STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 23, 2014

TFF yaipa shushu Yanga 'kuiua' Al Ahly

MECHI namba 118 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Tanzania Prisons iliyokuwa ichezwe Februari 26 mwaka huu itapangiwa tarehe nyingine.

Uamuzi wa kuiondoa mechi hiyo iliyokuwa ichezwe Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam umefanywa ili kuipa fursa zaidi Yanga kujiandaa kwa mechi yake ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi Al Ahly ya Misri itakayofanyika Jumamosi (Machi 1 mwaka huu).

Al Ahly na Yanga zitarudiana wiki moja baadaye kati ya Machi 7, 8 au 9 mwaka huu jijini Cairo, Misri.

PSG yaifumua Toulouse nyumbani, Ibrahimovic apiga hat-trick

Zlatan Ibrahimovic akishangilia moja ya mabao yake wakati wakiiangamiza Toulouse nyumbani kwao.
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa, PSG imeendelea kuonyesha dhamira yao ya kutetea taji hilo baada ya kupata ushindi wa kishindo ugenini dhidi ya Toulouse walipoilaza mabao 4-2, huku Zlatan Ibrahimovic akifunga hat-trick yake tatu msimu huu katika ligi hiyo.
Ibrahimovic alianza kwa kufungwa kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 32 kabla ya Wissam Ben Yedder kusawazisha dakika moja kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili wageni waliingia kivingine kwa kulisakama lango la wenyeji wao na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa na Ezequeil Lavezzi katika dakika ya 56 kabla ya Ibarhimovic kurejea tena nyavuni kwa kufunga bao la tatu dakika ya 68 akimalizia kazi nzuri ya Yohan Cabaye.
Ben Yedder alifunga bao la pili kwa wenyeji katika dakika ya 72 na dakika moja kabla ya mchezo huo kumalizika nyota wa Sweden, Ibrahimovic alikamilisha hat-trick yake kwa kufunga bao la nne lilil;oifanya PSG kujikita zaidi kileleni ikifikisha pointi 61 baada ya michezo 26.
Katika mechi nyingine Rennes ilipata ushindi mnono wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nantes kwa mabao ya Ntep, Konradsen na Toivonen.

Spurs yaduwazwa na Norwich City

Joseph Yobo tackles Paulinho during Norwich's Premier League match with Tottenham.
Norwich walipowashikisha adabu Spurs
BAO pekee lililofungwa na Robert Snodgrass katika dakika ya 47 liliiwezesha Norwich City kupata ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Tottenham Hotspur katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyomalizika muda mchache uliopita.
Kipigo hicho ambacho hakikutarajiwa na Spurs kimeifanya timu hiyo iliyotoka kupoteza mechi yake ya Ligi Ndogo ya Ulaya (Europa League), kusaliwa na  pointi 50 na kubali nafasi ya tano nyuma ya Liverpool iliyoshinda mapema leo waliowazidi pointi sita.
Mfungaji wa bao hilo alifunga kwa pasi ya Bradley Johnson na kuwaduwaza vijana wa Tim Sherwoood waliokuwa wakiwafukuza Liverpool katika mbio za kuwepo kwenye Top 4.

Ajali hii imetokea leo na kuua mmoja Moro

 Mlipuko mkubwa wakati matenki ya mafuta yakilipuka
Askari wa kikosi cha zimamoto wakijaribu kuuzima moto huo

Hakuna cha kufanyika kutokana na moto mkubwa na moshi mwingi wakati magari hayo yakiteketea


 Ankle habari. Leo asubuhi eneo la Mikese, Morogoro, tumekutana na na ajali  mbaya sana ya magari mawili, moja la mafuta, kugongana uso kwa uso na kutumbukia mtaroni na yote kushika moto. Inasadikiwa mtu mmoja ambaye ni dereva wa magari hayo kateketea kabisa kwa moto. Picha na Mdau Sixmund KWA HISANI YA MICHUZI BLOG

