STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013


WAPINZANI WA MIYEYUSHO, MASHALI WAFAHAMIKA KUPIGANA NAO TAMASHA LA USIKU WA MATUMAINI UWANJA WA TAIFA

Bondia Thomas Mashali (kulia) akitia saini ya dole gumba kwenye mkataba wa kupambana kwa ajili ya kuchangia elimu siku ya Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7, mwaka huu katika uwanja mpya wa Taifa jijini Dar. Mashali atacheza na Bondia Patrick Amote kutoka Kenya. Tamasha hilo litawashilikisha wasanii mbalimbali pamoja na wabunge. Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akisaini mkataba kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya katika Tamasha la Usiku wa Matumaini. Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Thomas Mashali akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Patrick Amote katika Tamasha la Usiku wa Matumaini.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya.

Ajali nyingine mbaya jijini Mbeya, 17 wanusurika kufa kiajabu





Daladala ambayo ilikuwa inatoka Mbalizi kwenda Songwe  yenye namba za usajili T 635 ALS ikiwa imeharibika vibaya Baada ya Ajali kutokea Eneo la Ifisi Mbalizi Mbeya
Hapa ndipo eneo ambalo Daladala iliingia wakati ilijaribu kulipita Gari lengine akiwa mwendo kasi na kuukutana na Tela la Mafuta
Daladala upande wa nyuma
 Lori aina ya Scania yenye namba ZA usajili T378 AGD likiwa limepaki Baada ya ajali hiyo kutokea

Mabaki ya daladala
Wananchi mbalimbali wakiwa wanashuhudia ajali hiyo iliyo tokea Ifisi Mbalizi Mbeya
Hivi ndivyo Daladala inavyo onekana upande wa Mbele baada ya Ajali kutokea


 Dereva wa daladala ambaye ndiye aliye sababisha ajali hiyo Nikutusya Mwanja akiwa anapelekwa chumba cha matibabu ya Haraka.

 
 Baadhi ya Majeruhi waliokuwemo katika ajali hiyo
Wakazi mbalimbali wakiwa katika Hospitali ya Ifisi Mbalizi Mbeya kutazama ndugu zao waliopata ajali.
Askari wa usalama barabarani wakiandikishana Dhamana na ndugu wa Dereva wa Daladala ili apate dhamana ya kutibiwa
*****************


WATU  17 wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuharibika vibaya kufuatia ajali iliyohusisha Gari la abiria aina ya Toyota Hiace na Scania.
Ajali hiyo imetokea  leo majira ya Saa Saba Mchana katika eneo la Ifisi nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Ifisi(ICC) Mbeya Vijijini.
Mashuhuda  wa ajali hiyo wamesema gari la abiria Toyota Hiace lenye namba za usajili T 635 ALS likiendeshwa na Nikutusya Mwanja likitokea Mbalizi kuelekea Songwe iliingia kwenye Trela la Scania lililokuwa likitokea Tunduma kuelekea Dar Es Salaam.
Wamesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa gari ndogo ambapo Dereva alikuwa akijaribu kulipita gari lingine lakini mbele akakutana na Lori ambalo alipojaribu kulikwepa akaingia kwenye Trela lake na kupinduka vibaya.
Trela hilo lenye namba za usajili T 675 ACT likiwa linavutwa na Kichwa chenye namba za usajili T 378 AGD halikuweza kuumia sana kutokana na kwenda kwa mwendo mdogo ambapo majeruhi wote wamekimbizwa katika Hospitale teule ya Ifisi kwa matibabu zaidi.
Muuguzi Msaidizi wa Hospitali Teule ya Ifisi Elimath Sanga amethibitisha kupokelewa kwa majeruhi 17 na kwamba kati ya majeruhi hao 3 hali zao siyo nzuri sana ingawa majina yao hayakuweza kupatikana.
Ameongeza kuwa majeruhi wengi wameumia sehemu za kichwani na miguuni na kwamba baada ya kumaliza kupatiwa huduma ya kwanza wataangalia ni wangapi wanaweza kuruhusiwa na wengine kulazwa.
Hata hivyo habari kutoka eneo la tukio zimesema kuwa Kondakta wa gari dogo aliyefahamika kwa jina moja la Ayubu alitoweka mara baada ya kutokea kwa ajali ingawa haifahamiki kama ni kurukwa kwa akili au ni kukimbia kesi.

