STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 28, 2012

Barclays Premier League | FIXTURES

Saturday 29 September 2012
ArsenalvChelseaEmirates Stadium13:45
EvertonvSouthamptonGoodison Park16:00
FulhamvMan CityCraven Cottage16:00
NorwichvLiverpoolCarrow Road16:00
ReadingvNewcastleMadejski Stadium16:00
StokevSwanseaBritannia Stadium16:00
SunderlandvWiganStadium of Light16:00
Man UtdvTottenhamOld Trafford18:30
Sunday 30 September 2012

Aston VillavWest BromVilla Park17:00

KOCHA MPYA YANGA AWASILI KIMYAKIMYA

Brandts

Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA mpya wa Yanga, Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts, beki wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi na klabu ya PSV Eindhoven ya Holanzi, atawasili wakati wowote kuanzia leo kusaini mkataba na kuanza kazi katika klabu hiyo.
Hata hivyo, Yanga imeamua kufanya siri ujio wa kocha huyo, kwa sababu haitaki mapokezi ya mbwembwe, kutokana na rekodi yake ya kutodumu na makocha.
Yanga, imetimiza malengo yake ya kuwa kocha mpya, kabla ya kucheza na wapinzani wao wa jadi, Simba SC, Oktoba 3, mwaka huu baada ya kumfukuza Mbelgiji, Tom Saintfiet, kutokana na kufikia makubaliano na Brandts.
Mholanzi huyo aliyefukuzwa APR ya Rwanda baada ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Agosti mwaka huu amepewa ukocha wa Yanga, baada ya Mbrazil Marcio Maximo kukataa nafasi hiyo kwa mara ya pili.
Mtaalamu huyo, alizaliwa Februari 3, mwaka 1956 mjini Nieuw-Dijk, Gelderland, mbali na PSV Eindhoven, alichezea pia Roda JC Kerkrade, MVV Maastricht na De Graafschap.
Brandts aliichezea mechi 28 timu ya taifa ya Uholanzi na kuifungia mabao matano na pia alicheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1978.
Katika fainali hizo, Raundi ya pili kwenye mechi na Italia, aliweka rekodi ya kuwa mchezaji pekee aliyezifungia mabao timu zote katika mechi moja kwenye fainali za Kombe la Dunia.
Alianza kujifunga dakika ya 18, kisha akaisawazishia Uholanzi dakika ya 50 katika mechi ambayo, mchezaji mwenzake Arie Haan baadaye aliifungia timu yake bao la ushindi na kutoka kifua mbele kwa mabao 2–1.
Alipostaafu soka akawa kocha na katikati ya msimu wa 2007–2008, Brandts aliambiwa hataongezewa mkataba NAC-Breda, licha ya matokeo mazuri ya kushika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu Uholanzi (Eredivisie), ingawa uamuzi huo haukuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo na nafasi yake akapewa Robert Maaskant kuanzia msimu wa 2008–2009.
Akateuliwa kuwa Kocha wa Rah Ahan mwaka 2009, kabla ya kufukuzwa Desemba 2009 na kuibukia APR ya Rwanda mwaka 2010, ambako ‘riziki’ yake imeisha miezi miwili iliyopita na sasa amepata maisha mapya Yanga.
Akiwa APR, Brandts alifungwa mechi zote mbili na Yanga iliyokuwa ikifundishwa na Mbelgiji Tom Saintfiet katika Kombe la Kagame, moja ya makundi 2-0 na nyingine ya Nusu Fainali 1-0. Yanga iliibuka bingwa, ikiifunga Azam FC 2-0 kwenye fainali.
Brandts atakutana na wachezaji wake wa zamani wawili Yanga, beki Mbuyu Twite anayeanza msimu wa kwanza katika klabu hiyo na kiungo Haruna Niyonzima anayeingia katika msimu wa pili, ambao alifanya nao kazi APR.
 
CHANZO:BIN ZUBEIRY

Chelsea uso kwa uso na Man Utd Kombe la Ligi

 

 

BAADA ya kufanikiwa kupenya katika michuano ya Kombe la Ligi, mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Chelsea na Manchester United zinatarajiwa kuvaana katika hatua ya 16 Bora ya michuano ya Kombe la Ligi.

