STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 13, 2013

Golden Bush Veterani kuzivaa Kilwa Veterani, Mwana United Dar


BAADA ya kufanikiwa kuwasambaratisha KMKM Vetereani nyumbani visiwani Zanzibar, wakali wa soka la wazee jijini Dar es Salaam wikiendi hii wanatarajia kushuka tena dimbani kuvaana na mateverani wenzao wa Kilwa na Mwanza United katika mechi za kuelekea pambano lao na watani zao Wahenga Fc.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Mlezi wa klabu hiyo inayoundwa na wanasoka nyota wa zamani na wale wanaoendelea kukipiga katika timu za Ligi mbalimbali nchini, Onesmo Waziri 'Ticotico', mechi hizo zitachezwa Jumamosi na Jumapili kwenye viwanja tofauti.
Ticotico alisema mechi ya kwanza itachezwa jioni kwenye uwanja wa TP Afrika uliopo Sinza, dhidi ya Kilwa Veterani na mechi itakayofuata itakuwa ya Jumapili kwa kiuwakabili Mwanza United.
 Taarifa yake kamili inasomeka kama ifuatavyo:
 
Wadau,
 
Wale Mabingwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watakuwa uwanjani tena weekend hii kama ifuatavyo:
 
Siku
Muda
Uwanja
Mechi
Jumamosi
1630hrs
TP
Golden Bush Veterans VS Kilwa Viterens
Jumapili
0800hrs
St James' Park
Golden Bush Veterans VS Mwanza United
 
Karibuni njooni muangalie soka la hali ya juu sana likitandazwa na Mabingwa wenu ikiwa ni sehemu mahususi kabisa ya maandalizi ya mechi yetu na Wahenga ambayo iko karibu sana.
 
Kwa kuzingatia hilo mechi zote zinazofuata sasa tutalazimika kutowatumia wachezaji wanaochezea Wahenga kwasababu tuko kwenye maandalizi ya mwisho mwisho kuandaa kikosi cha maangamizi siku ya kufunga mwaka.
 
Karibuni sana.
 
Onesmo Waziri

No comments:

Post a Comment