STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 13, 2013

Offside Trick sasa watoa Talaka hadharani

Mmoja wa wanaounda kundi la Offside Trick, Hammer Q
KUNDI maarufu la miondoko nya mduara, Offside Trick la visiwani Zanzibar, limeachia wimbo mpya uitwao 'Talaka' ikiwa ni siku chache tangu waachie video ya wimbo wao wa 'Nipe Nikupe waliomshirikisha Mzee Yusuf.
Mmoja wa wasanii wanaounda kundi hilo, Hussein Mohammed 'Hammer Q', aliiambia MICHARAZO kuwa wameamua kutoa wimbo huo mpya kama zawadi kwa mashabiki wao katika kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2014.
Hammer Q alisema wimbo huo kama zilivyo nyimbo zao nyingine zipo katika miondoko hiyo ya mduara na wanafanya mipango kurekodi video yake.
"Baada ya kuachia video ya 'Nipe NIkupe' tuliyoimba na Mzee Yusuf, tumeachia wimbo mwingine mpya uitwao 'Talaka' ambao tumeimba sisi wenyewe Offsiede Trick bila kumshirikisha mtu wakati tukijipanga kufanya video yake," alisema Hammer.
Kundi hilo la Offside Trick linaundwa na wasanii wawili Said Amdani 'Lil Ghetto' na Hammer Q aliyeziba nafasi ya Mudi Chriss aliyepo masomoni.

CECAFA aibu tupu Kenya, kisa...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrmP5BiHFglkwvnrMibnq4AQ_aSqD4vOZa3Us2aK3qsPI4i33h2ONpSixBBlFDMyvtVKIpZsLStp8DY33gYJkFK8qd8JKjm28hh3ukFyeOJ0v8FWAKq7CwnbInY-pMsB65SxD_huGIrnRp/s1600/CECAFA+Cup+2013+b.jpg
Na Somoe Ng'itu, Nairobi
SHIRIKISHO la Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) na la Kenya (FKF) yamechafuka baada ya kushindwa kulipia malazi kwa wakati timu zinazoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji huku pia wakikumbwa na kashfa ya kutoa hundi 'feki'.
Licha ya mbwembwe za Kombe kupelekwa uwanjani kwa helikopta,
Timu ya Taifa ya Sudan ilichelewa kufika uwajani kutokana na uongozi wa Hoteli ya Milele kuwazuia wakitaka kulipwa kwanza fedha zao kutoka FKF.
Waamuzi waliochezesha mechi kati ya Kilimanjaro Stars na Zambia (Chipolopolo), pia uongozi wa Hoteli ya Mvuli House uliwazuia kwa muda kutoka ukidai kulipwa kwanza kwa gharama zao za malazi.
Wachezaji wa timu ya soka ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) jana walizuiwa na uongozi wa Hoteli ya The Strands iliyoko Nairobi West, kuondoka kutokana na deni la Sh.milioni 5.5 za Kenya.
Uongozi wa hoteli hiyo kwa kutumia askari wake iliwazuia wachezaji wa Zanzibar Heroes kuondoka hotelini hapo hadi watakapolipwa fedha wanazoidai FKF.
Wachezaji hao ambao timu yao ilitolewa katika hatua ya makundi ya mashindano ya Kombe la Chalenji tangu Desemba 5, mwaka huu walishindwa kurejea kwao kutokana na kukosa tiketi za kurudia pamoja na kuzuiwa na wamiliki wa hoteli mpaka deni lao watakapolipwa na FKF.
Kutokana na vurugu zilizokuwa zinafanywa na wachezaji wa Zanzibar Heroes wakisisitiza  kuondoka iliwalazimu wamiliki wa hoteli hiyo kuwaita askari wengine wa Jeshi la Polisi la Kenya kwa ajili ya kuhakikisha amani inakuweao kwenye eneo hilo.
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, nahodha wa Zanzibar Heroes, Awadh Juma, alisema kwamba walipigiwa simu na Mwenyekiti wa FKF, Sam Nyamweya, jana saa 10:00 alfajiri akiwataka wajiandae ili waondoke na ndege ya saa tatu.
Juma alisema baada ya kujiandaa na kubeba mabegi yao saa 12 asubuhi jana, walikuta askari wamejaa kwenye geti wakiwaeleza hawaruhusiwi kuondoka mpaka FKF watakapolipa deni wanalowadai.
Habari kutoka ndani ya hoteli hiyo zilieleza kuwa FKF ilikuwa inadaiwa zaidi ya Sh. milioni 20 za Kenya ambazo ni gharama za kuihudumia timu hiyo pamoja na kikosi cha Nigeria (Super Eagles) kilichokaa hapo wakati kimekuja nchini hapa kuikabili Harambee Stars mapema mwaka huu.
Hata hivyo, FKF ililipa nusu ya deni hilo na ilidaiwa pia kutoa hundi feki ya Sh. milioni 5.5  za Kenya jambo ambalo liliwaudhi wamiliki wa hoteli hiyo.
Saa 3: 20 asubuhi Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye, alifika katika hoteli hiyo ili kuanza mazungumzo na wamiliki wa hoteli hiyo lakini hakufanikiwa mpaka pale alipoamua kumuita Nyamweya.
Saa 4:44 Nyamweya alifika katika eneo la tukio kuendelea na mazungumzo lakini kilichoafikiwa ni uongozi wa hoteli kuhitaji fedha zao ndiyo iwaruhusu wachezaji wa Zanzibar Heroes waondoke.
Hata hivyo, wachezaji wa Zanzibar Heroes waligoma kumruhusu Nyamweya kuondoka kwenye hoteli hiyo na kulazimisha waruhusiwe kuondoka na ikiwezekana wakalale hata uwanja wa ndege na si kubaki hotelini hapo.
Kocha Mkuu wa Zanzibar Heroes, Salum Bausi, alilazimika kufanya maamuzi magumu ya kuwataka wachezaji wake wawe wavumilivu na kumruhusu Nyamweya aondoke na kuongozana na mwakilishi wa hoteli kwenda kulipwa fedha wanazodai.
Saa  6:12 mchana Nyamweya na wenzake pamoja na Musonye waliondoka hotelini hapo na kuelekea benki ili kukamilisha zoezi hilo na kuwaeleza wachezaji kwamba wataondoka leo kurejea Tanzania.
Mbali na Zanzibar Heroes, pia wachezaji wengine wa timu ya Sudan Kusini ambao nao walitolewa kwenye hatua ya makundi walilazimika kujilipia wenyewe tiketi za kurudi nyumbani.
NIPASHE

