STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 23, 2014

AC Milan yaifumua Sampdoria kwao 2-0

Adel Taarabt Adel Taarabt of Milan celebrates after scoring the opening goal during the Serie A match between SSC Napoli and AC Milan at Stadio San Paolo on February 8, 2014 in Naples, Italy.
Adel Taarabt
AC Milan imeendelea kujikongoja kwenye Ligi Kuu ya Seria A baada ya jioni hii kupata ushindi wa pili mfululizo kwa kuilaza Sampdoria nyumbani kwao kwa mabao 2-0.
Adel Taarabt alianza kuiandikia Milan bao la kwanza katika dakika ya 12 bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili vijana wa Clarence Seedorf waliingia kwa kasi na kupata bao la pili lililofungwa na Adil Rami kwenye dakika ya 58, huku Sampdoria ikimpoteza Lopez aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu.
Ushindi huo umeifanya Milan kufikisha pointi 35 na kubaki nafasi ya 9 ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Juventus inayotarajia kushuka dimbani muda mchache kuvaana na Torino.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo jana ilishuhudiwa Roma ikipata ushindi ugenini dhidi ya Bologna kwa bao 1-0, Livorno ikilala nyumbani kwa mabao 3-2 dhidi ya Hellas Verona, Udinese na Atalanta zikitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1 sare iliyoipata pia Inter Milan dhidi ya Cagliari na Chievo Verona iliisasambua Catania kwa mabao 2-0.








































No comments:

Post a Comment