STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 19, 2013

Maskini! Watoto wa3 wa familia moja wateketea kwa moto



WATOTO watatu wa familia moja wenye umri kati ya miaka miwili na sita, mmoja wao mwanafunzi wa shule ya awali, wamekufa baada ya nyumba walimokuwa wamelala kuungua moto.

Tukio hilo lililozua simanzi kubwa, lilitokea katika Kijiji cha Lushamba, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza, saa 5:00 usiku wa kuamkia Septemba 16, mwaka huu.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Careen Yunus, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, ingawa hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi.

Mama mzazi wa watoto hao anadaiwa kuwaacha watoto hao na kwenda kwa rafiki yake, ambaye mahusiano yao hayakutajwa.

Kitendo hicho ambacho kiliwaudhi wanakijiji na kutaka kumvamia, kumshambulia na kumuua mama huyo.

Hata hivyo, mama huyo alinusurika baada ya uongozi wa kata hiyo chini ya Afisa Mtendaji wake, Amos Mabula, kuingilia kati na kutuliza hasira za wananchi hao.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Bulyaheke, Mabula, aliwataja watoto waliofariki dunia katika ajali hiyo kuwa ni Joseph Alfonce (6),  mwanafunzi wa Shule ya Awali Kanyala; sofia Alfonce (4) na Ndeva Alfonce (2).

Mama wa watoto hao, Naomi Kilembi (25), anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.

Mumewe, Alfonce Budanda, ambaye walijaliwa kuzaa watoto wanne, akiwamo mwenye umri wa miezi mitano aliyekuwa ametoka na mama yake usiku huo, wakati tukio hilo linatokea alikuwa safarini.

Mabula alisema akiwa mlinzi wa amani katika kata hiyo, baada ya wananchi kukusanyika eneo la tukio wakiwa na hasira, mama wa watoto hao alitokea, huku watoto wakiwa wameshateketea kwa moto.

Alisema kuwa alichukua hatua baada ya mama huyo kukiri mbele yake kuwa alikuwa ametoka usiku na kuwaacha watoto hao.

Awali, Diwani wa Kata hiyo, Bagesi Ngele, akizungumzia tukio hilo, alisema tabia hiyo haiwezi kuruhusiwa kuendelea.

Alisema tukio hilo lingeweza kuzuilika kama hatua zingechukuliwa kunzia kwa familia yenyewe kwani kitendo cha kuwaacha watoto peke yao huku kukiwa moto ni cha hatari ikizingatiwa ilikuwa nyumba

TFF yatoa siku 14 kuiona mikataba ya makocha VPL, FDL


Kocha wa Azam na wasaidizi wake inatakiwa mikataba yao TFF

Brandts wa Yanga na Minziro nao wanatakiwa mikataba yao itue TFF
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.


Simba, Mgambo wavuna Sh. Mil 58


Na Boniface Wambura
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mgambo Shooting Stars iliyochezwa jana (Septemba 18 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 58,365,000.

Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh. 4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.

Baby Madaha alamba 'bingo' Kenya

Baby Madaha
Bosi Mpya wa Madaha, Joe Kariuki
MSHIRIKI wa zamani wa BSS, Baby Madaha amelamba 'bingo' baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi na kampuni na Candy n Candy Records ya nchini Kenya wenye thamani ya Sh. Mil 20 za Kenya ambazo ni sawa na Sh. Mil 50 za kitanzania.
Mbali na donge hilo, pia kampuni hiyo inayoongozwa na Mkurugenzi wake, Joe Kariuki imepa msanii huyo anayetamba kwenye fani ya muziki na filamu nchini, gari aina ya Audi TT.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema mkataba huo aliingia hivi karibuni na kampuni hiyo na tayari ameshafyatua kazi mpya kupitia kampuni hiyo iitwao 'Summer Holiday' ambao anatarajia kuizindua rasmi Oktoba 6 jijini Dar es Salaam.
Baby alisema uzinduzi huo utakaoambatana na 'party' ya kusherehekea mafanikio yake kisanii itafanyika kwenye ukumbi wa Dar Live na kusindikizwa na burudani za wasanii mbalimbali.
"Nimeingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi nchini Kenya kupitia kampuni ya Candy n Candy ambayo mbali na fedha pia wamenipa usafiri na tayari nimeshatoa kazi chini yao  iitwayo Summer Holiday iliyoanza kutamba kwenye vituo vya Channel O na MTV," alisema.
Msanii huyo aliyeibuliwa na shindano la BSS 2008, alisema anajisikia fahari kuwa msanii wa kwanza wa kike nchini kupata mkataba mnono kama huo nchini Kenya na imani yake ni mwanzo wa safari yake kuelekea kwenye kilele cha mafanikio kimuziki.