AC Milan yaifumua Sampdoria kwao 2-0

Adel Taarabt Adel Taarabt of Milan celebrates after scoring the opening goal during the Serie A match between SSC Napoli and AC Milan at Stadio San Paolo on February 8, 2014 in Naples, Italy.
Adel Taarabt
AC Milan imeendelea kujikongoja kwenye Ligi Kuu ya Seria A baada ya jioni hii kupata ushindi wa pili mfululizo kwa kuilaza Sampdoria nyumbani kwao kwa mabao 2-0.
Adel Taarabt alianza kuiandikia Milan bao la kwanza katika dakika ya 12 bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili vijana wa Clarence Seedorf waliingia kwa kasi na kupata bao la pili lililofungwa na Adil Rami kwenye dakika ya 58, huku Sampdoria ikimpoteza Lopez aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu.
Ushindi huo umeifanya Milan kufikisha pointi 35 na kubaki nafasi ya 9 ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Juventus inayotarajia kushuka dimbani muda mchache kuvaana na Torino.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo jana ilishuhudiwa Roma ikipata ushindi ugenini dhidi ya Bologna kwa bao 1-0, Livorno ikilala nyumbani kwa mabao 3-2 dhidi ya Hellas Verona, Udinese na Atalanta zikitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1 sare iliyoipata pia Inter Milan dhidi ya Cagliari na Chievo Verona iliisasambua Catania kwa mabao 2-0.








































Liverpool, Newcastle Utd zashinda England

Jordan Henderson
Jordan Henderson akifunga moja ya mabao yake
Newcastle striker Loic Remy shoots past keeper Brad Guzan for his side's winner against Aston Villa
Luic Remy akifunga bao dakika za jioni likiizima Aston Villa
LIVERPOOL imeendelea kujiimarisha kwenye nafasi ya nne baada ya jioni hii kuikwanyua Swansea City kwa mabao 4-3, huku Newcastle United ikipata ushindi nyumbani dhidi ya Aston Villa kwa bao 1-0 katika Ligi Kuu ya England.
Mabao mawili ya Daniel Sturridge na mengine kama hayo ya Jordan Henderson yalitosha kuizima Swansea iliyokuwa ugenini kwa kuisaidia Liverpool kufikisha jumla ya pointi 56 na kuendelea kujikita kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo.
Sturridge aliiandikia bao Liverpool dakika ya tatu tu ya mchezo akimalizia kazi nzuri ya Raheem Sterling, kabla ya Henderson kuongeza la pili dakika ya 20 kwa pasi ya Sturridge kabla ya Jonjo Shelvey dakika tatu baadaye  na wageni kusawazisha bao dakika ya 26 kupitia kwa Winfried Bony na Sturridge kufunga bao la tatu dakika ya 36 kwa pasi ya Luis Suárez.
Kipindi cha pili kilianza kwa Bony kufunga bao la kusawazisha dakika mbili baada ya mapumziko kwa mkwaju wa penati na Henderson alifunga bao la ushindi dakika ya 74.
Katika mechi nyingine, Newcastle United ikiwa nyumbani iliitandika Aston Villa kwa bao 1-0 , goli hil;o likiwekwa kimiani na  Luic Remy dakika za nyongeza kabla ya pambano hilo kumalizika.
Kwa ushindi huo Newcastle United imechupa hadi nafasi ya nane ikifikisha pointi 40 huku Aston Villa ikisaliwa na pointi zake 28 ikishika nafasi ya 13.

Simba yafa Taifa, Azam yashindwa kurudi kileleni

 * Yabanwa na Prisons wakiruhusu bao jioni
Simba iliyokufa Taifa mbele ya maafande wa JKT Ruvu
Azam iliyoshindwa kurejea kileleni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2
JKT walioitafuna Simba uwanja wa Taifa
Prisons walioendeleza maajabu yake katika duru la pili
WAKATI Azam ikishindwa kurejea kileleni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Prisons, 'Wekundu wa Msimbazi', Simba wameendelea kugawa pointi baada ya kuangukia pua mbele ya JKT Ruvu kwa kufungwa 3-2.
Simba inayonolewa na kocha Zdrakov Logarusic 'Loga' ilijikuta ikipoteza pointi 10 katika mechi ya nne baada ya maafande wa JKT Ruvu chini ya kocha Fred Felix Minziro kushtukiza kwa kipigo hicho leo jioni.
Mabao ya Husseni Bunu katika dakika ya 13 na Emmanuel Switta dakika ya 44 na 53 yalitosha kuinyong'onyesha Simba iliyokuwa inarejea nyumbani jijini Dar es Salaam baada ya kupata matokeo mabovu ugenini ikiambulia pointi mbili katika mechi zake tatu.
Hata hivyo vijana wa Simba walipambana na wapinzani wao waliokuwa pungufu na kufanikiwa kurejesha mabao mawili yalifungwa kwa mikwaju ya penati na Amissi Tambwe moja likiwa la penati dk 74 na 86.
Kwa kipigo hicho Simba imesalia kwenye nafasi ya nne ya msimamo ikiwa na pointi zake 32, tatu pungufu na Mbeya City ambayo nayo jana ililala mbele ya Coastal Union ya Tanga kwenye mfululizo wa ligi hiyo.
Katika mechi nyingine iliyochezwa uwanja wa Chamazi, Prisons Mbeya imeendelea kujikongoja baada ya kuibana Azam na kulazimisha sare ya mabao 2-2.
Bao la kusawazisha la Prisons lilifungwa zikiwa zimesalia dakika mbili kabla ya mchezo huo kuisha wakati Azam wakiamini wameibuka na ushindi na pengine kurejea kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya jana kushushwa na Yanga iliyoifumua Ruvu Shooting kwa mabao 7-0.
Wageni Prisons ambao wanafikisha mechi ya tano bila kupoteza mchezo wowote ikijikusanyia jumla ya pointi 11 ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwana na Omega Seme kabla ya Aggrey Morris kuisawazisha.
Kipre Tchetche aliiongozea Azam bao la pili ilikiwa bao lake la 10 kabla ya kuja kutolewa kwa kadi nyekundu kutokana na kupewa kadi ya njano ya pili.
Laurian Mpalila aliiokoa Prisons isiadhirike baada ya kufunga bao la pili na la kusawazisha zikiwa zimeshalia dakika  mbili kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na kufanya timu hizo zigawane pointi moja moja.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014    
                                  P    W     D    L    F     A   GD  PTS