Uholanzi yaingia Tano Bora, Tanzania yapaa FIFA

WAKATI Tanzania ikizidi kupaa katika viwango vya ubora wa soka duniani kutoka nafasi ya 116 hadi 109 ikiwa na maana imepanda nafasi saba, nchi ya Uholanzi imefanikiwa kuingia kwenye Tano ya orodha mpya iliyotangazwa na Shirikisho la Kimataifa la Soka, FIFA, huku nchi ya England ikiporomoka kwa nafasi mbili.
Katika orodha mpya nafasi nne za juu imeendelea kubaki vile vile kama ilivyokuwa mwezi uliopita ambapo Hispania ianongoza , ikifuatiwa na Ujerumani kisha Argentina na Croatia.
Ureno ya Cristiano Ronaldo imeshuka kwa nafasi mopja hadi nafasi ya sita, ikifuatiwa na Colombia, Italia, England na Ecuador.
Kwa ukanda wa Afrika Ivory Coast wameendelea kuongoza orodha ikiwa nafasi ya 13 duniani ikifuatiwa na Ghana iliyopo nafasi ya 21 duniani na Mali (23).
Ukanda wa Afrika Mashariki na kati, Uganda inaongoza ikishika nafasi ya 24 Afrika na 93 duniani ikifuatiwa na Ethiopia, kisha Tanzania iliyopanda kwa nafasi saba hadi nafasi ya 109 duniani na 32 Afrika.
Inayofuata baada ya Tanzania ni Kenya iliyolala jana 1-0 kwa Nigeria, kisha Burundi, Rwanda, Sudan, Eritrea, Sudan Kusini, Somalia na Djhibout inayoshika mkia.

Khadija Kopa amlilia mumewe akiwa Rukwa

Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa Rukwa na Mpanda wakimsindikiza kuapanda ndege msanii wa taarab na malkia wa mipasho Tanzania ''Khadija Omar kopa'' kwenye uwanja wa ndege wa mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leo alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye Maadhimnisho ya siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyoadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya (kushoto) akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania, Khadija Omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leo alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
 
Chanzo:Masai Nyota Mbofu

Hatimaye Ngwair apumzishwa nyumba yake ya milele

BAADA ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na majonzi makubwa, hatimaye mwili wa msanii Albert Mangweha 'Ngwair' umepumzishwa leo katika nyumba yake ya milele katika makaburi ya eneo la Kihonda Morogoro.


Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri, ambapo
Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini Afrika Kusini, wiki iliyopita. 
Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao wamehudhuria mazishi hayo.
16f11344cea711e2813a22000a1f8f34_7
75e8603ecea511e29ecd22000aaa08de_7
4406673ccea511e2850422000a1f9a85_7
“Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa sana ni umati usioelezeka mungu akulaze mahali pema peponi,” ameandika Izzo B kwenye Instagram.

Naye Lady Jaydee kupitia Twitter ameandika: Mpk hapa tulipomsindikiza panatosha. Mungu amrehemu, kazi tumeimaliza. Life goes on.”
e1147594cea211e2a86422000a1f9839_7
ee9d94facea411e2a9ea22000ae81462_7
f18745b2cea411e2aa3022000a9e2931_7



Aidha msanii aliyekuwa na Ngwair nchini Afrika kusini Mgaza Pembe maarufu kama M to the P, naye alifanikiwa kutimba nchini na kumuaga 'swahiba' wake kabla ya kuzikwa baada ya awali kufichwa ukweli kuhusu kiofo cha mwenzake.

