STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 24, 2014

Hatimaye wazee wa Uturuki watua salama Dar

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom nchini Tanzania Bara, Yanga wameshawasili salama jijini Dar es salaam wakitokea jijini Antalya nchini Uturuki walipokuwa wameweka kambi ya wiki mbili kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Young Africans imetua uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl JK Nyeree majira ya saa 9:30 alfajiri kwa shirika la ndege la Turkish Airline na moja kwa moja kikosi cha wachezaji 27 na benchi la Ufundi kimeingia kambini kujiandaa na mchezo huo wa kesho.
Kocha mkuu wa Young Africans Hans Van Der Plyum amesema anashukuru kikosi chake kimefika salama jijini Dar es salaam na amesema vijana wake watafanya mazoezi mepesi leo jioni kabla ya kesho kushuka dimba la Uwanja wa Taifa.
Akiongelea kambi ya Antalya Hans amesema kambi ilikuwa nzuri na mafanikio makubwa kwani vijana wameonyesha uwezo wa hali ya juu katika nidhamu, kujituma, upendo na kushirikiana kitu ambacho ndio nguzo ya timu kufanya vizuri.
Aidha Hans amewaomba wanachama wa Young Africans, wapenzi na washabiki kesho kujitokeza kwa wingi kuja kuishuhudia timu yao iliyokuwa kambini Uturuki itakapocheza na wauza mitumba wa Ilala Ashanti United na kuitambulisha staili yao ya uchezaji kutoka Antalya.

Mtibwa Sugar yaikamia Azam


Kocha wea Mtibwa Mecky Mexime
KOCHA wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime amesema vijana wake wapo tayari kuvaana na Azam kwenye mechi ya fungua dimba la duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoanza kesho akisema ama zao au za Azam.
Mexime alisema maandalizi waliyofanya na mechi chache za kujipima nguvu walizocheza yamewafanya wachezaji wake kuiva tayari kuipigania timu yao ili iweze kufanya vyema kwenye duru hilo aliloliita la 'kufa au kupona'.
Mtibwa waliomaliza kwenye nafasi ya sita katika duru la kwanza watakuwa wageni wa Azam kwenye uwanja wa Azam Complex, huku wakiwa na rekodi ya kutoka sare ya 1-1 katika mzunguko wa kwanza.
"Tunashukuru vijana wangu wote wapo fiti, hakuna majeruhi hata mmoja na tunamalizia maandalizi ya mwisho kabla ya kuja Dar kuvaana na Azam. Tumepania kupata ushindi ili kujiweka pazuri," alisema Mexime.
Nahodha huyo wa zamani wa Mtibwa na Taifa Stars, alisema anafahamu Azam ni timu nzuri na imekuwa ikiwapa upinzani wanapokutana nayo, lakini safari hii wanakuja kivingine kuhakikisha wanapata ushindi mechi zao za ugenini.
"Ingawa Azam ni timu ngumu na isiyotabirika, lakini wajiandae kwa kipigo kwa sababu tumepania duru la pili tufanye vizuri zaidi na ilivyokuwa duru la kwanza," alisema Mexime anayesaidiana na wachezaji wenzake wa zamani, Zuberi Katwila na Patrick Mwangata.

TFF yaonya makocha, wasemaji wa timu kuhusu uchochezi

Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawakumbusha makocha na maofisa habari wa klabu za Ligi Kuu kujiepusha na kauli za chuki, uchochezi
na uongo kwa shirikisho na waamuzi kila timu zao zinapofanya vibaya kwenye mechi.

Ni wajibu wa makocha kuzungumzia matokeo ya timu zao kiufundi badala ya kushambulia waamuzi na TFF kwa maneno makali. 
 
Pia maofisa habari nao wanatakiwa kuwa makini katika kauli zao kuhusiana na matokeo na masuala
mengine.

Kwa wale watakaokwenda kinyume TFF itawafikisha kwenye vyombo vya kinidhamu na maadili kwa ajili ya kuchukuliwa hatua stahiki.

