STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 24, 2013

Banana Zorro, Khadija Kopa kupamba Miss Ukonga kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhWIQs31cc1ObyFSwZFkTslMrCrqe8JOHfVCu5nkNNQIMV-QitnF79eyi9AgiPQKx9mq3a7k7lemiNEE0Y6epiRyqHRbVYnrCXUJvSOY0_6ingI_jceO6O3ekt0BiFPfLJBng9Pq07XD6o/s400/IMGP0489.JPG
Banana Zorro na mmoja wa waimbaji wake wa B-Band wakitumbuiza

http://1.bp.blogspot.com/-Jqs6ERoQU2M/TvC57BGBQ_I/AAAAAAAAGQw/A8s-FsEMnZs/s1600/kopa.jpg
Khadija Kopa
WASANII nyota nchini Banana Zorro na bendi yake ya B-Band pamoja na Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa kesho wanatarajiwa kuwasinidikiza warembo 17 watakaochuana kuwania taji la urembo la Redd's Miss Ukonga 2013, litakalofanyika jijini Dar es Salaam.
Warembo hao watachuana kwenye shindano litakalofanyika kwenye ukumbi wa Wenge Garden na kusindikizwa na burudani ya wasanii hao wanaotamba nchini na nyimbo mbalimbali.
Mratibu wa shindano hilo, Rashid Kazumba aliiambia MICHARAZO kuwa jumla ya warembo 17 watachuana kuwania taji hilo sambamba na kuwania nafasi ya kuwania ushiriki wa shindano la Miss Ilala litakalofanyika baadaye.
Kazumba alisema maandalizi kwa ujumla kwa ajili ya kinyang'anyiro hicho yamekamilika na kwamba inasubiriwa tu kuona nani atakayeibuka kidedea usiku wa kesho.
Aliwataja baadhi ya warembo watakaochuana katika shindano hilo lililodhaminiwa na makampuni kadhaa nchini ni pamoja na Glory Jigge, Happiness Jackson, Flosek Mwakanyamale, Annatolia Raphael, Musnat Hassan, Gift Swai, Natasha Mohamed, Vanessa Magule, Queen John, Martha Gewe, Nancy Obasi, Mwanamkasi Bakari na Diana Joachim.



No comments:

Post a Comment