STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 13, 2013

Waliokufa ajali ya Burdan hawa hapa, majeruhi wengine hali tete

MAJINA ya abiria waliopoteza uhai katika ajali ya Basi la Burdan iliyotokea jana Kijiji cha Taula Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga yameanza kutajwa.
Ajali hiyo iliyotokana na basi hilo linalodaiwa kuwa katika mwendo kasi  na kupinduka mara kadhaa na kuacha na kujeruhi watu zaidi ya 70.
Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe walipopoteza maisha katika ajali hiyo wametambuliwa kuwa ni Dareva wa basi hilo, Luta Kundaeli Kimaro, Mama Ally mkazi wa eneo la Kwasamangube Korogwe, Joyce Mokiwa (36) mkazi wa NHC Korogwe na Rehema Mandondo ambaye ni mkazi wa kambi ya Maziwa.
Wengine waliokufa ni Msoke Mosha ambaye ni mwalimu wa Mgombezi Korogwe, Bashiri Shafii wa Kilole Korogwe, Bryton wa eneo la Lutheran Korogwe, Rehema Nassoro (23) mkazi wa Bagamoyo Kilole Korogwe, Agnes Linus mkazi wa Mandera na Mariamu Juma.

No comments:

Post a Comment