STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 3, 2013

Chelsea hoi wa QPR, Liverpool yazidi kupeta

Wachezaji wa QPR wakimpongeza Shaun Wright Phillips aliyefunga bao pekee lililoiangusha Chelsea jana usiku.

WAKATI Liverpool ikiendeleza wimbi la ushindi kwa kuisambatarisha timu ya Sunderland kwa mabao 3-0, Chelsea walijikuta wakiteleza nyumbani kwao uwanja wa Stanford Bridge kwa kudunguliwa bao 1-0 na 'vibonde' wa Ligi Kuu ya England, QPR inayonolewa na kocha Harry Redknapp.
Chelsea ilikumbana na kipigo hicho kutokana na bao la nyota wake wa zamani Shaun Wright-Phillips aliyefunga katika dakika ya 78 kutokana na kazi nzuri ya Mmorocco Adel Taarabt.
Kipigo hicho kimeiacha Chalsea kwenye nafasi ya nne ikiwa na pointi 38 ikishindwa kuipiku Tottenham waliowazidi pointi moja wanaokamata nafasi ya tatu nyuma ya Manchester City na Manchester United.
Liverpool wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumba waliinyoa Sunderland kwa mabao 3-0, mabao wawili yakitupiwa kambani na Luis Suarez, huku bao la awali likifungwa na Raheem Sterling akimalizia kazi ya Suarez.
Katika mechi nyingine ya mfululizo wa ligi hiyo Newcastle United imeendeleza wimbi la vipigo kwa kulala nyumbani kwao mabao 2-1 toka kwa Everton.

No comments:

Post a Comment