STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 23, 2014

Hivi ndivyo Extra Bongo ilivyozindua albamu yake Dar Live


Makhirikhiri walikuwepo kutoa burudani jana Dar Live
Kiongozi wa Extra Bongo, Ally Choky (kushoto) na Muumin Mwinjuma wakiimba kwa pamoja katika uzinduzi wa albamu ya Mtenda akitendewa usiku huu Dar Live.
Banza alikuwa kivutio kikubwa siku ya jana
Choki na Montanabe walifanya yao
Ally Choki na Banzastone wakiimba pamoja
BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo 'Wazee wa Kimbembe' usiku wa jana ilikata kiu ya mashabiki wa muziki nchini baada ya kuzindua kwa kishindo albamu yao ya  'Mtenda Akiitendewa'.
Uzinduzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam huku ukipambwa na makundi mbalimbali ya burudani ikiwamo bendi ya Mashujaa Musica, Linah, Amin, Makhirikhiri na  Khadija Kopa.
Extra Bongo ilipanda jukwaani kuanzia saa nane usiku baada ya makundi hayo kutoa burudani huku mkurugenzi wa bendi hiyo akiingia ukumbini kwa gari la wagonjwa akitanguliwa na waendesha pikipiki ambao ni maarufu kama bodaboda.
Wakati huo wanenguaji wa bendi hiyo walikuwa tayari jukwaani wakifanya vitu vyao kisha Choki akashuka katika gari hilo na kupanda jukwaani na kuonyesha ishara ya kuzima shoo hiyo na kuanza kuimba wimbo wa 'Mtenda Akitendewa'.
Tukio hilo liliwafanya watu waliofurika ukumbini humo walianza kushangilia huku wengine wakimtuza wakati akiimba na pia 'kushambulia' jukwaa sambamba na waimbaji wake akiwamo Banzastone.
Pamoja na uzinduzi huo kupata mashabiki wengi, ulitaka kuharibiwa na wingi wa makundi yaliyoalikwa kutoa burudani ambayo yalichukua muda mrefu jukwaani na hivyo kusababisha uzinduzi huo kumalizika alfajiri.
Baadhi ya mashabiki walisikika wakilalamika kuwa wingi huo wa makundi ya kusindikiza bendi ndiyo uliochangia Extra Bongo ichelewe kupanda jukwaani na hivyo kufanya baadhi yao kuchoka kabla ya kuishuhudia bendi hiyo.
"Choki angealika hata bendi moja tu ingetosha, lakini anachukua makundi mengi ambayo yametumia muda vibaya na sasa Extra Bongo inapanda jukwaani usiku wa maneno wakati sisi tumeshachoka," alilalamika shabiki mmoja.
Alisema kuwa watu walifika kuishuhudia Extra Bongo ikizindua albamu, lakini baadhi yao walijikuta wakichoka na kukata tamaa baada ya kusubiri kwa muda mrefu bila kuona bendi hiyo ikipanda jukwaani.
"Ni kweli kwenye shughuli

No comments:

Post a Comment