STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 24, 2013

Banka kuitema Bandari-Kenya, huenda akarejea nyumbani au....!


Banka (kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wa Kitanzania wanaocheza wote Bandari-Kenya
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Kenya, Mohammed Banka amesema hafikirii kuongeza mkataba mpya na timu yake ya Bandari Kenya bila kueleza sababu.
Banka, alisema kuna mambo mawili kichwani mwake baada ya kuisha kwa mkataba wake na klabu hiyo yenye maskani yake Mombasa, ama arejee nyumbani au kujiunga na timu nyingine.
Kiungo huyo alisema mkataba wake unatarajiwa kuisha miezi miezi mwili ijayo na hivyo hajaamua kuongeza mkataba mpya zaidi ya kutaka kuondoka klabuni hapo.
"Tunamalizia duru la kwanza Jumapili kwa kuumana na Sofapaka na mimi ndiyo namalizia mkataba wangu na sifikirii kuongeza tena zaidi ya kurudi nyumbani au kusonga mbele," alisema Banka.
Mchezaji huyo aliyekuwa miongoni mwa walioipandisha Ligi Kuu timu hiyo ambayo kwa sasa ipo nafasi ya sita kwenye msimamo wa timu 16, alisema haoni sababu ya kubaki Bandari bila kufafanua.
Hata hivyo hivi karibuni mchezaji huyo alidokeza kuna mambo hayapo sawa hasa suala la masilahi tofauti na makubaliano yaliyokuwepo kati yake na uongozi wa timu hiyo ilipopanda daraja.


No comments:

Post a Comment