Timu hizo vigogo vimepangwa kuumana katika droo ya michuano hiyo iliyotolewa juzi baada ya timu hizo kupata ushindi katika mechi zao za hatua iliyopita ambayo ilishuhudia mabingwa watetezi wa Ligi ya England ikitupwa nje na Aston Villa.

Ratiba hiyo inaonyesha pia timu za Liverpool na Swansea City zilizobadilishana makocha zitavaana, huku Sunderland itaumana na Middlesbrough kuwania nafasi ya kutinga robo fainali hapo baadae.

Mechi hizo za kuwania kutinga robo fainali zinatarajiwa kuchezwa Oktoba 29 mwaka huu ambapo timu zilizopangwa kung'oa hatua hiyo ya 16 Bora ni kama ifuatavyo hapo chini:

 

Sunderland v Middlesbrough
Swindon Town v Aston Villa
Wigan Athletic v Bradford City
Leeds United v Southampton
Norwich City v Tottenham Hotspur 
Liverpool v Swansea City
Chelsea v Manchester United

Reading v Arsenal

FAINALI ZA STR8 MUZIKI ZAFANA MWANZA



Izzo Bizness akishusha michano
 






FAINALI za tamasha la muziki la STR8 zilimalizika jana mjini hapa kwa kishindo cha aina yake huku tuzo ya DJ Bora yenye thamani ya thamani ya Sh. milioni 7 ikimuangukia DJ Juma Ramadhani.

Ilikuwa ni patashika nguo kuchanika wakati ma-DJ na ma-MC walipokuwa wakipambana vikali kuwania moja ya vifaa vya kisasa kabisa katika masuala ya kuchezesha muziki, DJ Pioneer.


Ruyobya Johaness a.k.a DJ YT alikamata nafasi ya pili katika kategori ya ma-MC akiondoka zawadi kadhaa zikiwamo fedha taslimu Sh.100,000.


Mshindi katika kategori ya MC alikuwa ni Joash Magadula ambaye pamoja na tuzo pia alipata nafasi ya kurekodi albamu katika moja ya studio tatu bora za muziki nchini.


Nchana Anthony alishika nafasi ya pili katika kategori hiyo ya ma-MC na aliondoka na zawadi kadhaa na fedha taslimu Sh.100,000.


Fainali hizo ambazo ni za tatu tangu zianzishwe nchini zinaratibiwa na kampuni ya Sigara nchini (TCC) kwa lengo la kukuza vipaji miongoni mwa vijana na kutengeneza nafasi ya ajira.


Michuano hiyo ambayo ilihusisha ma-Mc 85 na ma-DJ 25 zilichuja washindani wake hadi 16 kwa MC na 10 kwa ma-DJ katika raundi ya kwanza kabla ya raundi ya pili kutoa washiriki wa fainali.


Ma-DJ hao walipewa maksi kwa kuangaliwa na majaji kuhusu uwezo wao wa kuchanganya muziki, uwezo wa kiufundi, wanavyomudu vifaa wanavyofanyia kazi na jinsi wanavyoburudisha.


Ma-DJ sita waliofika fainali walikuwa Bernard Fabian, DJ Yt, Robert Rowan, DJ Megastar, Tony Wyclif na Juma Ramadhani.


Kategori ya MC ilihusisha mshiriki kupewa mada ya kuielezea kwa mtindo wa kufokafoka kwa dakika tatu kiushairi kimpangilio.


Matukio hayo ya fainali yalinogeshwa na burudani mbalimbali zikiwamo zilizotolewa na wakali wa Bongofleva kama rapa Izzo Bizness ambaye ni maarufu kupitia wimbo wake wa 'Riz-One (Ongea na Mshua)’ .


Walikuwapo pia vijana wa kundi la kudansi la BFB la Mwanza, ambao walipagawisha mashabiki kwa staili zao mbalimbali za kucheza ikiwamo kwa sarakasi.


Aliyetingisha zaidi katika vionjo alikuwa ni mshindi mwaka 2010 katika kategori ya MC, DJ Simba, ambaye alionesha ubabe wake katika kucheza na biti kiasi cha kufanya ukumbi mzima kurindima kwa shangwe.


“Vipaji hivi vinatakiwa kulelewa na kuendelezwa,” alisema Deogratius Kamugisha, mwenyeji wa mashindano hayo ambaye pia ni Meneja wa TCC Mwanza.


