STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 3, 2013

Thomas Mashali kuuanza mwaka dhidi ya Mkenya

 
Bondia Thomas Mashali
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini Thomas Mashali anatarajiwa kupanda ulingoni Januari 12 katika ukumbi wa Friends Corner Manzese Jijini Dar es Salaam kutetea Ubingwa wa Afika  Mashariki.
 
Akiongea na waandishi wa habari Mratibu wa pambano hilo Aisha mbegu alisema mashali atapambana kuzipiga na Mkenya Bernard Mackoliech mpambano utakaokuwa wa raundi 10.
 
Alisema maandalizi yamekamilika ikiwa pia na kutumiwa tiketi kwa bondia huyo mkenya ambaye anatarajiwa kuwasili januari nane kwa ajili ya kupima uzito na kupanda ulingoni.
 
“tunataraji mpambano utakuwa mkali wa kukata na shoka ukizingatia mashali ameweka kambi kwa muda mrefu nje ya mkoa lakini pia Mackoliech ni bondia mahiri ambaye anasaka rekodi ya kwenda kucheza nje ya nchi”,alisema Aisha.
 
Alisema nafasi iko wazi kwa watu wanaotaka kudhamini ili kuhakikisha mpambano huo unafanikiwa ukizingatia ndio mpambano wa kwanza kwa mwaka 2013 na pia mashali anavutia mashabiki wengi.
 
Kwa upande wake rais wa TPBO amesema mapambano ya utangulizi yanatarajiwa kuwa manne na mabondi tayari wamesaini mikataba na watatangazwa hivi karibuni.
 
Bondia Thomas Mashali anatetea ubingwa huo wa Afrika mashariki na kati ambao aliupata baada ya kumpiga Mganda Medi Sebyala Jijini Dar es salaam mpambano uliohudhuriwa na mashabiki lukuki.
 
Mwisho.

No comments:

Post a Comment