STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013

Khadija Kopa afiwa na mumewe



MUIMBAJI nyota wa muziki wa taarab nchini,  Khadija Omar Kopa, amefiwa na mumewe kipenzi Jaffari Ally.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa MICHARAZO na muimbaji wa Five Star, Husseni Mohammed 'Hammer Q' ni kwamba Jaffar alifariki usiku wa kuamkia leo akiwa hospitalini.
Marehemu alikuwa anasumbuliwa na matatizo katika mfumo wa upumuaji na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam. 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.

No comments:

Post a Comment