Alisema kwamba michuano hiyo ilikuwa si tu burudani bali pia ilitoa mwanya wa mafanikio mengine kama ajira.


Alisema washindi wa michuano iliyopita kwa sasa wako katika ajira mbalimbali zikiwemo vilabu vya usiku na vituo vya radio.


"Hii ni namna ya kutengeneza ajira," alisema na kuongeza kwamba mashine ya kuchezea muziki kama aliyopewa Juma Ramadhani ni chanzo cha ajira kwani anaweza kuitumia yeye au kuikodisha kwa wengine anapokuwa hana kazi nayo.


Mchuano mingine miwili itafanyika mjini Dar es Salaam na Mbeya kukamilisha tamasha la mwaka huu.

UDOM YAKARIBIA KUINGIZA FILAMU YA MY MAN 2 SOKONI.


Filamu Mpya Ya My Man Sehemu ya 2 inatarajiwa kuingia Sokoni muda si mrefu kutokana na kumalizika kwa kazi nzima ya utengenezaji wake.

Filamu hii ya kitanzania ambayo story yake imeandikwa na Kijana Geric Kimaro anayesomea Shahada ya Kwanza ya Filamu katika Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) akiwa mwanafunzi wa Mwaka wa 2 Chuo Hapo.

Akiongea na Mtandao  wa LUKAZA BLOG amesema " Mashabiki wa filamu za kitanzania wakae Mkao wa Kula kwasababu kwanza hawataboreka kutokana na waigizaji wake ni Vijana wanaosomea fani ya Filamu katika ngazi ya Shahada ya Kwanza ambao wana vipaji na ujuzi pia katika tasnia ya filamu nchini lakini pia Katika filamu hiyo ambayo imetengenezwa na kampuni ya BORNAGAIN na kumshirikisha Nguli wa filamu za Bongo Mwenye Swaga za Uchungaji, Pastor Myamba." 

Mbali na Kumshirikisha Pastor Myamba amesema kuwa katika filamu hiyo kuna sura mpya nyingi ambazo ni vipaji na zao kutoka Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) ambapo wengi wao ni wanafunzi wanaosomea Shahada ya Kwanza ya Filamu,Na amefanya hivi kuonyesha na Kutambulisha vipaji ambavyo badi vipo Shuleni.

Alimalizia kwa Kusema kuwa Filamu hii sio ya Kukosa kwasababu humo ndani ni kuna vitu vipya ambavyo havijawahi kuonekana katika filamu za bongo, Kwahiyo Usikose nakala Yako

RICK ROSS KUCHANA SERENGETI FIESTA DAR OKT 6



Na Mwandishi Wetu, Dar
Msanii nyota kutoka nchini Marekani, mzaliwa wa nchini  Marekani, anayetambulika kwa jina la kisanii kama Rick Ross, ambaye kwa jina halisi anajulikana kama William Leonard Roberts II, anatarajia kutua nchini Tanzania hivi karibuni kwa ajili ya kushiriki kikamilifu kushambulia jukwaa la Serengeti Fiesta 2012, litakalofanyika Oktoba 6 ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Katika kuhakikisha mambo yanakwenda sawa bin sawia kwa kila idara kuhusiana na tamasha hilo, waandaaji ambao ni Prime Time Promotions Ltd wakishirikiana na Clouds Media Group huku mdhamini wao mkubwa ikiwa ni kampuni ya bia ya Serengeti,wameandaa shamara shamra mbalimbali za kuhakikisha tamasha hilo mpaka linafika kileleni,linaamsha na kuacha gumzo la kipekee kabisa miongoni mwa wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake, ikibidi mpaka Kigoma mwisho wa reli kwa namna moja ama nyingine.

Msanii huyo mwenye umahiri mkubwa wa kufloo awapo jukwaani mpaka sasa anatamba na nyimbo/albamu kadhaa kama vile  Hold Me Back 2012 God Forgives, I Don't, Hustlin' 2006 Port of Miami Diced Pineapples 2012 God Forgives, I Don't So Sophisticated 2012 God Forgives, I Don't 911 2012 God Forgives, I Don't Stay Schemin 2012 Rich Forever Aston Martin Music. 