M to the P aliyekuwa amelazwa hoi hospitalini wakati Ngwair akiaga dunia, aliwasili nchini baadaya kupata ukweli wa mwenzake baadaya awali kufichwa kuwa ametangulia Dar wakati yeye alipokuwa hoi hospitalini na alishindwa kujizuia kumlilia rafikiye huyo wakati akiuaga mwili wa Ngwair leo mchana.
Inaelezwa alipewa taarifa na rafikie wa kike aitwaye Maggie baada ya kumdodosa sana ukweli kuhusu Ngwair na namna waliokuwa wakimtembelea hospitali alikolazwa walivyotoweka ghafla.
Chanzo:Mpekuzi Huru

Binti Michael Jackson anusurika kujiua, kisa...!


http://www.aceshowbiz.com/images/wennpic/paris-jackson-immortalized-handprint-ceremony-03.jpg
Binti wa MJ, Paris Jackson anayedaiwa kutaka kujiua

BINTI wa nyota wa zamani wa miondoko ya Pop duniani, Michael Jackson ambaye kwa sasa ni marehemu, Paris, 15,  amenusurika kujiua na kulazwa kwa sasa hospitali moja iliyopo mjini Carfornia.
Hata hivyo taarifa zilizonukuu mtandao wa kituo cha runinga cha ABC kinasema kuwa Paris anaendelea vyema kwa mujibu wa msemaji wa familia baada ya kupatiwa huduma na madaktari waliompokea.
Inaelezwa kuwa, binti huyo amekuwa katika sononi kubwa tangu baba yake alifariki Juni 2009 na ndicho kinachoelezwa kilimfanya kutaka kujiua.
Paris ni binti mkubwa wa nyota huyo wa zamani wa muziki duniani, ndugu zake wengine wakiwa ni Prince Jackson na Blanket ambaye ni binti mdogo kuzaliwa kati ya watoto hao watatu wa Wacko Jacko.

Haya ni baadhi ya magari aina ya Polaris Rangers RZR zitakazotambulishwa mbio za Puma Rally 2-13








http://www.totalmotorcycle.com/ATV-Quad/2010ATVmodels/2010-Polaris-RangerRZRSc.jpg

Taifa Stars yawatoa hofu Watanzania mechi dhidi ya Morocco

http://www.michezoafrika.com/NewsImages/Taifa-Stars-vs-Morocco.jpg
Thomas Ulimwengu akiwatoka wachezaji wa Morocco katika mechi ya awali iliyochezwa jijini Dar

BAADHI ya wachezaji wa timu ya soka ya taifa, TaifaStars wamewataka watanzania wasiwe na hofu yoyote dhidi ya pambano lao na wenyeji wao Morocco kwa kuahidi kuibuka na ushindi licha ya kucheza ugenini.
Stars inatarajiwa kuvaana na Morocco usiku wa Jumamosi nchini humo katika mechi ya mkondo wa pili kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazili.
Katika mechi ya kwanza ilioyochezwa Machi mwaka huu, Stars iliisambaratisha Morocco kwa mabao 3-1 na kuzidi kung'ang'ania nafasi ya pili katika kundi lao la C ikiwa na pointi 6, moja nyuma ya vinara, Ivory Coast ambayo itakuwa ugenini wikiendi hii kucheza na Gambia.
Licha ya kutambua ugumu wa mechi hiyo ya Jumamosi dhidi ya Morocco baadhi ya wacheza wa Stars wamewatoa hofu watanzania kwa kutamba kuwa ni lazima wawazime kwa mara nyingine Morocco japo wapo nyumbani kwao.
Mmoja wa wachezaji hao aliyezungumza na MICHARAZO kutoka Morocco ni Zahoro Pazi aliyerejeshwa katika kikosi hicho, alisema haoni sababu ya watanzania kuwa na mchecheto dhidi ya mechi hiyo kutokana na namna wachezaji wa Stars walivojiandaa.
Pazi alisema wachezaji wote wana ari na morali kubwa ya kuhakikisha wanaipa Stars ushindi mbele ya wenyeji wao kwa nia ya kujiweka nafasi nzuri kabla ya kuvaana na Ivory Coast katika mechi ijayo.
"Tunaendelea vyema na tunapenda kuwaambia watanzania nyumbani wasiwe na hofu, tutapigana kiume kuwapa raha na tunaamini Morocco watakaa Jumamosi hata kama watatucheza usiku," alisema.
Naye Himid Mao, alisema ushidni Jumamosi ni lazima kwa namna walivyofanya maandalizi na kujiamini kuwa wanaweza kurudia walichokifanya Tanzania kwa Morocco kwakuwalaza mabao 3-1.
Stars ambayo haijawahi kushiriki Fainali hizo za Kombe la Dunia, inahitaji ushindi ili kurejea nyumbani kuwasubiri Ivory Coast kabla ya kumalizia mechi za kundi lake Septemba mwaka huu dhidi ya Gambia ambao mpaka sasa wanaburuza mkia wakiwa na pointi moja tu.

