000 (laki tano) kwa kutowasilisha orodha ya wachezaji wake (team match list) kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre- match meeting) kama ilivyoainishwa katika Kanuni ya 14(2k) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu dhidi ya Ndanda katika mechi hiyo iliyofanyika Novemba 24, 2017 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Pia Kamati imeiomba Sekretarieti ya Bodi ya Ligi kutoa Waraka mwingine kwa klabu kuzikumbusha kuhusu kutoa orodha ya wachezaji kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting).
Mechi namba 83 (Yanga 1 vs Tanzania Prisons 1). Tanzania Prisons imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.
Adhabu dhidi ya Tanzania Prisons katika mechi hiyo iliyochezwa Novemba 25, 2017 Uwanja wa Azam Complex ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Wachezaji Lambart Sabiyanka wa Tanzania Prisons na Obrey Chirwa wa Yanga wamesimamishwa kwa kuzingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kutokana na kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu, wakisubiri malalamiko dhidi yao kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF.
Pia Kamati imeiomba TFF iipatie Bodi ya Ligi uamuzi (ruling) wa Kamati ya Nidhamu juu ya mchezaji wa Yanga kusimamishwa baada ya mechi dhidi ya Mbao FC wakati akisubiri mashtaka yake ili kuufanyia kazi kwa ajili ya mapendekezo ya marekebisho ya Kanuni.
Mechi namba 84 (Mbao 1 vs Mwadui 0). Klabu ya Mbao FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuruka uzio wa ndani na kwenda kushangilia katika eneo lisiloruhusiwa katika mechi iliyochezwa Novemba 25, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Adhabu dhidi ya Mbao FC ni uzingativu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 90 (Lipuli 0 vs Tanzania Prisons 1).Mtunza Vifaa wa Lipuli FC, George Mketo amesimamishwa akisubiri suala lake la kuwatukana waamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 30, 2017 Uwanja wa Samora mjini Iringa kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Mechi namba 94 (Mbao 2 vs Yanga 0). Kocha wa Mbao FC, Etiene Ndayiragije amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuondolewa kwenye mchezo (ordered off) na Mwamuzi kwa kushindwa kuheshimu taratibu na kuonywa mara tatu.
Adhabu hiyo dhidi ya Kocha Ndayiragije katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 31, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(11) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Pia klabu ya Mbao FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(10) kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 96 (Mwadui 2 vs Ruvu Shooting 1).Klabu ya Mwadui imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo iliyochezwa Januari 1, 2018 Uwanja wa Mwadui Complex. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 42(10) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu

LIGI DARAJA LA KWANZAMechi namba 37 Kundi B (JKT Mlale 1 v Mufindi United 0). Klabu ya Mufindi United imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na Kiongozi wake Hussein Turuka kutoa lugha chafu kwa Mwamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 31, 2017 mjini Songea. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 40 Kundi B (Mawenzi Market 1 v Polisi Dar 0). Klabu ya Mawenzi Market imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kutaka kuwapiga waamuzi na kuwashawishi ball boys kuchukua mipira iliyotoka nje na kuwapelekea jukwaani.  Adhabu hiyo katika mechi hiyo iliyochezwa Desemba 31, 2017 ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Pia Kocha Mkuu wa Mawenzi Market amepewa Onyo Kali kwa kuchelewa kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre-macth meeting) kwa dakika saba. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo.
Mechi namba 39 Kundi C (Dodoma FC 3 v Alliance Schools 2). Klabu ya Alliance Schools imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa timu yake kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 30, 2017 mjini Dodoma. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(10) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mchezaji Shaban William wa Alliance Schools amesimamishwa, hadi suala lake la kumpiga Mwamuzi litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Waamuzi wote wanne; Andrew Shamba, Abdallah Mkomwa, Athuman Athuman na Omari Juma wamefungiwa miaka mitatu kila mmoja kwa kuchezesha mechi hiyo chini ya kiwango. Adhabu dhidi ya waamuzi hao imezingatia Kanuni ya 38(1a) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.
Pia Kamishna wa mechi hiyo Mackshem T. Nzunda amefungiwa miaka mitatu kwa kushindwa kutoa taarifa ya mchezo kwa usahihi. Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 39(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Kamishna.
Kamati imeomba suala la waamuzi hao ambao baadhi yao ni wa Ligi Kuu, kupitia TFF liwasilishwe kwenye chombo chenye dhamana ya kisheria ya rushwa kufanyiwa uchunguzi zaidi.