Nyinginezo ni  2010 Teflon Don DJ Khaled 2008 Trilla Lemme See 2012 So Sophisticated Amsterdam 2012 God Forgives, I Don't Black Magic 2012 Maybach Music Group Presents Self Made, Vol. 2: The Untouchable Empire The Boss 2008 Trilla You the Boss 2011 You the Boss Touch'n You 2012 Touch'N You Bag of Money 2012 Maybach Music Group Presents Self Made, Vol. 2: The Untouchable

AZAM, JKT RUVU KUANZA KUONEKANA SUPER SPORT WEEKEND 


Mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kesho inaingia raundi ya nne, ambapo kwa mechi za Super Weekend ambazo zitakuwa zikionyeshwa moja kwa moja (live) na kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini. 
Miongoni mwa mechi zitakazoonyeshwa na kituo hicho, mechi ya kwanza itakuwa ni kati ya Azam na JKT Ruvu Stars, itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ambayo itaanza saa 1 kamili usiku kwa viingilio vya sh. 3,000 mzunguko, sh. 5,000 kwa VIP C na VIP B wakati VIP A kiingilio kitakuwa ni sh. 10,000.
 
Jumamosi pia kutakuwa na mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons, ambayo pia itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni na siku ya jumapili, Yanga na African Lyon zote za jijini Dar es Salaam, zitakutana katika uwanja huo huo kuanzia saa 11 kamili jioni.

Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam wenyewe utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar, mchezo utakaochezwa Oktoba 1, mwaka huu kuanza saa 10.30 jioni.
Na mechi ya mwisho ya Super Weekend itachezwa Oktoba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikizikutanisha Yanga na Simba kuanzia saa 1 kamili usiku.

SHY-ROSE BHANJI APITISHWA CCM KUWANIA NEC- TZ BARA



Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mh. Shy-Rose Bhanji amefanikiwa kuwa mmoja wa wagombea 10 waliopitishwa kati ya 31 na Kamati ya Halmashauri Kuu ya CCM-NEC kugombea Ujumbe wa Halmashauri kuu ya CCM NEC Tanzania bara. Katika kinyang'anyiro hicho Mh. Shy-Rose Bhanji anapambana na baadhi ya mawaziri na viongozi wa juu wa chama hicho.

MAMA AFRIKA SARAKASI YAFANA


... ilikuwa ni maajabu na kweli.
 
Kijana mwingine alionyesha umahili wake ni huyu kama vile unavyomuona.
Michezo ya kamba nayo ilikuwa ya kuvutia.
 Mchezo mwingine ulikuwa niwa kurushiana vikapu ya kutimia miguu.
 Vijana wakionyesha uhodari wao wa kupaa juu.
 
Vijana wakiaga mara baada ya onyesho kumalizika.

FAINALI ZA MICHUANO YA SAFARI POOL MWANZA YAFUNGULIWA 


Waamuzi wa mchezo wa Pool wakiongoza maandamano ya kuingia ukumbini wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Safari Pool Taifa yaliyofunguliwa rasmi jana katika Hoteli ya Monarch jijini Mwanza na Mkuu wa Wilya ya Ilemela, Amina Masenza.

 Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akizungumza na wachezaji wa Pool (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Safari Pool Taifa yaliyofunguliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amina Masenza katika Hoteli ya Monarch jijini Mwanza
Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amina Masenza (wapili kulia) akifungua rasmi mashindano ya Safari Pool Taifa .Kulia ni Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ilemela(OCD),Debora Magiligimba.Wengine kutoka kushoto ni Katibu wa chama cha Pool Mkoa wa Ilala, Mohamed Mwarabu, Mwenyekiti wa kamati ya mashindano, Haji Kapulila na Makamu mwenyekiti wa TAPA, Fred Mushi


Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amina Masenza akizungumza na wachezaji (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Safari Pool Taifa katika Hoteli ya Monarch jijini Mwanza.Kushoto ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool Taifa, Fred Mushi.

BONDIA RAJABU MAOJA AELEKEA NAMIBIA


. Ataiwakilisha Tanzania kwenye programu ya “IBF Utalii wa Michezo” (IBF Sports Tourism)

. Anakutana na bingwa wa Namibia kwenye mpambano wa IBF Africa.


Mtanzania Rajabu mtoto wa Jumanne Maoja mkazi wa jiji la Tanga anaondoka na Shirika la Ndege la Afrika ya Kusini (South African Airways) kuelekea jijini Windhoek, Namibia ambako ana kibarua kikali kuiwakilisha Tanzania kwenye IBF Utalii wa Michezo (IBF Sports Tourism).

