STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 6, 2018

Liver, Man Utd watakata, Lukaku, Virgil watupia

Virgil akishangilia bao lake
Lukaku akishiangilia bao akiwa na Lingard
Man United wakipongezana

Liverpool wakipongezana
MANCHESTER, England
MANCHESTER United imeendelea kugawa dozi baada ya usiku wa kuamkia leo kuitungua Derby Count kwa mabao 2-0, huku LIverpool wakiitoa nishai Everton kwa kuichapa mabao 2-1 katika mchezo mwingine mkali wa michuano hiyo.
Romelu Lukaku aliifungia Man United bao la pili dakika ya 90 huku Jesse Lingard akitupia kambani bao la kuongoza dakika ya 84 katika mechi kali iliyopigwa Uwanja wa Old Trafford.
Katika pambao jingine Liverpool ikiwa uwanja wa nyumbani wa Anfield iliitandika wapinzani wao wa jadi Everton kwa mabao 2-1 na kuing'oa kwenye michuano hiyo.
Beki wa Liverpool, Mholanzi Virgil van Dijk akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Wenyeji walitangulia kufunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti kupitia James Milner dakika ya 34 kabla ya Gylfi Sigurosson kuisawazisha Everton katika dakika ya 65 na kwenye dakika ya beki mpya wa Liverpool, Virgil van Dijk alitupia kambani bao la ushindi dakika sita kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Ushindi huo umeifanya Liverpool kuungana na Man United kutinga Raundi ya Nne ya michuano hiyo na leo Jumamosi na kesho Jumapili michezo mingine kibao itapigwa katika mfululizo wa michuano hiyo mikongwe nchini England.

No comments:

Post a Comment