STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 13, 2013

Ajali hii imetokea asubuhi hii Kimara-Korogwe

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo

Bodaboda ikiwa chini ya Fusso lenye namba T961 BZF baada ya kugongwa eneo la Kimara asubuhi ya leo
MATUKIO ya ajali zinazohusu Pikipiki maarufu kama bodaboda yanaendelea kukithiri ambapo asubuhi ya leo eneo la Kimara mwendesha chombo hicho alijikuta akibamizwa na kuaachwa hoi yeye na abiria wake eneo la Kimara Korogwe.
Dereva huyo ambaye hakufahamika jina lake anadaiwa alikuwa akimpeleka abiria wake Ubungo kutokana na kero ya foleni katika barabara ya Morogoro na kujikuta wakiishia Hospitali baada ya kujeruhiwa huku pikipiki yake ikiwa imeharibika baada ya kugongwa na Fusso hilo lililokuwa likitokea mkoani kuja jijini Dar.
Pia katika ajali hiyo ilihusisha basi la wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo lilibamizwa kwa nyuma upande wa kulia na Fusso hilo na kuharibika huku ikielezwa baadhi ya abiria wa basi hilo dogo aina ya Toyota Coaster kujeruhiwa kidogo.

No comments:

Post a Comment