01.Yanga                   17   11    05   01   41   12   29  38
02.Azam                    17   10    07   00   31   12   19  37
03.Mbeya City           19   09    08   02   24   16   08  35
04.Simba                    19   08    08   03   35   19   16  32
05.Kagera Sugar         19   06    08   05   16  15   01  26
06.Coastal Union        19   05    10    04  14  09   05  25
07.Mtibwa Sugar        19   06    07    06   23  23   00  25
08.Ruvu Shooting        19  06    07   06    20  26  -06  25
09.JKT Ruvu              19   07    01    11   16  29  -13  22
10.Prisons                   18   04    08    05   17  18  -01  20
11.Mgambo                19   05    05    09   12  27  -15  20
12.Oljoro                    20   02    09    09   15  30  -15  15
13.Ashanti                   18   03    05    10   15  30  -15  14
14.Rhino Rangers        19   02    07    10   12  23  -11  13

Wafungaji:
17- Tambwe Amisi (Simba)
10- Kipre Tchetche (Azam)
09- Elias Maguri (Ruvu Shooting) Hamis Kiiza, Didier Kavumbagu (Yanga)
08-Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Mrisho Ngassa (Yanga)
07- Peter Michael (Prisons)
06- Themi Felix (Kagera Sugar), Mwegani Yeya (Mbeya City)
05- Tumba Sued (Ashanti Utd), Jerry Santo (Coastal Union)
04- Jerry Tegete (Yanga), Jonas Mkude, Betram Mombeki (Simba), Bakar Kondo, Salum Machaku (JKT Ruvu), Jerome Lambele (Ruvu Shooting), Abdallah Juma (Mtibwa Sugar)
03- Haruna Chanongo, Ramadhani Singano (Simba), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu) Humphrey Mieno, Mcha Khamis (Azam), Amir Omary (Oljoro), Jeremia John (Mbeya City), Said Dilunga (Ruvu Shooting), Simon Msuva (Yanga), Emmanuel Switta(JKT Ruvu), Laurian Mpalila (Prisons)

MAUAJI YA KIKATILI DAR USTAADH AMCHINJA MTOTO


* Muuaji naye auawa, kumbe mgonjwa wa akili
* Alijaza damu kwenye ndoo
Add caption

mwili wa maremu mtoto Jamali aliechinjwa na ustadhi mbagala charambe mianzini
mwili wa marehem ustadhi mohamed kurangwa aliemchnja mtotoukishushjwa katika hospitali ya Temeke
baadhi ya wakazi wakichungulia nyumba lililotokea tukio la mauaji ya kikatili







