STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 13, 2013

Hatimaye Ivo Mapunda akata mzizi wa fitina

Ivo Mapunda akiweka dole gumba katika mkataba wake na Simba mbele ya Katibu Mkuu wa Simba, Evodias Mtawala. (Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry)
HATIMAYE mzizi wa fitina juu ya kipa Ivo Mapunda kutua Simba au kuendelea kuidakia Gor Mahia umekatwa baada ya kipa huyo wa Kili Stars, kuamua kusaini mkataba wa miaka miwili usiku wa jana jijini Nairobi.
Ivo ambaye amekuwa gumzo nchini Kenya kwa umahiri wake wa kudaka na hasa kunyaka mikwaju ya penati, alisaini mkataba huo mbele ya Katibu Mkuu wa Simba, Evodias Mtawala na kukamilisha tetesi zilizokuwa zimezagaa za Mnyama kumnyakua kipa huiyo wa zamani wa Yanga na Prisons na African Lyon.
Mbali na Ivo, Simba imenyakua pia beki wa Gor Mahia, Donald Musoti ikiwa ni katika kujiimarisha kwa duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Januari 25.
Simba pia imenyakua kipa Yew Berko aliyekuwa akiidakika Yanga baada ya kutoridhishwa na kiwango cha kipa Abel Dhaira kutoka aUganda waliomsajili msimu huu.

No comments:

Post a Comment