STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 24, 2013

Klabu za Ligi Kuu kupigwa msasa kuhusu usajili wa TMS




Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa semina ya usajili kwa njia ya mtandao (Transfer Matching System-TMS) kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom kwa ajili ya msimu wa 2013/2014.

Semina hiyo itafanyika Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF saa 3 kamili asubuhi ikishirikisha watu wawili kutoka kila klabu ambao ni TMS Manager, na ofisa mwingine wa klabu.

Klabu za ligi hiyo zinazotakiwa kuhudhuria semina ya usajili ni Ashanti United, Azam, Coastal Union, JKT Ruvu, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Oljoro JKT, Rhino Rangers, Ruvu Shooting, Simba, Tanzania Prisons na Yanga.

Semina hiyo huenda ikazisaidia klabu za ligi hiyo ambao mara kadhaa wamekuwa wakiingia mkenge katika zoezi la usajili wa wachezaji kutokana na mfumo huo mpya kuwakanganya kama ilivyojitokeza msimu huu ulioisha katika usajili wa mchezaji Mbuyi Twitte aliyegombewa Simba na Yanga.

No comments:

Post a Comment