STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 3, 2013

Golden Bush Veterani, Wahenga Fc kurudiana Januari 12

Kikosi cha Golden Bush Veterani ambacho kinatarajiwa kurudiana na Wahenga Fc Januari 12

BAADA ya kukaribisha mwaka kwa kipigo cha aibu cha mabao 4-3 kutoka kwa wapinzani wao, timu ya soka ya Golden Bush Veterani, imekata rufaa na sasa watarudiana na wapinzani wao Wahenga Fc Januari 12.
Tayari pande zote zimekuwa zikitoleana tambo mbalimbali Wahenga wakisisitiza kuwa waliamua kutoa zawadi ya mwaka mpya kwa watani zao kwa kuwapa kipigo hicho, huku Golden Bush kikisisitiza kuwa waliotewa na kwamba mechi hiyo ya kisasi wataifumua Wahenga mabao 7-0.
Golden Bush tayari kimeweka hadhaarani kikosi kitakachoshuka dimbani siku ya mechi hiyo ambapo golini atakuwepo Hamza, kipa wa timu yao ya vijana huku kulia atasimama Chidi Rasta, kushoto Abuu Ntiro, Mmalawi Wisdom Ndhlovu atacheza kama beki namba nne na mkoba atakuwa Majaliwa.
Kiungo nama sita atacheza Yahya Issa, wingi ya kulia atasimama mlezi wao, Onesmo Wazir 'Ticotico' na Katina Shija atazungusha dimba la juu, Herry Morris atacheza kama mshambuliaji wa kati na Kapeta atacheza namba 10 na Said Swedi Panucci atacheza wingi ya kushoto.
Pamoja na Golden Bush kujinasibu kushinda mchezo huo wa marudiano, Wahenga wamekejeli wakieleza kuwa wao hawana hofu yoyote kwa sababu soka wanalijua japo wachezaji wao hawana majina makubwa kama ya wapinzani wao ambao katika mechi zao mbili za awali walitoka sare ya 1-1 na kisha kuwanyuka mabao 4-2 kabla ya kuwazima wiki mwishoni mwa wiki kwa mabao hayop 4-3 mechi zote zikichezwa kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Dar es Salaam.

Je, nani atakayeiobuka na ushindi? Tusubiri kuona hiyo Januari 12.

No comments:

Post a Comment