Ruvu Shooting yamnyakua Mfungaji Bora FDL

http://www.greatfootball.com.ua/tanzania/logo-big/ruvu_shooting_stars.gif

BAADA ya kuwanyakua wachezaji wawili kwa mpigo Cosmas Lewis toka Azam na Elias Maguli kutoka Prisons-Mbeya,  maafande wa Ruvu Shooting imefanikiwa kumnasa mshambuliaji mwingine nyota, Jerome Lembeli kutoka kwa timu iliyopanda daraja ya Ashanti United.
Lembeni aliyewahi kuichezea Moro United na kutamba kwenye timu ya taifa ya vijana U17 ametua Ruvu kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kusainishwa juzi na uongozi wa klabu hiyo.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire alisema kunyakuliwa kwa mshambuliaji huyo aliyeifungia Ashanti mabao 16 wakati wakiirejesha ligi kuu  kuna kusuidia kuimarisha safu ya ushambuliaji wa timu yake ambayo msimu uliopita haikuwa na bahati hasa ilipompoteza Abdallah Seif Karihe aliyepo Azam.
Bwire alisema rekodi za kuvutia za Lembeli ndizo zilizowafanya wamsajili katika muendelezo wao wa kuimarisha kikosi chao kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu 2013-2014.
Limbeli ndiye aliyeifungia Tanzania katika michuano ya U17 bao pekee walipotwaa ubingwa wa Dunia na pia alikuwa mfungaji wa pili katika michuano ya U17 ya Copa Coca Cola iliyofanyika Afrika Kusini akifunga mabao matano moja pungufu la mfungaji bora toka Nigeria.
Pia amekuwa akitoa mchango mkubwa katika  timu za taifa za Serengeti Boys na ilemya U20 tangu alipoanza kuitwa, mbali na kuichezea timu ya taifa mara kadhaa ilipokuwa chini ya kocha Marcio Maximo kabla ya kurejea kwao Brazili.
"Kwa sifa hizo katika kufumania nyavu tumeona ni vyema tuwe naye na tumemsajili kwa mkataba wa miaka miwili tukiamini atatoa mchango mkubwa kwa kikosi cha timu yetu ambacho kimepania msimu ujao iwe tishio baada ya msimu huu kuteleza," alisema Bwire.
Klabu mbalimbali za soka kwa sasa zipo katika harakati za kuimarisha vikosi vyao baada ya kumalizika kwa msimu wa 2012-2013 ambapo ilishuhudiwa timu za majeshi zikichechemea na kuziacha timu za kiraia zikitamba ambapo Yanga ilikuwa bingwa, ikifuatiwa na Azam, Simba,Kagera Sugar, Mtibwa Sugar na Coastal Union zilizomaliza kwenyue Sita Bora.

CHANETA yateua katibu mkuu wa muda

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhPSKf8_wO8O8dSbKi_p0N0JZB5cEPqF9bBLrUQPAKeKW-W7pigpA4aLHh5l5WTWkDRtVLQKJHTkDWW3iyucmYpTe5S4qaub6iAXgJXs4QgUQq1w4q22gF_uGq31xjaE7j60qTteQGClfW0/s1600/9+netiboli.jpg

