STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 1, 2013

NYota wa zamani wa soka wataka 2013 uwe wa mapinduzi katika kandanda

Mecky Mexime


NYOTA wa zamani wa soka nchini wamewataka wadau wa mchezo huo kujipanga ili kuhakikisha mwaka 2013 unakuwa wenye tija na mafanikio kwa mchezo wa kandanda baada ya mwaka uliopita wa 2012 kutokuwa na cha kujivunia.
Wakizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa pambano maalum la kuuaga 2012 na kuukaribisha 2013 wachezaji hao wakiongozwa na nahodha wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mecky Mexime, walisema mwaka uliopita ujlikuwa na matukio ya kuumiza katika soka kwa timu za Tanzania kushindwa kung'ara.
Hivyo wakataka mwaka 2013 uwe wa mapinduzi ili Tanzania iweze kurejesha makali yake ya miaka ya nyuma ilipotikisa soka la Afrika.
"Awali ya yote tunashukuru kuweza kukutana wachezaji wa zamani ambao tulipoteana kitambo, lakini kubwa ni kutaka kuona mwaka 2013 unakuwa wa mapinduzi katika soka ili Tanznaia itambe kimataifa," alisema Mexime ambaye kwa sasa ni kocha wa timu ya Mtibwa Sugar.


Katina Shija

Madaraka Seleman
Wengine waliotoa  maoni yao kutaka mwaka 2013 uwe na mabadiliko katika michezo hususani soka ni Yahya Issa, Nico Nyagawa, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio', Katina Shija, Wazir Mahadhi, Zubeir Katwila, kipa Steven Marashi, Onesmo Waziri 'Ticotico', Abuu Ntiro na wengine ambao walikuwa wakiichezea timu ya Golden Bush Veterani waliokuwa wakiumana na Wahenga Fc na kukubali kipigio cha aibu cha mabao 4-3.

No comments:

Post a Comment