Maoja atakutana na bingwa wa nchi ya Namibia, Goettlieb Ndokosho kwenye mpambano uliopewa jina la “Vita Vya Jangwa la Kalahari” (The Battle for the Kalahari Desert) na waandaaji wa mpambano huo wa raundi 12 kumpata bingwa wa IBF Afrika katika uzito wa unyoya. Kinda Boxing Promotions inayoongozwa na bwana Simon Nangolo ambaye ni mkaguzi mwandamizi wa ndani wa mahesabu (Senior Internal Auditor) nchini Namibia ndio waandaaji wa mpambano huo wakukata na shoka.

Mshindi wa mpambano huo atakutana na bingwa wa IBF Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba ya Uarabu na Uajemi, Mtanzania Ramadhani Shauri ambaye hivi karibuni alimkung’uta bondia Sande Kizito wa Uganda katika mpambano ulioishia raundi ya 8 baada ya Kizito kushindwa kuendelea.

Huu unakuwa mpambano wa tatu kwa Watanzania mwaka huu kuwania ubingwa wa IBF katika bara la Afrika, Mashariki ya Kati ya Ghuba ya Uajemi ambako tayari mikanda miwili ya IBF iko Tanzania.

Mpambano wa Mtanzania Rajabu Jumanne Maoja na Goettlieb Ndokosho wa Namibia utafanyika katika jiji la Windhoek, mji mkuu wa nchi ya Namibia tarehe 29 Septemba siku ya Jumamosi.

Mtanzania Rajabu Jumanne Maoja atafuatana na Kocha wake Ibrahim Raphael Jorum ambaye naye anatoka katika jiji la Tanga.

Msimamizi mkuu wa mpambano huo ni Mtanzania Onesmo Alfred McBride Ngowi ambaye atalisimamia pambano hilo lililo na upinzania mkubwa!

Mungu mbariki Rajabu Jumanne Maoja, Mungu ibariki nchi nzuri ya Tanzania.

Imetolewa na:
Utawala
KAMISHENI YA NGUMI ZA KULIPWA NCHINI (TPBC)

ESTHER BULAYA AKIKABIDHI JEZI ZA MPIRA KWA VIJANA



 Mbunge wa viti maalumu kundi la vijana mkoa wa Mara, Ester Bulaya akikabidhi jezi na mpira kwa wenyeviti na makatibu wa vijana wa CCM wilaya ya Butiama kwenye hafra fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Chama cha Mapinduzi mjini Musoma. (Picha na Berensi Alikadi)

Jeshi Stars yaivua Magereza ubingwa wa Wavu


MABINGWA mara tatu mfululizo wa michuano ya wavu ya wanawake, Magereza, wamevuliwa ubingwa huo na maafande wenzao wa Jeshi Stars baada ya kubwagwa kwa seti 3-1 katika mechi ya fainali iliyopigwa kwenye viwanja vya Bwalo la Umwema mjini Morogoro.
Kwa upande wa wanaume, timu ya Magereza ilitetea vyema taji lao baada ya kuwachapa Jeshi Stars kwa seti 3-0 katika mechi nyingine ya fainali iliyochezwa jana.
Nahodha wa Jeshi Stars (Wanawake), Zainab Thabit alisema timu yake imetwaa ubingwa huo kutokana na ujasiri wa kupambana hadi mwisho waliouonyesha dhidi ya mabingwa hao wa muda mrefu huku Ester Noel wa Magereza akiahidi kwamba mwakani watajifua zaidi kuhakikisha wanarejesha taji walilopoteza.
Mgeni rasmi katika fainali hizo, Katibu Mkuu Msaidizi wa Baraza la Michezo Taifa (BMT), Mohamed Kiganja, alisema mwamko wa baadhi ya michezo kama wavu umeendelea kuwa ni mdogo kwa kukosa ufadhili na ndio sababu mikoa mingi imeshindwa kuleta timu.
Aidha, Kiganja alilaumu baadhi ya viongozi kuua michezo kwa kugombea nyadhifa kwenye vyama vya michezo kwa matarajio fulani ambayo wakiyakosa huvitelekeza.
Alishauri zifanyike juhudi za kuibua vipaji vipya kwa kuweka nguvu kwenye ngazi ya shule badala ya kuendelea kutumia wachezaji walioibuliwa zamani kwenye michuano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Msingi (UMISHUMTA), ambao wameendelea kuliwakilisha taifa.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania, Muarami Msumi, alitaka serikali kupitia kitengo chake cha uwekezaji kuhakikisha wawekezaji wanapewa masharti ya kujenga viwanja vya michezo kama sehemu ya uwekezaji, sambamba na kuendelea kujenga na kuimarisha viwanja vya michezo kuanzia ngazi za shule za awali.
Timu 11 zikiwamo tatu za wanawake zilishiriki michuano hiyo.

