STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 24, 2013

Chegge, Mhe Temba wanaswa na Maringo 7


Mhe Temba na Chegge

Maringo Saba katika pozi
MCHEKESHAJI anayetamba kwenye kipindi cha Mizengwe, Rashid Costa 'Maringo 7' amewajumuisha wakali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Said Chegge, Mheshimiwa Temba na 'bosi' wao Saidi Fella kwenye filamu yake anayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Maringo 7 aliyewahi kutamba na michezo ya kuigiza ya kwenye runinga akiwa na kundi la Shirikisho Msanii Afrika, alisema filamu hiyo itafahamika kwa jina la 'Papaa' na atawashirikisha wakali hao na nyota wengine wa filamu nchini.
"Nipo katika maandalizi ya mwisho ya kukamilisha filamu yangu mpya itakayoitwa 'Papaa' ambayo mbali na kucheza mimi na nyota wengine wa filamu, pia ndani mwake kutakuwa na Said Fella, Mhe. Temba, Said Chegge na YP," alisema Maringo 7.
Maringo 7, alisema ana imani kazi hiyo itathibitisha kipaji alichonacho katika sanaa ya uigizaji na muziki, fani anazozifanya kwa wakati mmoja kwa sasa.

No comments:

Post a Comment