STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 23, 2014

Barcelona yapigwa ugenini licha ya Messi kutupia

Messi akiwa hoi baada ya ttimu yake kunyukwa mabao 3-1 jana
Messi akidhibitiwa na wachezaji wa Real Sociedad
LICHA ya Lionel Messi kufunga bao linalomfanya kuzidi kuweka rekodi ya ufungaji mabao ndani ya Barcelona, mabingwa watetezi hao wameshindwa kuepuka kipigo ugenini dhidi ya Real Sociedad baada ya kjunyukwa mabao 3-1.
Kipigo hicho kimeifanya Barca kushindwa kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Hispania, La Liga na kjuiacha Real Madrid itanue, huku kukiwa na hati hati ya kuporomoshwa hadiu nafasi ya tatu iwapo Atletico Madrid itaibuka na ushindi leo dhidi ya Osasuna.
Bao la kujifunga la Alexander Song katika dakika ya 32, liliashiria balaa kwa wageni japo Messi alilisawazisha dakika nne baadaya baada ya kumalizia kazi nzuri ya Matrin Montoya na kufanya timu ziende mapumziko zikiwa nguvu sawa ya kufungana bao 1-1.
Kipindi cha pili wenyeji walicharuka zaidi na kujipatia mabao mawili yaliyofungwa na Griezmann  katika dakika ya 54 akimalizia pasi ya Carlos Vela, kabla ya Zurutuza kuongeza bao jingine dakika nne baadaye akimalizia pande la Griezmann.
Kwa matokeo hayo Barcelona wamesalia katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 60, baada ya kucheza mechi 25, huku Sociedad ikpanda hadi nafasi ya tano kwa kufikisha pointi 43.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana na mapema leo Celta de Vigo ikiwa nyumbani ilibanwa na Getafe na kutoka nao sare ya bao 1-1, huku Almería na Malaga nazo zikitoshana nguvu ya suluhu ya bila kufungana.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea leo kwa michezo kadhaa ambapo Rayo Vallecano itaumana na Sevilla, Real Betis itaialika Athletic Club, Valencia na Granada zitaonyeshana kazi na Osasuna itaialika Atlético Madrid na Jumanne Espanyol itaumana na Villarreal.

No comments:

Post a Comment