AZAM KUIENGUA SIMBA KILELENI LEO?

Kikosi cha Azam kitakachopambana na JKT Ruvu leo usiku

TATIZO la majeruhi limeendelea kuikumba timu ngumu ya JKT Ruvu baada ya nyota wake Credo Mwaipopo, Damas Makwaya na George Minja kuondolewa katika kikosi kitakachoshuka dimbani leo kuivaa Azam katika mechi yao ya Ligi Kuu ya Bara itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 1:00 usiku na kuonyeshwa ‘live’ kupitia kituo cha televbisheni cha Super Sport.
Azam inasaka pointi tatu zaidi leo kuwapiku vinara Simba na kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi kuu ya Bara.
Akizungumza na NIPASHE jana, kocha wa JKT Ruvu, Charles Kilinda, alisema kuwa Makwaya ataikosa mechi ya leo kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya misuli, Minja jeraha la goti na mwaipopo atakuwa nje akiuguza maumivu ya jeraha paja.
Kilinda amesema kuwa anasikitika kuwakosa wachezaji hao, lakini hana hofu kwa vile ana wachezaji wengine wazuri wa kuziba nafasi zao, wakiwamo Ramadhan Kauogo na Dumba Ramadhan.
"Pamoja na kuwakosa majeruhi hao, bado kikosi changu kina ari kubwa ya kuibuka na ushindi," alisema Kilinda.
Hata hivyo, Kilinda alilalamikia ratiba ya ligi kwa kusema kwamba imewabana mno kwani  wamejikuta wakicheza mechi tatu mfululizo dhidi ya timu tatu zilizokamata nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi msimu uliopita,  ambazo ni Simba, Azam na Yanga.
Katika mechi mbili zilizopita kabla ya leo, JKT Ruvu walicheza dhidi ya Simba na kuchapwa 2-0 na kasha wakafungwa tena 4-1 katika mechi iliyopita dhidi ya Yanga.
Endapo Azam itashinda, itakwea kileleni kwenye msimamo wa ligi kwani itafikisha pointi 10, moja zaidi ya vinara wa sasa, Simba.
Coastal Union ya jijini Tanga iliyoshinda nyumbani 3-2 katika mechi yao ya juzi dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani ilikwea hadi katika nafasi ya pili baada ya kufikisha pointi nane.
Ligi hiyo inayoshirikisha timu 14, itaendelea pia kesho wakati Simba itakapocheza dhidi ya Prisons ya Mbeya kwenye uwanja huo huo wa Taifa kuanzia saa 11:00 jioni huku Yanga na African Lyon wakivaana keshokutwa Jumapili, pia kwenye Uwanja wa Taifa.
Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam utachezewa mechi kati ya Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar itakayochezwa Oktoba 1 kuanza saa 10.30 jioni na mechi ya mwisho ya 'Super Weekend' itachezwa Oktoba 3 kwenye Uwanja wa Taifa na kuwakutanisha mahasimu wa jadi, Yanga na Simba kuanzia saa 1:00 usiku.
Wakati huo huo, Shirikisho la Soka Nchini (TFF) limesikitishwa na taarifa za kifo cha Katibu Mkuu mstaafu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Erasto Zambi kilichotokea Septemba 26 jijini Dar es Salaam kutokana na maradhi.
Zambi ambaye anatarajiwa kuzikwa keshokutwa Jumapili, kabla ya kuwa kiongozi TOC, kwa muda mrefu alikuwa mwalimu wa michezo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambapo wanamichezo wengi hasa waliokuwa wanafunzi katika chuo hicho wamepita mikononi mwake.

