STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 19, 2013

Golden Bush Veterani yaendeleza ubabe Dar

Wakali wa soka la maveterani Dar, Golden Bush
GOLDEN Bush Veterani, maarufu kama 'Wakali wa Soka la Maveterani Dar' kama kawa asubuhi ya leo wameendelea kuzinyanyasa timu za wazee jijini humo baada ya kuwanyuka Ukonga Veterani kwa mabao 2-0.
Timu hiyo ilipata ushindi katika michezo ya Bonanza iliyofanyika kwenye viwanja wa Staki Shari, Ukonga ambapo wakali hao waliwacharaza wapinzani wao hao.
Mabao ya Di Natale na 'kisiki' wa zamani wa Moro Utd na Yanga, Yahya Issa yalitosha kuizamisha Ukonga Veterani na kuwafanya Golden Bush kurejea maskani mwao wakichekaaa kwa ushindi huo.
Msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema licha ya ushindi huo bado hakufurahishwa kwa vile walipania kutoa kipigo zaidi ya hicho.
Ticotico alisema wamekuwa na mazoea ya kuzigonga timu pinzani mabao kuanzia manne hiyo ushindi wa 2-0 wanaona kama hawakutenda haki kwa Ukonga.

No comments:

Post a Comment