STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 23, 2014

Spurs yaduwazwa na Norwich City

Joseph Yobo tackles Paulinho during Norwich's Premier League match with Tottenham.
Norwich walipowashikisha adabu Spurs
BAO pekee lililofungwa na Robert Snodgrass katika dakika ya 47 liliiwezesha Norwich City kupata ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Tottenham Hotspur katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyomalizika muda mchache uliopita.
Kipigo hicho ambacho hakikutarajiwa na Spurs kimeifanya timu hiyo iliyotoka kupoteza mechi yake ya Ligi Ndogo ya Ulaya (Europa League), kusaliwa na  pointi 50 na kubali nafasi ya tano nyuma ya Liverpool iliyoshinda mapema leo waliowazidi pointi sita.
Mfungaji wa bao hilo alifunga kwa pasi ya Bradley Johnson na kuwaduwaza vijana wa Tim Sherwoood waliokuwa wakiwafukuza Liverpool katika mbio za kuwepo kwenye Top 4.

No comments:

Post a Comment