KMKM kutua leo jioni kuivaa Yanga na Simba Taifa wikiendi hii

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi59R0MYcrxWHLeSNnC_vM50rvpo6pW4S079-xz073BM1qMzHu78BZ3M2A6-Rcffg0AKuCNlGJTx77XuEspNUQTYpSZxeIwClivBXmTswWbLyuGBKDZoXuu3mnXKpUwrCIZ62qjbxpxVhkw/s640/4.jpg
Kikosi cha KMKM kitakachotua leo Dar kuumana na Simba na Yanga mwishoni mwa wiki
TIMU ya KMKM ya Zanzibar inatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam jioni ya leo  ikitokea visiwani Zanzibar kwa ajili ya kucheza mechi za kirafiki na Yanga na Simba, ambapo katika mechi ya kesho dhidi ya Yanga kiingilio cha chini kabisa ni sh.5,000.
Kwa mujibu wa mratibu wa mechi hiyo George Wakuganda alisema, timu hiyo itawasili jioni kwa Boti ya kwenda Kasi ikiwa na kikosi kamili na mechi ya kwanza ni kati ya Yanga na KMKM Uwanja wa Taifa,Dar es Salaam, huku Simba wakicheza keshokutwa katika uwanja huo huo.
Alisema vingilio kwa VIP A ni sh.20,000, VIP B sh.15,000, VIP C sh.10,000, orange sh.7,000 , bluu na kijani viingilio ni sh.5,000.
"Tunaamini kwa kipindi hiki kirefu ambacho timu zilikuwa mapumzikoni, wachezaji watarudi na kitu kipya uwanjani ikiwa na makocha kuwatambulisha wachezaji wao wapya," alisema Wakuganda
Kwa upande wa kocha wa Yanga Ernest Brandts alisema anaimani kabisa mechi hiyo itampa mwanga kuelekea mechi hiyo na wapinzani wao Simba, hivyo anazidi kuwanoa wachezaji wake ili wawe fiti zaidi.
"Naamini KMKM sio timu mbaya hasa kipindi hiki ambacho timu yangu inajiandaa na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara, hivyo kwa kiasi kikubwa itanisaidia kujenga kikosi changu," alisema kocha huyo.
Alisema pia mechi hiyo atawatumia wachezaji wake wapya kipa Juma Kaseja na kiungo Hassan Dilunga ambao wamesajiliwa kipindi hiki cha dirisha dogo kwa ajili ya kuongeza nguvu katika kikosi chake.
Kocha huyo alisema wachezaji wake wote wapo fiti ukiondoa wale ambao wapo kwenye timu zao za Taifa, waliomo kwenye michuano ya Kombe la Challenji ambayo inamalizika leo nchini Kenya.
Alisema mechi hiyo imekuja kipindi kizuri kwa kuwa wachezaji wake walikuwa mapumziko, hivyo hata wakivaana na Simba atakuwa amejua wapi kuna mapungufu katika kikosi chake kabla ya mechi hiyo ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini.
Hata hivyo kocha huyo alisema wachezaji waliomo kwenye timu za Taifa, hana uhakika kama watacheza mechi hiyo kwa kuwa siku ya mechi ndio wanatua nchini wakitokea Nairobi, Kenya.