Mechi zote tiketi za Elektroniki isipokuwa Taifa, soma vituo vilipo

Uwanja wa Taifa ambao utaendelea kukamua kikawaida
VIWANJA vyote ambavyo tayari vimefungwa mfumo wa elektroniki vitatumia tiketi za elektroniki isipokuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambao wenyewe utachelewa kidogo ili kuangalia kwanza mfumo huo unavyofanya kazi katika viwanja vingine.

Kwa viwanja vinavyotumia mfumo huo tiketi zinanunuliwa kupitia mtandao wa Vodacom ambapo mteja ni lazima awe amesajiliwa katika MPESA. Ataanza kwa kupiga *150*03*02# ambapo atapewa namba ya kumbukumbu anayotakiwa kuihifadhi kwani ataulizwa wakati anafanya malipo kwa kupitia MPESA ambapo ataingia kama kawaida kwa kutumia *150*00#.

Baada ya kulipa atapewa namba ya tiketi ambapo atakwenda kwenye mashine maalumu za kuchapa (printer) ambazo ziko katika vituo mbalimbali na kuchapa tiketi hiyo ambayo ndiyo atakayokwenda nayo uwanjani.
Njia nyingine ya kununua ni kwa wateja wa benki ya CRDB ambayo wamejisajili kwenye simbanking. Wao wataingia kwa kutumia *150*03# na kufanya malipo ya tiketi. Nao baada ya kupata namba watakwenda ku-print tiketi kwenye mashine hizo maalumu.
Vilevile tiketi zinapatikana kupitia maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo katika maeneo mbalimbali nchini. Watakaonunua kupitia maduka hayo watapata tiketi na kwenda moja kwa moja uwanjani.

*DAR ES SALAAM*
Kwa mechi za Dar es Salaam (Uwanja wa Azam) ambao ndiyo unaanza kutumia tiketi za elektroniki maduka ya CRDB Fahari Huduma yanayouza tiketi hizo ni; 
1 Shs Distributors Limited (Mtoni Kwa Aziz Ally),
ABC Computer (Mtaa wa Samora), Abdi Ally Abdi (Kariakoo), Aika- El Traders (Africana), Amaly Investment (Mtaa wa Sikukuu, Kariakoo), Athuman Fakhi Adam (Kongowe, Mbagala) na Bemuda Supplies Agency (Tegeta- Kibo Complex).
Benedict Traders (Barabara ya Uhuru/Lumumba), Ellytex Investment (Mtaa wa Indira Gandhi), Fedha Investment Limited (Pamba Road), Fuya Godwin Kimbita (Tegeta Block E), Hakika Limited (Mtaa wa Swahili, Kariakoo), Irice Stationary (Tegea Kwa Ndevu), Joshua Andrew Kisamo (Mtaa wa Kongo, Kariakoo), LB Pharmacy (Mtoni Kijichi) na Lista Phares Barnabas (Tabata Segerea).
L.M.S. Agro Chemical (Sokoni Kariakoo), Matei Laurent Kiria (Mbuyuni,
Kinyerezi), Michael Elisante Mchomvu (Mtaa wa Sikukuu, Kariakoo), Palmall General Supplies (Barabara ya Shekilango), Rafabi Communications (Mtaa wa Livingstone, Kariakoo), Therry Inestment Limited (Tegeta Kibaoni) na Wemerick Independent Vehicle Diagnostic Company Limited (Mtaa wa Boko).

Mashine za kuchapia tiketi zipo matawi ya CRDB Azikiwe, Holland House (mashine mbili), Kariakoo, Tabata, Tegeta, Mbezi beach, Vijana na Quality
Center. Mashine nyingine maeneo ya ATM ya Mtaa wa Shaurimoyo (mbili), Kawe Oilcom, Tabata Camel, Manzese, Ubungo Oilcom, Sabasaba na Mbagala Oilcom.

*BUKOBA*

Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Tak-Biir Investment Company (Mtaa wa
Jamhuri, Bilele), Mary Mother of Peace Buhembe School (Sido Block,
Rwamishenye), Muleba Secretarial Bureau (Nyerere Road), Akimu Abdallah
Tirutoijwa (Mtaa wa Forodhani), Jamila Rajabu Songoro (Mtaa wa Jamhuri, Bilele), Rukia Kassim Mohamed (Mtaa wa Kashai, Kashenye) na Novath Michael Kibira (Uganda Road, Majengo).

