STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 3, 2013

SAJUKI  KUZIKWA KESHO MAKABURI YA KISUTU

Sajuki akichapa mzigo enzi za uhai wake
Sajuki na mkewe Wastara enzi za uhai wake
Baba yake Sajuki... Mzee Kilowoko akiwasiliana na ndugu na jamaa kwa simu wakati akiwa kwenye msiba wa mwanawe, Tabata jijini Dar es Salaam jana. Familia imeamua Sajuki azikwe makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam kesho Ijumaa.

Wasanii wa vichekesho, Mtanga (kushoto) na Kiwewe (aliyejishika goti) wakiwa na waombolezaji wengine katika msiba wa Sajuk.

Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu Sajuki
Tutakukumbuka milele Sajuki... msanii nyota wa filamu za Kibongo, Suzan Lewis 'Natasha' akiwa kwenye msiba wa Sajuki mapema leo kushiriki maandalizi ya shughuli za mazishi, eneo la Tabata jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya waombolezaji wa msiba wa Sajuki waliofika mapema Tabta

Piga pale...! Sajuki (kulia) akiwa katika maandalizi ya filamu yake ya Vita wakati wa enzi za uhai wake.


Waombolezaji wakiwa na majozni tele katika msiba wa Sajuki, Tabata jijini Dar es Salaam.
HATIMAYE ule utata kuhusiana na mahala pa kumzika msanii Juma Kilowoko 'Sajuki' umepatiwa jibu baada ya baba yake kukubali kuwa azikwe jijini Dar es Salaam.

Kutokana na uamuzi huo, sasa msanii huyo aliyekuwa nyota na kipenzi cha wengi enzi za uhai wake atazikwa kesho 
saa 7:00 mchana baada ya swala ya Ijumaa kwenye makaburi ya Kisutu.

Awali, baba wa msanii huyo alitaka mwanawe akazikwe kwao mkoani Songea. Hata hivyo, baada ya kuketi na kujadili kwa kina na familia yake, akaamua kutangaza kuwa mwanawe huyo kipenzi atazikwa jijini Dar es Salaam ili kutoa nafasi kwa rafiki zake wengi aliokuwa akishirikiana nao katika kazi zake za kila siku za kisanii kupata nafasi ya kushiriki mazishi yake.

Mzee Kilowoko ametoa msimamo huo mpya leo hoo hii, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kutangaza awali kuwa mwanawe atakwenda kuzikwa Songea.

Sajuki amefariki leo asubuhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa katika wodi ya wagonjwa mahututi na kupumua kwa msaada wa mashine kabla ya kuaga dunia mishale ya saa 1:00 asubuhi.



Mashabiki wa filamu za Kibongo nchini watamkumbuka marehemu kwa filamu zake kama 'Round', 'Shetani wa Pesa', 'Hero of the Church', 'Vita' na 'Briefcase, 'Revenge', 'Dhambi', 'Mboni Yangu', 'Two Brothers', na'Behind the Scene'.
Sajuki alizaliwa mwaka 1986 Songea mkoani Ruvuma, ameacha mke na mtoto mmoja.

No comments:

Post a Comment