STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013

CHANETA yateua katibu mkuu wa muda

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhPSKf8_wO8O8dSbKi_p0N0JZB5cEPqF9bBLrUQPAKeKW-W7pigpA4aLHh5l5WTWkDRtVLQKJHTkDWW3iyucmYpTe5S4qaub6iAXgJXs4QgUQq1w4q22gF_uGq31xjaE7j60qTteQGClfW0/s1600/9+netiboli.jpg

CHAMA cha netiboli chini (CHANETA) kimemteua Maimuna Mrisho kuwa katibu mkuu wa muda wa chama hicho hadi pale atakapopatikana wa kuajiriwa.
Uteuzi huo umefanywa na kamati ya utendaji ya chama hicho katika kikao kilichofanyika Juni mosi mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Katiba ya CHANETA, katibu huyo atakaa madaraka kwa muda wa miezi sita, hadi pale chama hicho kitakapopata katibu mkuu wa kuajiriwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa CHANETA, Anna Kibira alisema uteuzi huo umepitishwa na wajumbe wa kamati ya utendaji wakati wakiendelea na mchakato wa kupata katibu mkuu wa kuajiriwa.
Mbali na hilo, Kibira alisema katika kikao hicho pia walipitisha wajumbe wa kamati mbalimbali ambazo ni Kamati ya Mashindano, Kamati ya Shule na Vyuo, Kamati ya Ufundi na Mafunzo, pamoja na Kamati ya Fedha na Mipango.
Alisema mbali na kamati hizo, pia waliteuwa walezi watano wa chama na washauri watano ambao watashirikiana na uongozi katika utendaji wa kazi za chama hicho.
Alifafanua zaidi kuwa CHANETA pia likutana na chama cha netiboli cha Zanzibar (CHANEZA) Juni 2 kujadili mambo yahusuyo umoja wa michezo wa vyama hivyo.
Alisema moja ya maazimio waliokubaliana ni pamoja na kukitambua chama cha netiboli cha kimataifa (IFN), Netiboli Afrika (CANA) na chama cha netiboli cha Afrika Mashariki (EANA).
Alisema mambo mengine waliyokubaliana ni pamoja na kuteua timu ya taifa ya Muungano, ambayo itajumuisha wachezaji wa pande zote mbili, ikiwamo pia kuteua makocha wa timu hizo kutoka pande hizo.
Alisema kutokana na makubaliano hayo wameunda kamati ya pamoja ambayo itasimamia utekelezaji wa maazimio hayo ambayo itakuwa chini ya wenyeviti, watendaji wakuu, waweka hazina, na mjumbe mmoja kutoka Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na la Zanzibar, BMTZ.
Wakati huo huo, timu za Jeshi Stars, JKT Mbweni na Filbert Bayi zimetakiwa hadi kufikia Juni 10 ziwe zimethibitisha ushiriki wa mashindano ya klabu bingwa ya Afrika Mashariki.

Chanzo:NIPASHE

No comments:

Post a Comment