STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 1, 2013

KABURU, WENZAKE WAHOJIWA UPORAJI FEDHA ZA SIMBA

Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange 'Kaburu'

MAKAMU Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ na katibu mkuu wa klabu hiyo, Evodius Mtawala ni miongoni mwa watu waliohojiwa na Jeshi la Polisi jana kusaidia uchunguzi mkali kuhusiana na ujambazi uliosababaisha kuporwa kwa Sh. milioni 10.59 za klabu hiyo zilizotokana na mgawo walioupata katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Tusker ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi.
Akizungumza na jana jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, alisema kuwa wameshawahoji Kaburu, Mtawala na watu wengine kadhaa ili kupata maelezo muhimu yatakayosaidia kupatikana kwa ukweli kuhusiana na kilichotokea.
"Tumewahoji viongozi hao wawili wa Simba (Kaburu na Mtawala) ili kujua taratibu za uhifadhi na utunzwaji wa fedha na mali za klabu yao... maana inastusha kusikia mtu mmoja anakwenda nyumbani kwake na mali ya klabu, tena buila ulinzi wowote ule," alisema Kenyela.
"Tumeamua pia kuwahoji ili kujua hasa ni nini kilichotokea kuanzia Uwanja wa Taifa maana tulibaini kuwa wao (Kaburu na Mtawala) ndiyo waliosaini na kupokea mgawo wa Simba kule uwanjani (Taifa),"  aliongeza.
Kataka hatua nyingine, Kenyela alisema kuwa Mhasibu wa Klabu hiyo, Erick Sekiete na watu wengine wawili, Said Pamba na Stanley Phillipo (23) waliokuwa wakishikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo waliachiwa kwa dhamana jana.
Sekiete na wenzake hao, walivamiwa wakati wakiwa katika eneo la Sinza kwa Remmy baada ya kuteremka katika gari aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T869 BKS iliyokuwa ikiendeshwa na Pamba.
Katika tukio hilo, ilidaiwa kuwa Sh. milioni 7.59 na dola za Marekani 2,000 (Sh. milioni tatu) zilizotokana na mgawo wa klabu hiyo katika mechi yao dhidi ya Tusker FC ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ziliporwa baada ya Sekiete (28) kuvamiwa na majambazi sita katika eneo la  Sinza kwa Remmy jijini Dar es Salaam ambapo risasi kadhaa zilipigwa hewani. Tukio hilo lilitokea saa 3:20 usiku.
Kamanda Kenyela alieleza kuwa Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alimdhamini Sekiete huku Phillipo akidhaminiwa na ndugu yake aitwaye Julius Kiwale.
Kamanda Kenyela alisema kuwa Pamba, ambaye alikuwa dereva wa gari lililowabeba Sekiete na Phillipo, alidhaminiwa na Kasim Pamba.
“Wanatakiwa waripoti katika Kituo cha Polisi Magomeni Jumatano (kesho),” aliongeza Kenyela.


Chanzo;NIPASHE
----------

KALA JEREMIAH KUTOKA NA ALBUM YAKE MPYA


Baada ya kufanya vizuri katika baadhi ya redio na televisheni kwa ngoma yake ya Dear GodKala Jeremiah sasa ameweka wazi kwamba siku ya tarehe 20 mwezi huu anatarajia kutoka na album yake mpya inayokwenda kwa jina la Pasaka.

