STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 28, 2012

Chelsea uso kwa uso na Man Utd Kombe la Ligi

 

 

BAADA ya kufanikiwa kupenya katika michuano ya Kombe la Ligi, mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Chelsea na Manchester United zinatarajiwa kuvaana katika hatua ya 16 Bora ya michuano ya Kombe la Ligi.

Timu hizo vigogo vimepangwa kuumana katika droo ya michuano hiyo iliyotolewa juzi baada ya timu hizo kupata ushindi katika mechi zao za hatua iliyopita ambayo ilishuhudia mabingwa watetezi wa Ligi ya England ikitupwa nje na Aston Villa.

Ratiba hiyo inaonyesha pia timu za Liverpool na Swansea City zilizobadilishana makocha zitavaana, huku Sunderland itaumana na Middlesbrough kuwania nafasi ya kutinga robo fainali hapo baadae.

Mechi hizo za kuwania kutinga robo fainali zinatarajiwa kuchezwa Oktoba 29 mwaka huu ambapo timu zilizopangwa kung'oa hatua hiyo ya 16 Bora ni kama ifuatavyo hapo chini:

 

Sunderland v Middlesbrough
Swindon Town v Aston Villa
Wigan Athletic v Bradford City
Leeds United v Southampton
Norwich City v Tottenham Hotspur 
Liverpool v Swansea City
Chelsea v Manchester United

Reading v Arsenal

No comments:

Post a Comment