CHAMA cha netiboli chini (CHANETA) kimemteua Maimuna Mrisho kuwa katibu mkuu wa muda wa chama hicho hadi pale atakapopatikana wa kuajiriwa.
Uteuzi huo umefanywa na kamati ya utendaji ya chama hicho katika kikao kilichofanyika Juni mosi mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Katiba ya CHANETA, katibu huyo atakaa madaraka kwa muda wa miezi sita, hadi pale chama hicho kitakapopata katibu mkuu wa kuajiriwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa CHANETA, Anna Kibira alisema uteuzi huo umepitishwa na wajumbe wa kamati ya utendaji wakati wakiendelea na mchakato wa kupata katibu mkuu wa kuajiriwa.
Mbali na hilo, Kibira alisema katika kikao hicho pia walipitisha wajumbe wa kamati mbalimbali ambazo ni Kamati ya Mashindano, Kamati ya Shule na Vyuo, Kamati ya Ufundi na Mafunzo, pamoja na Kamati ya Fedha na Mipango.
Alisema mbali na kamati hizo, pia waliteuwa walezi watano wa chama na washauri watano ambao watashirikiana na uongozi katika utendaji wa kazi za chama hicho.
Alifafanua zaidi kuwa CHANETA pia likutana na chama cha netiboli cha Zanzibar (CHANEZA) Juni 2 kujadili mambo yahusuyo umoja wa michezo wa vyama hivyo.
Alisema moja ya maazimio waliokubaliana ni pamoja na kukitambua chama cha netiboli cha kimataifa (IFN), Netiboli Afrika (CANA) na chama cha netiboli cha Afrika Mashariki (EANA).
Alisema mambo mengine waliyokubaliana ni pamoja na kuteua timu ya taifa ya Muungano, ambayo itajumuisha wachezaji wa pande zote mbili, ikiwamo pia kuteua makocha wa timu hizo kutoka pande hizo.
Alisema kutokana na makubaliano hayo wameunda kamati ya pamoja ambayo itasimamia utekelezaji wa maazimio hayo ambayo itakuwa chini ya wenyeviti, watendaji wakuu, waweka hazina, na mjumbe mmoja kutoka Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na la Zanzibar, BMTZ.
Wakati huo huo, timu za Jeshi Stars, JKT Mbweni na Filbert Bayi zimetakiwa hadi kufikia Juni 10 ziwe zimethibitisha ushiriki wa mashindano ya klabu bingwa ya Afrika Mashariki.

Chanzo:NIPASHE

Deluxe Modern Taarab yafyatua 3 mpya

Mwanahawa Ally 'Chipolopolo'
KUNDI jipya la muziki wa taarab la High Class maarufu kama Deluxe Modern 'Watoto wa Kujaribu' limekamilisha nyimbo mbili mpya na kufanya ifikishe jumla ya nyimbo tatu wanazoziandaa kwa ajili ya albamu yao ya kwanza.
Akizungumza na MICHARAZO asubuhi ya leo, Mkurugenzi wa kundi hilo Mwanahawa Ally 'Chipolopolo' alisema nyimbo hizo ni 'Acha Kazi Ufanye Kazi' na 'Mwenye Kunirusha Roho Huwezi'.
Mwanahawa alisema nyimbo hizo zimeungana na wimbo wao wa kwanza uitwao 'Riziki Ina Wakati' ambao umekuwa gumzo tangu ulipoanza kusikika hewani kwenye maonyesho yao ya kila wiki.
"Tumekamilisha nyimbo tatu ambao ni maandalizi ya kupakua albamu yetu ya kwanza, baada ya 'Riziki Ina Wakati' sasa tumeibuka na 'Acha Kazi Ufanye Kazi' na 'Mwenye Kunirusha Roho Huwezi," alisema.
Mwanahawa mtoto wa mwanamuziki wa zamani wa bendi za Urafiki Jazz, Bima Lee, Shikamoo Jazz na Msondo Ngoma anasema wamepanmga mpaka kufikia wakati wa sikukuu ya Idd wawe wameikamilisha albamu yao na kuizindua pamoja na kulizindua kundi lao lenye wasanii tisa.
"Tumepanga kabla ya Septemba tuwe tumeikamilisha albamu yetu na kuzindua kundi hilo ambalo maskani yake ni Keko," alisema Mwanahawa  aliyewahi kuyafanyia kazi makundi la Dar Modern, Zanzibar Stars na King's Modern.

Khadija Kopa afiwa na mumewe



MUIMBAJI nyota wa muziki wa taarab nchini,  Khadija Omar Kopa, amefiwa na mumewe kipenzi Jaffari Ally.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa MICHARAZO na muimbaji wa Five Star, Husseni Mohammed 'Hammer Q' ni kwamba Jaffar alifariki usiku wa kuamkia leo akiwa hospitalini.
Marehemu alikuwa anasumbuliwa na matatizo katika mfumo wa upumuaji na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam. 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.