GOlden Bush yaaga mwaka 2012 kwa aibu yanyukwa na Wahenga

LICHA ya kuwatumia nyota wa zamani wa klabu kubwa za soka nchini za Simba, Yanga na Mtibwa, timu ya soka ya Golden Bush Veterani jana uliuaga mwaka 2012 na kuukaribisha kinyonge mwaka 2013 baada ya kutandikwa mabao 4-3 na wapinzani wao wakubwa, Wahenga Fc katika pambano maalum la kirafiki.
Pambano la timu hizo lilifanyika jana jioni kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Dar es Salaam ambapo Golden Bush, ilijikuta ikipelekwa puta na Wahenga iliyokuwa aikiongozwa na kipa wa zamani wa Yanga na Mtibwa, Mengi Matunda.
Japo Golden Bush, iliyowatumia nyota kama Yahya Issa, Athuman Machuppa, Abuu Ntiro, Waziri Mahadhi, Said Swedi na nduguye Salum Swedi 'Kussi', Nico Nyagawa, Heri Morris, Katina Shija na wengineo iliweza kuongoza kwa mabao 2-1 hadi wakati wa mapumziko, lakini ilishindwa kuepuka kipigio katika mchezo huo.
Golden Bush ilianza kujipatia bao la kuongoza katika dakika ya 18 baada ya Heri Morris kufumua shuti kali lililomshinda kipa wa Wahenga, David 'Seaman' kabla ya Said Swedi kuifungia timu hiyo bao la pili kwa kichwa akiuynganisha krosi pasi ya Nico Nyagawa.
Hata hivyo katika dakika ya 31 Wahenga walipata bao lao la kwanza kupitia kwa mchezaji wao aitwae God aliyeusukumia mpira wavuni kwa shuti karibu na lango lwa Golden Bush.
Kipindi cha pili kilishuhudiwa kwa Golden Bush ikifanya mabadiliko makubwa katika kikosi chao ikiwamo kumtoa Onesmo Waziri 'Ticotico' aliyekuwa akisumbua mbele licha ya kucheza akiwa majeruhi, lakini mabadiliko hayo hayakuwasaidia baada ya Wahenga kutumbukiza wavuni bao la kusawazisha katika dakika ya 65 kupitia Frank 'Super Et'oo'.
Wakati Golden Bush wakitafarakari jinsi walivyofungwa bao hilo, Wahenga walipata bao jingine la tatu lililofungwa kwa njia ya penati na kipa David Seaman katika dakika ya 78 baada ya mmoja wa wachezaji wa timu hiyo kuchezewa rafu ndani ya lango la Golden Bush.
Jahazi la Golden Bush lilizidi kuzama katika dakika ya 82 wakati Wahenga walipojipatia bao lao la nne lililofungwa na beki aliyepanda mbele kusaidia mashambulizi Shomar aliyewatoroka mabeki wa Golden Bush ambao katika mechi ya jana walionekana kuyumba kusiko kawaida.
Hata hivyo zikiwa zimesalia dakika nne, Golden Bush ilijipatia bao lao tatu la kujifutia machozi, lililofungwa kwa ,mpira wa adhabu ndogo na Salum Swedi 'Kussi' baada ya Machota kuchezewa vibaya na mabeki wa Wahenga nje ya eneo la hatari.
Mara baada ya pambano hilo, Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema wamekikuibali kipigo cha wapinzani wao, licha ya kwamba alimtupia lawama mwamuzi wa pambano hilo, Ally Mayay kwamba 'aliwauma' na kuahidi kuomba pambano la marudiano na wapinzani wao hao ili kukata mzizi wa fitina.
"TUmekubali kipigo, lakini tutaomba mechi ya marudiano, tunaamini leo tumefungwa kwa sababu mwamuzi alikuwa 'wao', hatuamini kama hawa jamaa wana uwezo wa kuwafunga wakati hivi karibuni tuliwanyuka mabao 4-2 baada ya awali kutokana nao sare ya 1-1," alisema Ticotico.
Hata hivyo baadhi ya watazamaji wa mchezio huo wakieleza kipigo walichopewa Golden Bush kilikuwa halali kutokana na kuzidiwa ujanja na Wahenga, huku wakiwapoingeza walioandaa pambano hilo kwa kuwapa burudani ya kuagia mwaka na kuwashuhudia nyota waliotamba zamani katika klabu mbalimbali nchini ambao walikuwa hawajui wapo wapi kwa sasa baada ya kutoweka kwenye ligi kuu.

NYota wa zamani wa soka wataka 2013 uwe wa mapinduzi katika kandanda

Mecky Mexime


NYOTA wa zamani wa soka nchini wamewataka wadau wa mchezo huo kujipanga ili kuhakikisha mwaka 2013 unakuwa wenye tija na mafanikio kwa mchezo wa kandanda baada ya mwaka uliopita wa 2012 kutokuwa na cha kujivunia.
Wakizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa pambano maalum la kuuaga 2012 na kuukaribisha 2013 wachezaji hao wakiongozwa na nahodha wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mecky Mexime, walisema mwaka uliopita ujlikuwa na matukio ya kuumiza katika soka kwa timu za Tanzania kushindwa kung'ara.
Hivyo wakataka mwaka 2013 uwe wa mapinduzi ili Tanzania iweze kurejesha makali yake ya miaka ya nyuma ilipotikisa soka la Afrika.
"Awali ya yote tunashukuru kuweza kukutana wachezaji wa zamani ambao tulipoteana kitambo, lakini kubwa ni kutaka kuona mwaka 2013 unakuwa wa mapinduzi katika soka ili Tanznaia itambe kimataifa," alisema Mexime ambaye kwa sasa ni kocha wa timu ya Mtibwa Sugar.


Katina Shija

Madaraka Seleman
Wengine waliotoa  maoni yao kutaka mwaka 2013 uwe na mabadiliko katika michezo hususani soka ni Yahya Issa, Nico Nyagawa, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio', Katina Shija, Wazir Mahadhi, Zubeir Katwila, kipa Steven Marashi, Onesmo Waziri 'Ticotico', Abuu Ntiro na wengine ambao walikuwa wakiichezea timu ya Golden Bush Veterani waliokuwa wakiumana na Wahenga Fc na kukubali kipigio cha aibu cha mabao 4-3.

KOCHA MFARANSA ATUA SIMBA AAHIDI MAKUBWA

Kocha wa Simba, Mfaransa Liewig akizungumza na waandishi baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana
HATIMAYE kocha mpya wa Simba, Mfaransa Patrick Liewig ametua nchini  na kuahidi kuiletea mafanikio makubwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Liewig aliyekuja kutwaa nafasi iliyoachwa wazi na Mserbia Milovan Cirkovic, amesema 'Wanamsimbazi' watarajie mambo mazuri kutoka kwake, lakini kwa sharti la kumpa ushirikiano katika kila hatua wakati atakaposaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo na kuanza kibarua chake.
"Nimefurahishwa sana na mapokezi haya... najihisi kuwa nina deni kubwa. Naamini nitapata ushirikiano wa kutosha na baada ya kuzoeana na wachezaji, naamini Simba itafika mbali katika kila michuano," alisema kocha huyo.
Miongoni mwa watu waliofika uwanjani kumpokea kocha huyo ni Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, ambaye aliwaongoza mamia ya mashabiki wa Simba kumpokea kwa maandamano ya magari na pikipiki za bodaboda na bajaji.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinaeleza kuwa kocha huyo atasaini mkataba wa kuifundisha klabu hiyo kwa miezi 18 na tukio hilo litakamilishwa leo asubuhi.