LIGI DARAJA LA PILIMechi namba 18 Kundi B (Africans Sports 1 v Kitayosce 2). Kitayosce imepigwa faini ya sh. 50,000 (elfu hamsini) baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Taratibu za Mchezo.
Adhabu dhidi yao katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 29, 2017 jijini Tanga imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu taratibu za Mchezo.
Mechi namba 16 Kundi C (Mighty Elephant 1 v Green Warriors 3). Kocha wa Green Warriors, Azish Kondo amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) baada ya kuondolewa kwenye mchezo (ordered off) na Mwamuzi kwa kutumia lugha chafu.
Adhabu hiyo dhidi ya Kocha Kondo katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 29, 2017 mjini Songea imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(10) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Mechi namba 18 Kundi C (Mkamba Rangers 0 v Boma 1). Klabu ya Mkamba Rangers imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuingia uwanjani (pitch).  Adhabu hiyo katika mechi hiyo iliyochezwa Desemba 29, 2017 ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 16 Kundi D (Area C v Nyanza). Timu ya Nyanza FC imeshushwa madaraja mawili na matokeo ya michezo yako yote imefutwa kwa kutofika uwanjani bila kutoa sababu yoyote na kusababisha mechi yao dhidi ya Area C iliyokuwa ichezwe Desemba 29, 2017 mjini Dodoma isifanyike.
Uamuzi huo dhidi ya Nyanza FC umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 28(1) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Kutofika Uwanjani. Pia kwa mujibu wa Kanuni ya 28(2) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Kutofika Uwanjani, imepigwa faini ya sh. 2,000,000 (milioni mbili) ambapo sh. 1,000,000 (milioni moja) itachukuliwa na Bodi ya Ligi, na sh. 1,000,000 (milioni moja) italipwa timu pinzani.
Vilevile Kamati imeiomba Sekretarieti kukiandikia barua Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Manyara (MARFA) ili kujua tatizo la timu hiyo.

MVUVUMWA VS FRIENDS Kamati imeipa Friends Rangers ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya Mvuvumwa kuchezesha wachezaji ambao hawajasajiliwa (non qualified) katika mechi ya Kundi A Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya timu hizo iliyochezwa Oktoba 29, 2017. Mvuvumwa ilishinda mechi hiyo mabao 4-1.
Uamuzi huo dhidi ya Mvuvumwa umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(18) na 42(20) za Ligi Daraja la Kwanza. Nayo Friends Rangers imepewa ushindi kwa kuzingatia Kanuni ya 14(37) na ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo. 
Vilevile viongozi wa Mvuvumwa waliohusika kughushi leseni zilizotumiwa na wachezaji hao ambao hawakusajiliwa watafikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya TFF kwa ajili ya hatua zaidi.

ALLIANCE SCHOOLSKamati imepitia malalamiko ya Alliance Schools kupinga uchezeshaji wa Mwamuzi wa mechi yao dhidi ya Dodoma FC iliyofanyika Desemba 30, 2017 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Baada ya kupitia hoja zote, Kamati haikukubaliana na malalamiko hayo kwa vile hayakuwa na vielelezo wala kanuni za kuyathibitisha. Pia kwa suala la muda, Kamati imejiridhisha kuwa kazi ya kutunza muda ni ya Mwamuzi.