STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 24, 2013

Salha, Hammer Q watoa albamu ya Mke na Mume

Salha Abdallah na mumewe Hammer Q
MUIMBAJI nyota wa taarab wa kundi la Dar Modern, Salha Abdallah akishirikiana na mumewe Husseni Mohammed 'Hammer Q' wamekamilisha kurekodi nyimbo tatu mpya kwa ajili ya kutoa albamu yao.
Akizungumza na MICHARAZO, Salha ambaye 'amelitosa' kundi la Five Star lililokuwa limetangaza kumnyakua hivi karibuni, alisema nyimbo mbili kati ya hizo zipo katika miondoko ya taarab na wimbo mwingine upo katika mahadhi ya mchiriku.
Salha aliyeripotiwa kupewa kipigo kikali na mumewe huyo kiasi cha kulazwa hospitalini kabla ya kusameheana, alizitaja nyimbo hizo tatu kati ya nne walizopanga kuwamo katika albamu hiyo kuwa  ni 'Tunaoana', 'Safiri Salama' na 'Nisamehe Tusonge Mbele'.
"Wimbo wa 'Nisamehe Tusonge Mbele' upo katika mahadhi ya Mchiriku na nyingine zipo katika miondoko ya taarab na kibao cha mwisho ambacho tutakirekodi baadaye ni ule wa 'Subhana Heri'," alisema Salha.
Muimbaji huyo aliyeingia kwenye fani hiyo mwaka 2008 kwa kuvutiwa na sauti tamu ya marehemu Mariam Khamis, alisema wameanza kutoa albamu hiyo lakini mipango yao ya baadaye kuja kuanzisha kundi lao ili kuepuka kuwatumikia watu.
"Tuna mipango ya kuja kuanzisha kundi letu wenyewe baada ya kufanya kazi kwa watu kwa kipindi kirefu bila ya kupata mafanikio yoyote ya maana," alisema Salha

No comments:

Post a Comment