Kikosi cha JKT Ruvu kikiwa mazoezini


CHANZO:NIPASHE

RAIS TFF AFAANUA SUALA LA UDHAMINI WA LIGI KUU TANZANIA BARA


RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Tenga ameingilia kati msuguano unaoendelea kati ya klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara na mdhamini mkuu wa ligi hiyo, kampuni ya huduma za simu ya Vodacom kuhusiana na kuwapo kwa kipengele cha upekee katika mkataba wa udhamini wa ligi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya TFF jijini Dar es Salaam jana, rais huyo alizionya klabu zinazokiuka makubaliano yaliyomo kwenye mkataba huo na kwamba klabu zitakazoendelea kufanya hivyo zitachukuliwa hatua.
“Tunashukuru kupata mkataba ambao ni mara mbili ya ilivyokuwa awali. Mkataba huu lazima ulindwe na uheshimiwe. Yeyote atayekiuka, atachukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu,” alisema Tenga.
Tenga aliyasema hayo wakati mazungumzo kati ya klabu na mdhamini yakiendelea pia jijini Dar es Salaam jana.
Klabu zinalamikia kuwapo kwa vipengele kadhaa katika mkataba huo, vikiwamo vya posho za wachezaji, usafiri na kipengele cha upekee ambacho kinazuia timu kuvaa jezi au kubandika nembo za wapinzani wa kampuni hiyo kibiashara (makampuni ya huduma za simu).
Tenga alisema kuwa kuwapo kwa kipengele cha upekee lazima kiheshimiwe si wakati wa mechi tu, bali hata wakati wa mazoezi ya timu zote 14 zinazoshiriki ligi hiyo kwa kuwa kampuni hiyo ina haki ya matangazo hadi kwenye viwanja vya mazoezi vya timu hizo.
“Klabu zote zinazoshiri Ligi Kuu lazima zielewe hilo. Hata kwenye viwanja vyao vya mazoezi hawaruhusiwi kuvaa jezi au kubandika mabango ya wapinzani wa Vodacom, maana tulikubaliana hivyo na kampuni hiyo kabla ya kusaini mkataba huu,” alisema.
“African Lyon hawakuelewa vizuri vipengele vilivyomo kwenye mkataba huo ndiyo maana tulizungumza nao baada ya kutokea kwa tukio la timu yao kuingia na jezi zenye nembo ya Zantel wakati wa mechi ya Ligi Kuu.
Alidai kuwa mdhamini mkuu wa Ligi ya England ni benki ya Barclays, lakini Liverpool wanavaa jezi zenye nembo ya wadhamini wao ambao ni benki ya Standard Chartered kwa vile benki hizo mbili si wapinzani kibiashara maana kila moja ina aina yake ya wateja.
Alisema kuwa shirikisho hilo liliamua kuondoa kipengele cha upekee katika udhamini kama ilivyokuwa kwenye mkataba wa miaka mitano wa kampuni hiyo uliomalizika mwishoni mwa mwezi uliopita, lakini kipengele hicho kimebaki kwenye bidhaa miongoni mwa wadhamini.
Aidha, Tenga alisema kuwa baadhi ya klabu zinazoshiriki ligi hiyo zinadaiwa kiasi kikubwa cha pesa na shirikisho hilo na kwamba pesa zote zitakazotolewa na wadhamini zitaingizwa kwenye akaunti maalum itakayokuwa chini ya Kamati ya Ligi ya TFF kabla ya kusambazwa kwa klabu husika.
“Klabu zimechelewa kupata fedha kutoka kwa mdhamini mkuu kwa sababu mkataba ulichelewa kusainiwa. Ni kweli kwamba baadhi ya klabu zinadai pesa ya msimu uliopita, lakini klabu nyingi hasa zile kubwa tunazidai kiasi kikubwa sana cha pesa. Safari hii tumefungua akaunti maalum ambapo pesa za wadhamini zitawekwa kabla ya kupelekwa kwa wahusika. Wale wanaodai watalipwa na wale tunaowadai tutakata pesa yetu kwanza kabla ya kuwapatia fungu lao,” alisema.
Alizitaja klabu zinazodaiwa na shirikisho hilo kuwa ni pamoja na Simba, Yanga na Tanzania Prisons na kwamba madeni hayo yalitokana na TFF kuzilipia faini katika nyakati tofauti kwa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), lakini alikataa kutaja kiasi hicho wanachozidai klabu.
Klabu zimekuwa katika mgongano na wadhamini kwa kudai kwamba kiasi wanachotoa cha Sh. bilioni 1.7 kwa mwaka ni kidogo mno kulinganisha na gharama za uendeshaji na kwamba, ili kipengele cha upekee kiendelee kuwapo, ni lazima waongeze fedha hizo na baadhi wamekaririwa wakitaka walau udhamini huo uwe wa Sh. bilioni 4 kwa mwaka.
Wakati ligi kuu ya Bara yenye timu 14 na kuhusisha mechi zaidi ya 180 kwa msimu ikidhaminiwa kwa Sh. bilioni 1.7, timu ya taifa pekee (Taifa Stars) hudhaminiwa na Kampuni ya Bia (TBL) kwa dau la zaidi ya Sh. bilioni 3.5 kwa msimu, bila kujali kwamba mechi zake huwa hazizidi 20 kwa mwaka.