USTAADH Mohamed Kurangwa (36), aliyemuua mwanafunzi wa Shule ya Msingi Nzasa Jamal Salum (12)  kisha naye kuuawa, ametajwa kuwa alikuwa ana matatizo ya akili.
Kurangwa alimuua Jamal mwanafunzi wa darasa la tano juzi jioni nyumbani kwake Mbagala Charambe Mianzini,  kwa kumchinja na kuweka kichwa cha marehemu huyu kwenye miguu ya mtoto huyo, kisha kuupeleka mwili wake choo cha nyumba anayoishi, muuaji.
Muuaji huyo alizoa  damu ya Jamal na  kuijaza kwenye ndoo kisha  kuiweka pembeni ya nyumba yake kabla ya kuingia chumbani kwake, kujifungia na kusoma Koran.
Ustaadhi Kurangwa  ambaye  aliuawa na wananchi,  wakati wa uhai wake alikuwa Imam wa msikiti wa Kareem ulioko Charambe.
MATATIZO YA AKILI
Mdogo wa muuaji  Daudi Kurangwa alisema  kati ya mwaka 1996-1997 marehemu kaka yake alishawahi kuugua ugonjwa wa akili na kutibiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Alieleza kuwa baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali alikuwa akiendelea kutumia dawa kwa kipindi  lakini aliziacha baada ya kuhisi amepona.
“Kati ya Juni na Julai mwaka jana aliugua tena  na kutibiwa katika hospitali ya Temeke,” alisema na kuongeza kuwa hata hivyo juzi Kurangwa hakuwa na dalili zozote za ugonjwa huo kumrudia.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Polisi Temeke, Jonathan Shana, akizungumzia tatizo la akili ,  alisema polisi inaendelea na uchunguzi na kueleza kuwa kuna taarifa kuwa muuaji kipindi cha nyuma aliwahi kuugua maradhi ya akili na kwamba kwa hivi karibuni alikuwa ni mzima na hajawahi kuonekana kama anaumwa.
Kamanda Shana alisema ukweli wa tukio hilo haujafahamika na kwamba Kanda Maalum ya Dar es Salaam imeunda kikosi kazi cha kuchunguza tukio hilo.
USHUHUDA WA RAFIKI
Akizungumza na NIPASHE Jumapili nyumbani kwa wazazi wa marehemu Jamal, rafiki wa mtoto huyo aliyenusurika kifo,  Ramadhani Hamisi (11) anayesoma darasa la tano katika  Shule ya Msingi Chemchem, alisema kabla ya kuchinjwa Ustaadhi Kurangwa alianza kumchoma visu mfululizo shingoni..
Ramadhani alisema anaishi na mjomba wake katika nyumba ya Ustadh huyo iliyoko Mianzini Njiapanda, sehemu ambapo imamu huyo alimchinja Jamal
“Siku  ya tukio nilimuomba marehemu Jamal, anisindikize kwenda nyumba  kuchukua kalamu, ilikuwa  saa 10:30 baada ya kupata kalamu hiyo ndani ya chumba tunachoishi na mjomba tulifunga mlango na kuanza kuondoka.
“Wakati  nafunga mlango marehemu Jamal alikuwa jirani yangu akiwa ameshika  madaftari na kalamu,” alisema Ramadhani kwa uchungu.
Aliendelea kueleza kuwa mara Ustadh Kurangwa alitokea akiwa na baiskeli, alipowaona aliiweka pembeni na kuja karibu nao akafungua pazia la mlango wa chumba chake, lakini wakati wanataka kuondoka, ghafla alimkamata Jamal na kuanza kumchoma  kisu sehemu mbalimbali shingoni.
"Nilimshuhudia akimchoma kisu  mara nyingi, Jamal alilia  akisema nisamehe Ustadh, nisamehe Ustadh," aliongeza mtoto huyo huku akitokwa na machozi.
Ramadhani alikimbia hadi nyumbani kwa Jamal  na kumueleza mama yake kuhusu tukio hilo na yaliyoendelea nyuma hakuweza kuyashuhudia tena.
JAMAL ACHINJWA
Mjumbe wa nyumba kumi wa Mtaa wa Mianzin,  Ester Msumba, aliyesema alikuwa wa kwanza kushuhudia tukio hilo, alieleza kuwa  alifika eneo la mauaji baada ya kumsikia  mwanamke mmoja akipiga mayowe kuomba msaada baada ya kuona kiwiliwili cha mtoto kimelala na kichwa chake kimewekwa miguuni.
Alisema mwanamke huyo alikwenda kwenye madrasa ya Ali Munawar  kumpeleka mtoto wake kwa ajili ya kumuanzishia masomo ya ziada, kwa vile licha ya kufundisha dini eneo hilo alilokuwa anaishi Kurangwa linatoa mafunzo hayo ya ziada.
"Baada ya kusikia sauti ya yule mama  nilikimbilia eneo la tukio, hapo nilikuta hali ni mbaya kwani niliona  mwili wa mtoto umelazwa chooni na kichwa chake kiliwekwa miguuni kwake," alisema msumba.
Alisema wakati wa mauaji hayo sauti ya mtoto Jamal  haikusikika hivyo ilikuwa vigumu kupata msaada.
Msumba alisema pamoja na mwili huo, alishuhudia ndoo iliyokuwa na damu iliyochanganywa na maji  kitu kilichoashiria muuaji alikinga damu hiyo kuzuia isitapakae na kusambaa chini.
Sakafu ya choo hicho ilikuwa imejaa damu na familia ilizuiliwa kukitumia kwa muda kupisha uchunguzi.
Baada ya kufanya tukio hilo, Ustadh Kurangwa, alikwenda chumbani kwake na kujifungia huku akisoma Kuran.
"Baada ya kumtafuta kwa muda mtu aliyefanya unyama huo, tuligundua   amejifungia ndani tulipomchungulia tulimuona akisoma Kuran huku kanzu yake ikiwa imetapakaa damu," alisema mjumbe huyo.
USTADHI KURANGWA AUAWA
Wananchi walimvamia  chumbani baada ya kubomoa dirisha na  kumshambulia kwa matofali na mawe hadi alipopoteza fahamu na kumvua nguo kisha kumtoa nje na  kumpiga  hadi alipokata roho.
WAZAZI WA JAMAL
Habiba Selemani (27) mama mzazi wa marehemu Jamal akizungumza na gazeti hili alisema anamuachia Mungu  kifo cha mwanawe.
"Namuachia Mungu kwanini  tukio hili afanyiwe Jamal," alisema mama mzazi, hata  hivyo, alikumbukia kuwa  kabla ya kifo chake  alikuwa anacheza na mdogo wake mwenye miezi sita na kumvisha nguo  alipomaliza aliniaga kwamba anakwenda kucheza.
"Aliniambia anakwenda kucheza lakini kwa mshangao alinieleza kuwa anaona nyota nyingi, sikujali nilimuacha aende zake," aliongeza kusema.
Kwa upande wake   Salimu Ally, ambaye ni baba mzazi, alisema amepokea msiba huo  mshituko mkubwa na hakuamini kilichotokea kwani ni  tukio  la kinyama.
Alieleza kuwa juzi  jioni wakati anakaribia  nyumbani aliwaona wanawake  wanaingia kwenye  nyumba hiyo yalikofanyika mauaji ya  mwanae na kushangaa kwani walikuwa  wanatoka na kulia.
Ally alisema hakujua kilichotokea na kwamba mawazo yake yalikuwa kufika nyumbani kwanza.
“Nilipofika nilimkuta mke wangu analia hajitambui ndipo mpangaji mwenzangu aliponieleza kuwa  mwanangu Jamal  kachinjwa niliumia sana , sikuweza kuamini,” alisema kwa huzuni.
Alikanusha kuwa marehemu mtoto wake alikuwa anasoma kwenye chuo cha Ustaadh huyo na pia hawafahamiani  japo Kurangwa  alimwita na kuingia naye ndani kisha kumchinja.
Mwili wake ungezikwa jana saa 10 jioni  baada ya kupatiwa kibali cha polisi kuchukua maiti kutoka hospitali ya Temeke.
Chanzo:NIPASHE JUMAPILI

