STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013

Deluxe Modern Taarab yafyatua 3 mpya

Mwanahawa Ally 'Chipolopolo'
KUNDI jipya la muziki wa taarab la High Class maarufu kama Deluxe Modern 'Watoto wa Kujaribu' limekamilisha nyimbo mbili mpya na kufanya ifikishe jumla ya nyimbo tatu wanazoziandaa kwa ajili ya albamu yao ya kwanza.
Akizungumza na MICHARAZO asubuhi ya leo, Mkurugenzi wa kundi hilo Mwanahawa Ally 'Chipolopolo' alisema nyimbo hizo ni 'Acha Kazi Ufanye Kazi' na 'Mwenye Kunirusha Roho Huwezi'.
Mwanahawa alisema nyimbo hizo zimeungana na wimbo wao wa kwanza uitwao 'Riziki Ina Wakati' ambao umekuwa gumzo tangu ulipoanza kusikika hewani kwenye maonyesho yao ya kila wiki.
"Tumekamilisha nyimbo tatu ambao ni maandalizi ya kupakua albamu yetu ya kwanza, baada ya 'Riziki Ina Wakati' sasa tumeibuka na 'Acha Kazi Ufanye Kazi' na 'Mwenye Kunirusha Roho Huwezi," alisema.
Mwanahawa mtoto wa mwanamuziki wa zamani wa bendi za Urafiki Jazz, Bima Lee, Shikamoo Jazz na Msondo Ngoma anasema wamepanmga mpaka kufikia wakati wa sikukuu ya Idd wawe wameikamilisha albamu yao na kuizindua pamoja na kulizindua kundi lao lenye wasanii tisa.
"Tumepanga kabla ya Septemba tuwe tumeikamilisha albamu yetu na kuzindua kundi hilo ambalo maskani yake ni Keko," alisema Mwanahawa  aliyewahi kuyafanyia kazi makundi la Dar Modern, Zanzibar Stars na King's Modern.

No comments:

Post a Comment