Golden Bush Veterani kuzivaa Kilwa Veterani, Mwana United Dar


BAADA ya kufanikiwa kuwasambaratisha KMKM Vetereani nyumbani visiwani Zanzibar, wakali wa soka la wazee jijini Dar es Salaam wikiendi hii wanatarajia kushuka tena dimbani kuvaana na mateverani wenzao wa Kilwa na Mwanza United katika mechi za kuelekea pambano lao na watani zao Wahenga Fc.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Mlezi wa klabu hiyo inayoundwa na wanasoka nyota wa zamani na wale wanaoendelea kukipiga katika timu za Ligi mbalimbali nchini, Onesmo Waziri 'Ticotico', mechi hizo zitachezwa Jumamosi na Jumapili kwenye viwanja tofauti.
Ticotico alisema mechi ya kwanza itachezwa jioni kwenye uwanja wa TP Afrika uliopo Sinza, dhidi ya Kilwa Veterani na mechi itakayofuata itakuwa ya Jumapili kwa kiuwakabili Mwanza United.
 Taarifa yake kamili inasomeka kama ifuatavyo:
 
Wadau,
 
Wale Mabingwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watakuwa uwanjani tena weekend hii kama ifuatavyo:
 
Siku
Muda
Uwanja
Mechi
Jumamosi
1630hrs
TP
Golden Bush Veterans VS Kilwa Viterens
Jumapili
0800hrs
St James' Park
Golden Bush Veterans VS Mwanza United
 
Karibuni njooni muangalie soka la hali ya juu sana likitandazwa na Mabingwa wenu ikiwa ni sehemu mahususi kabisa ya maandalizi ya mechi yetu na Wahenga ambayo iko karibu sana.
 
Kwa kuzingatia hilo mechi zote zinazofuata sasa tutalazimika kutowatumia wachezaji wanaochezea Wahenga kwasababu tuko kwenye maandalizi ya mwisho mwisho kuandaa kikosi cha maangamizi siku ya kufunga mwaka.
 
Karibuni sana.
 
Onesmo Waziri

Ajali hii imetokea asubuhi hii Kimara-Korogwe

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo
MATUKIO ya ajali zinazohusu Pikipiki maarufu kama bodaboda yanaendelea kukithiri ambapo asubuhi ya leo eneo la Kimara mwendesha chombo hicho alijikuta akibamizwa na kuaachwa hoi yeye na abiria wake eneo la Kimara Korogwe.
Dereva huyo ambaye hakufahamika jina lake anadaiwa alikuwa akimpeleka abiria wake Ubungo kutokana na kero ya foleni katika barabara ya Morogoro na kujikuta wakiishia Hospitali baada ya kujeruhiwa huku pikipiki yake ikiwa imeharibika baada ya kugongwa na Fusso hilo lililokuwa likitokea mkoani kuja jijini Dar.
Pia katika ajali hiyo ilihusisha basi la wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo lilibamizwa kwa nyuma upande wa kulia na Fusso hilo na kuharibika huku ikielezwa baadhi ya abiria wa basi hilo dogo aina ya Toyota Coaster kujeruhiwa kidogo.