TWIGA STARS
Katika hatua nyingine, Tenga pia aliomba wadhamini wajitokeze kuzisaidia timu za taifa za vijana na timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars) kwa kuwa zina hali mbaya kifedha.
“Tunatumia fedha nyingi sana kuiendesha timu ya Twiga Stars. Kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu, tumetumia Sh. milioni 222 kuihudumi timu hiyo wakati wa kambi na mechi ndani na nje ya nchi,” alisema Tenga.
Tenga, ambaye pia ni Rais wa Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), aliushukuru uongozi wa kituo cha televisheni cha Super Sport cha Afrika Kusini kwa kuamua kuonesha baadhi ya mechi za Ligi Kuu msimu huu.

FA YAMFUNGIA NA KUMPIGA FAINI JOHN TERRY KWA UBAGUZI



John Terry na Anton Ferdinand wakigombana katika tukio linalodaiwa Terry kumbagua Ferdinand
Terry akiwasili mahakamani kutoa ushahidi wa tuhuma hizo na kisha kukutwa hana hatia
LONDON, England
Katika sakata hilo ambalo lilifikishwa mahakamani na Terry kukutwa hana hatia, nahodha huyo wa zamani wa England anadaiwa kumbagua beki wa klabu ya QPR, Anton Ferdinand
HATIMAYE Chama cha Soka cha England (FA), leo kimefikisha tamati sakata la ubaguzi wa rangi lililokuwa likimkabili beki na nahodha wa Chelsea, John Terry na kutoa huku iliyotabiriwa na mtuhumiwa huyo mapema wiki hii.
Katika hukumu yake iliyotoka jana, iliyokuja baada ya mfululizo wa siku nne za kuhojiwa kwa nyota huyo na wakili wake kutoa ushahidi wa kumtetea, FA imemfungia nyota huyo mechi nne na faini ya pauni 220,000.
Katika sakata hilo ambalo lilifikishwa mahakamani na Terry kukutwa hana hatia, nahodha huyo wa zamani wa England anadaiwa kumtolea lugha za kibaguzi beki wa kimataifa wa England anayechezea klabu ya Queens Park Rangers, Anton Ferdinand.
Terry tayari alishakana kuhusika na tuhuma hizo anazodaiwa kuzitoa Oktoba mwaka jana wakati wa mechi baina ya Chelsea na QPR na kusema kuwa, FA inajaribu kukwepa ukweli uliomuacha huru kwenye Mahakama ya Westminster Magistrates.
Kutokana na kuhisi kuonewa na kutambua kama FA ilipanga kumhukumu isivyo, Terry mapema wiki hii alitangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya England, kama sehemu ya kutoa hisia zake kuwa FA kwamba haimtendei haki katika sakata hilo.
Akitangaza uamuzi wa kustaafu soka la kimataifa, Terry, 31, alisema: “Natangaza rasmi leo kuwa nastaafu soka la kimataifa. Napenda kutoa shukrani kwa makocha wote wa England walionichagua mimi kuwamo dimbani na timu hiyo mara 78.
“Nimefanya maamuzi haya mapema kabla hata ya kusikia nini kitaamuliwa juu yangu kwa tuhuma zinazonikabili kwa sababu nahisi FA, imepanga hukumu isiyo ya haki dhidi yangu, licha uamuzi mzuri wa mahakama ulionisafisha na tuhuma hizo.”