Nyamwela afyatua mpya na Tundaman


MNENGUAJI kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Mussa Hassan 'Super Nyamwela' amefyatua wimbo mpya uitwao 'Nyengele' akimshirikisha nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Tundaman ikiwa ni maandalizi yake ya kupakua albamu yake mpya na ya tatu.
Akizungumza na MICHARAZO, Super Nyamwela alisema wimbo huo ambao ni wa nne katika maandalizi ya albamu hiyo baada ya 'Duvele Duvele', na Maneno Maneno ameurekodia katika studio za C9 Records na anatarajia kuachia wiki ijayo.
Nyamwela alisema katika wimbo huo kama ulivyo 'Duvele Duvele' na 'Tumechete'  umepigwa kiasili kwa ajili ya kuleta vionjo tofauti na kutamba kuwa utakuwa funika bovu kwa namna Tundaman alivyompiga tafu.
"Nipo katika maandalizi ya mwisho ya kuachia audio na video ya wimbo wangu mpya uitwao 'Nyengele' ambao nimeuimba na Tundaman ikiwa ni maandalizi kutoa albamu yangu ya tatu baada ya 'Master of the Tample' na 'Afrika Kilomondo', " alisema Nyamwela.
Nyamwela alisema amepanga ndani ya mwaka huu albamu hiyo ya tatu itakuwa imekamilika na pia itafanyiwa uzinduzi , japo hajajua itafanyika mwezi gani na ukumbi gani.
"Nataka nikamilishe nyimbo zote audio na video kabla ya kuizindua rasmi," alisema Nyawela.