Neymar achekelea kuweka heshima Ulaya mapema zaidi

http://bostonherald.com/sites/default/files/styles/full/public/media/ap/d7a9ff3209aa48e190d014ef0569a8cf.jpg?c=612f6677417bc1fda3fcf6c08e08968f
Neymar akishangilia moja ya mabao yake matatu yaliyoizamisha Celtic juzi
BARCELONA, Hispania
NEYMAR amesema ameweka heshima Ulaya baada 'hat-trick' yake aliyofunga kuisaidia Barcelona kushinda 6-1 dhidi ya Celtic.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil alifunga magoli matatu ndani ya dakika 13 wakati Bara walipomaliza hatua ya makundi kwa ushindi mnono, huku Gerard Pique, Pedro na Cristian Tello wakifunga mabao mengine.
Barca waliingia katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Nou Camp wakiwa wamepoteza mechi mbili katika ya tatu zilizopita na Neymar alifarijika kwamba kikosi cha kocha Gerardo Martino kimerejea kushinda tena.
"Nina furaha - siyo tu kwa kufunga magoli matatu kwenye Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, ila pia kwa timu kushinda," alikaririwa na gazeti la Marca akisema.
"Sikuwa katika presha, lakini nilitaka kuweka heshima. Jambo muhimu ni kwamba tumeweza kuzipiku mechi zile mbili tulizopoteza na sasa ni lazima tubadili mitazamo yetu na kufikiria La Liga. "
Alipoulizwa kama anapenda kucheza katikati kuliko pembeni, alikataa kutoa maoni yake katika hilo, akisema anachohitaji ni kucheza tu.
"Napemda kucheza, sijali ni katikati ama pembeni," Neymar aliongeza.
Mechi ijayo ya Barca itakuwa ni ugenini dhidi ya timu ngumu ya Villarreal kesho baada ya kumaliza wakiwa vinara wa Kundi H la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Na tofauti ya mabao katika kipigo cha kwenye Uwanja wa Nou Camp imeifikia rekodi ya kufungwa 5-0 dhidi ya Artmedia Bratislava katika iliyokuwa mechi ya kwanza madarakani kwa kocha wa zamai Gordon Strachan mwaka 2005.
Celtic waliingia katika mechi hiyo wakiwa wamefunga jumla ya magoli 12 na hawajaruhusu hata moja katika mechi zao mbili za ligi zilizopita, wakati Barcelona walikuwa wamekula vipigo kutoka kwa Ajax na Athletic Bilbao.
Lakini Barca waliokuwa katika kiwango chao cha juu waliishushia Celtic kipigo chao cha 25 katika mechi 27 za ugenini za Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Hatimaye Ivo Mapunda akata mzizi wa fitina

Ivo Mapunda akiweka dole gumba katika mkataba wake na Simba mbele ya Katibu Mkuu wa Simba, Evodias Mtawala. (Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry)
HATIMAYE mzizi wa fitina juu ya kipa Ivo Mapunda kutua Simba au kuendelea kuidakia Gor Mahia umekatwa baada ya kipa huyo wa Kili Stars, kuamua kusaini mkataba wa miaka miwili usiku wa jana jijini Nairobi.
Ivo ambaye amekuwa gumzo nchini Kenya kwa umahiri wake wa kudaka na hasa kunyaka mikwaju ya penati, alisaini mkataba huo mbele ya Katibu Mkuu wa Simba, Evodias Mtawala na kukamilisha tetesi zilizokuwa zimezagaa za Mnyama kumnyakua kipa huiyo wa zamani wa Yanga na Prisons na African Lyon.
Mbali na Ivo, Simba imenyakua pia beki wa Gor Mahia, Donald Musoti ikiwa ni katika kujiimarisha kwa duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Januari 25.
Simba pia imenyakua kipa Yew Berko aliyekuwa akiidakika Yanga baada ya kutoridhishwa na kiwango cha kipa Abel Dhaira kutoka aUganda waliomsajili msimu huu.

Waliokufa ajali ya Burdan hawa hapa, majeruhi wengine hali tete

MAJINA ya abiria waliopoteza uhai katika ajali ya Basi la Burdan iliyotokea jana Kijiji cha Taula Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga yameanza kutajwa.
Ajali hiyo iliyotokana na basi hilo linalodaiwa kuwa katika mwendo kasi  na kupinduka mara kadhaa na kuacha na kujeruhi watu zaidi ya 70.
Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe walipopoteza maisha katika ajali hiyo wametambuliwa kuwa ni Dareva wa basi hilo, Luta Kundaeli Kimaro, Mama Ally mkazi wa eneo la Kwasamangube Korogwe, Joyce Mokiwa (36) mkazi wa NHC Korogwe na Rehema Mandondo ambaye ni mkazi wa kambi ya Maziwa.
Wengine waliokufa ni Msoke Mosha ambaye ni mwalimu wa Mgombezi Korogwe, Bashiri Shafii wa Kilole Korogwe, Bryton wa eneo la Lutheran Korogwe, Rehema Nassoro (23) mkazi wa Bagamoyo Kilole Korogwe, Agnes Linus mkazi wa Mandera na Mariamu Juma.