STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 19, 2013

Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa atiwa mbaroni kisa...!





 mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwasili  eneo la vurugu kabla  ya kuanza kwa  vurugu  hizo
 Mbunge Msigwa akiondoka  eneo la mashine  tatu 
 Machinga  wakisukuma gari ya  mbunge Msigwa 
 Polisi  wakimfuatilia  mbunge Msigwa kwa  nyuma baada ya  kufika eneo hilo  bila kufanya biashara kama alivyoahidi
Polisi  wakianza  kufukuza  wananchi  eneo hilo


 Polisi  wakipita  eneo la Mashine  tatu asubuhi 
 Abiria  na  wapiga  debe  stendi kuu  wakinawa maji baada ya  kupigwa mabomu na kumwagiwa maji ya kuwasha  na askari  wa FFU leo




 Hali  ikiendelea  kuwa  tete  kwa machinga  kufunga barabara  kuu  ya  Iringa  Dodoma na ile ya mashine  tatu
Ni Machafuko  Iringa  hivi  leo








Warembo Miss Tabata 2013 kutembelea Mbuga ya Mikumi

Miss Tabata wakiwa kwenye pozi ya picha ya pamoja



WAREMBO watakaoshiriki kinyang'anyiro cha shindano la Miss Tabata 2013 watatembelea mbuga ya  wanyama ya Mikumi wikiendi ijayo.

Mratibu wa shindano hilo Godfrey Kalinga mapema leo kuwa, lengo la ziara hiyo ni kukuza utalii wa ndani. Alisema kuwa warembo hao pia watapata fursa ya kujua vivutio vilivyomo kwenye mbuga hiyo iliyoko mkoani Morogoro.

“Hii siyo mara yetu ya kwanza kuwapeleka warembo wetu mbugani. Tumekuwa tukifanya kila mwaka,” alisema Kalinga.

Kapinga alisema kuwa ziara hiyo imedhaminiwa na CXC Africa.



Shindano la kumsaka Miss Tabata  litafanyika Mei 31 katika ukumbi wa Da’ West Park, Tabata.

Wadhamini wa shindano hilo ni Nipashe, Redds, Dodoma Wine, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, CXC Africa, Brake Point na Saluti5.

Warembo watakaoshiriki kwenye shindano hilo linaloandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts ni Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbalo (19),  Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Musa Kitereja (19),  Rehema Kihinja (20),  Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23), Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na  Suzan Daniel (18).



Warembo watano watachaguliwa kushiriki mashindano ya Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania.

Anayeshikilia taji la Miss Tabata kwa sasa ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.

Simba na Yanga zaingiza Mil, 500, zenyewe zazoa Mil. 250

Simba na Yanga zilipoumana jana uwanja wa Taifa
Na Boniface Wambura
PAMBANO la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.

Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.

Golden Bush Veterani yaendeleza ubabe Dar

Wakali wa soka la maveterani Dar, Golden Bush
GOLDEN Bush Veterani, maarufu kama 'Wakali wa Soka la Maveterani Dar' kama kawa asubuhi ya leo wameendelea kuzinyanyasa timu za wazee jijini humo baada ya kuwanyuka Ukonga Veterani kwa mabao 2-0.
Timu hiyo ilipata ushindi katika michezo ya Bonanza iliyofanyika kwenye viwanja wa Staki Shari, Ukonga ambapo wakali hao waliwacharaza wapinzani wao hao.
Mabao ya Di Natale na 'kisiki' wa zamani wa Moro Utd na Yanga, Yahya Issa yalitosha kuizamisha Ukonga Veterani na kuwafanya Golden Bush kurejea maskani mwao wakichekaaa kwa ushindi huo.
Msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema licha ya ushindi huo bado hakufurahishwa kwa vile walipania kutoa kipigo zaidi ya hicho.
Ticotico alisema wamekuwa na mazoea ya kuzigonga timu pinzani mabao kuanzia manne hiyo ushindi wa 2-0 wanaona kama hawakutenda haki kwa Ukonga.