Barafu, Mzee Majuto waja na Daladala pamoja na Monalisa

Kava la filamu mpya ya msanii Barafu
Barafu
BAADA ya kuwatumikia wenzake kwa muda mrefu, hatimaye msanii mahiri wa filamu, Seleman Abdallah 'Barafu' ameibuka na kazi yake binafsi iitwayo 'Daladala' inayozungumzia mikasa, vituko na kero zote zilizopo ndani ya usafiri huo wa umma.
Ndani ya filamu hiyo, mkali huyo ameigiza na wasanii wakongwe nchini kama Amri Athuman 'King Majuto', Yvonne Cherly 'Monalisa' na wengine.
Akizungumza na MICHARAZO Barafu anayefahamika pia kama 'Mzee wa Land Rover', alisema hiyo ni kazi ya kwanza kwake kuuitoa kupitia kampuni yake iitwayo 'Mtafuna Films Production' na ni 'serious comedy'.
Barafu alisema, anatarajiwa kuitoa hadharani filamu hiyo wiki mbili zijazo, na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata burudani na 'kuvunjika mbavu' kwa namna walivyoiigiza filamu hiyo na hasa vimbwanga vya Mzee Majuto.
"Kwa wale ambao wavijua vituko vya Mzee Majuto wajiandae kuumia zaidi kwa namna mzee huyo, mimi na Monalisa tulivyofanya mambo makubwa katika filamu hii ya 'Daladala'," alisema.
Barafu alisema baada ya kutoka kwa 'Daladala' ataanza maandalizi ya kazi zake nyingine kupitia kampuni yake mbali na zile za kushirikishwa na wenzake ambazo alidai hawezi kuziacha.

Chelsea hoi darajani, Barca 'yaua', Arsena yatakata

All smiles: Messi celebrates his opener with defener Dani Alves
Messi akishangilia moja ya mabao yake usiku wa kuamkia leo
Sulley Muntari
Sulley Muntari akishangilia bao la ushindi la Ac Milan alilofunga lala salama
Matchwinner: Marco Streller (second right) steals in at the near post to head Basle's decisive second goal
Basel wakijipatia bao la pili lililoizamisha Chelsea 'darajani' huku Mourhino akipewa ujumbe kupitia mabango kwamba Mata atatakiwa awe uwanjani na siyo kwenye benchi.
 Rumblings of discontent: A Chelsea fan shows his displeasure at Juan Mata's lack of first-team action
WAKATI Jose Mourinho na vijana wake wa Chelsea wakianguka 'darajani' kwa kulala mabao 2-1 mbele ya Basel ya Uswisi, Lionel Messi ameendelea kuboresha rekodi yake ya mabao baada ya kufunga 'hat trick' wakati Barcelona ikiizamisha Ajaz kwa mabao 4-0.
Chelsea ilikumbana na kipigo hicho na kuifanya icheze mechi nne bila kupata ushindi, japo walianza kutangulia katika mechi hiyo iliyochezwa Stanford Bridge kupata bao kupitia Oscar kabla ya Basel kusawazisha mabao yote katika kipindi cha pili.
Mabao ya washindi hao ambao wamekuwa wakizisumbua timu kubwa kila mara katika michuano hiyo, yalifungwa na Salah dakika ya 71 na Streller dakika ya 82.
Katika mechi nyingine Barcelona ikiwa uwanja wake wa nyumbani iliisasambua Ajax ya Uholanzi kwa kuishindilia mabao 4-0, huku 'mchawi mweupe' Messi akitumbukiza mara tatu na kuondoka na mpira wake nyumbani.
Bao jingine la mabingwa hao wa Hispania lilifungwa na Gerard Pique, ilihali Arsenal wakiwa ugenini nchini Ufaransa walitakata baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Olympique Marseille nao Ac Milan ikiwa nyumbani ilifunga Celtic mabao 2-0.
Mecchi nyingine matokeo yake ni Schalke 04 kuilaza Steau Bucharest mabao 3-0, Napoli kuitafuna Borussia Dotmund ya Ujerumani mabao 2-1 nchini Italia, kadhaalika Atletico Madrid wakitakata nyumbani kwa kuilaza Zenit kwa mabao 3-1na Porto ya Ureno kushinda ugenini mbele ya wenyeji wa Austria Wien.

Mabao 58 yafungwa Ligi Kuu, Tambwe nouma Ashanti, Prisons angalau sasa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSAUn1hwkMI3BcBcVeWb4YPc0cKNG2217o1rBuA9t_YRDuDqEfojRYqpc29if8_8ljHN5fIIGwDFx3hdNQ8y8cAo4E9tHnw8BP3Wr4L1T4iGcr2gWQ3Ua9aWJGULdoHdk_r9la7cxPVzw/s1600/DSC_0072.jpg
Tambwe Amissi

