STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013

Binti Michael Jackson anusurika kujiua, kisa...!


http://www.aceshowbiz.com/images/wennpic/paris-jackson-immortalized-handprint-ceremony-03.jpg
Binti wa MJ, Paris Jackson anayedaiwa kutaka kujiua

BINTI wa nyota wa zamani wa miondoko ya Pop duniani, Michael Jackson ambaye kwa sasa ni marehemu, Paris, 15,  amenusurika kujiua na kulazwa kwa sasa hospitali moja iliyopo mjini Carfornia.
Hata hivyo taarifa zilizonukuu mtandao wa kituo cha runinga cha ABC kinasema kuwa Paris anaendelea vyema kwa mujibu wa msemaji wa familia baada ya kupatiwa huduma na madaktari waliompokea.
Inaelezwa kuwa, binti huyo amekuwa katika sononi kubwa tangu baba yake alifariki Juni 2009 na ndicho kinachoelezwa kilimfanya kutaka kujiua.
Paris ni binti mkubwa wa nyota huyo wa zamani wa muziki duniani, ndugu zake wengine wakiwa ni Prince Jackson na Blanket ambaye ni binti mdogo kuzaliwa kati ya watoto hao watatu wa Wacko Jacko.

No comments:

Post a Comment