STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 1, 2013

KABURU, WENZAKE WAHOJIWA UPORAJI FEDHA ZA SIMBA

Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange 'Kaburu'

MAKAMU Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ na katibu mkuu wa klabu hiyo, Evodius Mtawala ni miongoni mwa watu waliohojiwa na Jeshi la Polisi jana kusaidia uchunguzi mkali kuhusiana na ujambazi uliosababaisha kuporwa kwa Sh. milioni 10.59 za klabu hiyo zilizotokana na mgawo walioupata katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Tusker ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi.
Akizungumza na jana jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, alisema kuwa wameshawahoji Kaburu, Mtawala na watu wengine kadhaa ili kupata maelezo muhimu yatakayosaidia kupatikana kwa ukweli kuhusiana na kilichotokea.
"Tumewahoji viongozi hao wawili wa Simba (Kaburu na Mtawala) ili kujua taratibu za uhifadhi na utunzwaji wa fedha na mali za klabu yao... maana inastusha kusikia mtu mmoja anakwenda nyumbani kwake na mali ya klabu, tena buila ulinzi wowote ule," alisema Kenyela.
"Tumeamua pia kuwahoji ili kujua hasa ni nini kilichotokea kuanzia Uwanja wa Taifa maana tulibaini kuwa wao (Kaburu na Mtawala) ndiyo waliosaini na kupokea mgawo wa Simba kule uwanjani (Taifa),"  aliongeza.
Kataka hatua nyingine, Kenyela alisema kuwa Mhasibu wa Klabu hiyo, Erick Sekiete na watu wengine wawili, Said Pamba na Stanley Phillipo (23) waliokuwa wakishikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo waliachiwa kwa dhamana jana.
Sekiete na wenzake hao, walivamiwa wakati wakiwa katika eneo la Sinza kwa Remmy baada ya kuteremka katika gari aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T869 BKS iliyokuwa ikiendeshwa na Pamba.
Katika tukio hilo, ilidaiwa kuwa Sh. milioni 7.59 na dola za Marekani 2,000 (Sh. milioni tatu) zilizotokana na mgawo wa klabu hiyo katika mechi yao dhidi ya Tusker FC ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ziliporwa baada ya Sekiete (28) kuvamiwa na majambazi sita katika eneo la  Sinza kwa Remmy jijini Dar es Salaam ambapo risasi kadhaa zilipigwa hewani. Tukio hilo lilitokea saa 3:20 usiku.
Kamanda Kenyela alieleza kuwa Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alimdhamini Sekiete huku Phillipo akidhaminiwa na ndugu yake aitwaye Julius Kiwale.
Kamanda Kenyela alisema kuwa Pamba, ambaye alikuwa dereva wa gari lililowabeba Sekiete na Phillipo, alidhaminiwa na Kasim Pamba.
“Wanatakiwa waripoti katika Kituo cha Polisi Magomeni Jumatano (kesho),” aliongeza Kenyela.


Chanzo;NIPASHE
----------

No comments:

Post a Comment