JUMLA ya mabao 58 yametinga wavuni mpaka sasa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa imemaliza raundi nne tangu ilipoanza rasmi Agosti 28 mwka huu, huku Mrundi Tambwe Amisi akiongoza orodha ya wafungaji baada ya jana kutupia mabao manne pekee yake wakati Simba ikiichinja Mgambo JKT kwa mabao 6-0.
Mfungaji Bora huyo wa michuano ya Kombe la Kagame, anafukuziwa na wachezaji wa Yanga na Simba, Jerry Tegete na Haruna Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja, huku wachezaji sita wengine wakiwa kwenye nafasi ya tatu na mabao mawili kila mmoja.
Wachezaji hao ni Didier Kavumbagu wa Yanga, Saad Kipanga wa Rhino Rangers, Bakar Kondo wa JKT Ruvu, Elias Maguri (Ruvu Shooting), Jonas Mkude wa Simba na Jerry Santo (Coastal Union).
Safu ya mbele ya Simba ndiyo mpaka sasa inaonekana kuwa kali baada ya kutumbukiza wavuni mabao 11 ikifuatiwa na watani zao Yanga wenye mabao nane, huku timu ya Prisons ndiyo yenye safu butu ya ushambuliaji ikitupia bao moja tu wavuni, ikizidiwa na timu za Oljoro JKT na Ashanti yenye mabao mawili kila moja.
Wakati ukuta wa JKT Ruvu ukiwa mgumu kupitika, ule wa maafande wenzao wa Mgambo JKT ndiyo 'nyanya' baada ya kuruhusu mabao 9 mpaka sasa ikifuatiwa na Ashanti (8) na Prisons iliyofungwa mabao 7.
Mashabiki wa soka watarajie mabadiliko makubwa ya orodha ya ufungaji na hata kwenye msimamo wa Ligi Kuu ambao kwa sasa unaoongozwa na Simba mwishoni mwa wiki wakati ligi hiyo itakapoendelea kwa timu zote 14 kushuka tena dimbani, huku pambano linalosubiriwa kwa hamu likiwa ni Yanga na Azam.
Chini ni msimamo wa sasa wa Ligi hiyo na orodha ya wafungaji mabao;

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                            P  W  D  L    F  A  GD  PTS
1. Simba                         4   3   1   0   11 2  9   10
2. JKT Ruvu                   4   3   0   1   6  1   5    9
3.  Ruvu Shooting           4   3   0   1   6  2   4    9
4.  Yanga                        4   1   3   0   8  4   4    6
5.  Azam                         4   1   3   0   5  3   2    6
6.  Coastal Union            4   1   3   0   4  2   2    6
7.  Mbeya City                4   1   3   0   3   2   1   6
8.  Kagera Sugar             4   1   2   1   3   3   0   5
9.  Mtibwa Sugar            4   1   2   1   2  3   -1   5
10.Rhino Rangers            4   0   3   1   4  6   -2   3
11. Mgambo JKT           4   1   0   3   1   9  -8   3
12. Prisons                      4   0   2   2   1   7  -6   2
13. Oljoro  JKT              4   0   1   3   2   6  -4   1
14. Ashanti United           4   0   1   3   2   8  -6   1

Wafungaji:

4- Tambwe Amisi (Simba)
3- Jerry Tegete (Yanga), Haruna Chanongo (Simba)
2- Didier Kavumbangu (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Jerry Santo (Coastal Union)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, (Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Iman Joel, Salim Majid (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, Kipre Tchetche (Azam), Mwagane Yeya, Steven Mazanda, Paul Nonga (Mbeya City), Laurian Mpalilem, Peter Michael (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli, Cosmas Ader (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga (Mgambo JKT), Themi Felix, Godfrey Wambura, Maregesi Marwa (Kagera Sugar), Amir Omary, Shaibu Nayopa (Oljoro JKT)

Matokeo ya mechi za awali


Agosti 24, 2013
Yanga vs Ashanti United (5-1)
Mtibwa Sugar vs Azam (1-1)
Oljoro JKT vs Coastal Union (0-2)
Mgambo JKT vs JKT Ruvu (0-2)
Rhino Rangers vs Simba (2-2)
Mbeya City vs Kagera Sugar (0-0)
Ruvu Shooting vs Prisons (3-0)

Agosti 28, 2013
Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar (1-0)
Rhino Rangers vs Azam (0-2)
JKT Ruvu  vs Prisons (3-0)
Mbeya City vs Ruvu Shooting (2-1)
Mgambo  vs Ashanti United (1-0)
Oljoro JKT vs Simba (0-1)
Yanga  vs Coastal Union (1-1)

Sept 14, 2013

Simba  vs Mtibwa (2-0)
Coastal Union  vs Prisons (0-0)
Ruvu Shooting va Mgambo JKT (1-0)
Oljoro JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Mbeya City  vs Yanga (1-1)
Kagera Sugar vs Azam (1-1)
Ashanti United  vs JKT Ruvu (0-1)


Sept 18, 2013
Prisons vs Yanga (1-1)
Simba vs Mgambo JKT (6-0)
Kagera Sugar vs JKT Oljoro (2-1)
Azam  vs Ashanti United (1-1)
Coastal Union  vs Rhino Rangers (1-1)
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City (0-0)
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu (1-0)

Ratiba ya mechi zijazo mwishoni mwa wiki hii
Jumamosi
Mgambo JKT vs Rhino Rangers
Prisons vs Mtibwa Sugar
Simba vs Mbeya City
Kagera Sugar vs Ashanti United

Jumapili:

 JKT Ruvu vs Oljoro JKT
Azam  vs Yanga
Coastal Union v Ruvu Shooting