Mashine tatu za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi laBukoba.

*TANGA*

Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Fax Auction Mart (Sabasaba Ground, Korogwe Road) na Rozalia Aloyce Masanja (Usagara, Block K). Mashine tatu za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Tanga.

*MBEYA*
 
Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Blue Bird Bureau de Change (Lupa way), Meenda Pharmacy Limited (Maendeleo), Access Computer Limited (Lupa way,
Sisimba) na Japhes James Mwanjisi (Mtaa wa Njisi). Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Mbeya (mbili), Tawi la Mwanjelwa na Uyole.

*MOROGORO*

Duka la CRDB Fahari Huduma ni Shambani Graduates Enterprises Limited (Kihonda) na pia kutakuwa na gari za CRDB (Mobile bank). Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Morogoro, Msamvu na Morogoro Agency.

*ARUSHA*

Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Fanuel John Andrew (Arumeru, Maji ya Chai),
Robert William Maeda (Arumeru, Usa River), Wakwetu General Supplies (Mtaa
wa Ngongongare, Arumeru), Wallace Ndawonga Mtawa (Kimandolu Suye), Side
Corner Multi Business (Levolosi, Makao Mapya Street) na Albertha Ibrahimu
General (Usa River Bus Stand).

Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo Benki ya CRDB Tawi la Arusha
(mbili), Tawi la Meru, TFA, TRA Mapato na Ngaramtoni.

*MWANZA*

Maduka ya CRDB Fahari Huduma ni Majura General Supplies (Mecco Street),
Prisca Joachim Kitani (Gilishi Street), Niche Consult (Nyerere Road),
Deogratias Just Silayo (Malimbe, Mkolani), Yohana Ndili Mahago (Igoma
Mashariki), Emily Elias Sambo (Sweya Street), Y Financing Limited
(Kilimahewa) na Mangare Office Solutions (Station Road).

Makoye E. Serikali (Ilemela, Kiseke Street), Elizabeth George Kiwia (Uhuru
Road), Mwalimu General Services (Kitangiri Road), George Edward Mulambo
(Pasiansi), Nginila Office Solutions (Rufiji Street), Elvando IT Solutions
(Nkrumah, Nyamagana), Sarimosa Company Limited (Kaluta Street) na Sahara
Trasport and Scrappers Dealers (Mission, Pamba Road).

Mashine za kuchapia tiketi (printers) zipo CRDB matawi ya Mwanza, Nyerere
na Mwaloni wakati nyingine zipo Nyanza, Buzuruga na Ilemela.

Kivumbi cha Ligi Kuu Tanzania Bara kuanza kutimka wikiendi hii

Wazee wa Uturuki watakaovaana na Ashanti Utd kesho Taifa

Ashanti Unitrd weatakubali 5 nyingine kwa Yanga?
 MZUNGUKO wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza kesho (Januari 25 mwaka huu) kwa mechi nne zitakazochezwa katika miji ya Bukoba, Dar es Salaam na Tanga.
Mabingwa watetezi Yanga watakuwa wageni wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati kwenye jiji hilo hilo Uwanja wa Azam Complex kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Azam FC na Mtibwa Sugar kutoka Morogoro.
Coastal Union na Oljoro JKT zitaumana kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, huku Kagera Sugar ikiikaribisha Mbeya City kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Raundi ya 14 ya ligi hiyo itaendelea Jumapili (Januari 26 mwaka huu) kwa mechi mbili. Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam utakuwa shuhuda wa mechi kati
ya Simba na Rhino Rangers kutoka Tabora wakati maafande wa JKT Ruvu na Mgambo Shooting watapambana Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.
 
Viingilio kwenye mechi ya Ashanti United na Yanga vitakuwa sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Viingilio mechi ya Mkwakwani vitakuwa sh. 10,000 kwa sh. 3,000, Uwanja wa Azam Complex sh. 10,000 kwa sh. 3,000, Uwanja wa Kaitaba ni sh. 5,000 kwa sh. 3,000.

TASWA FC, TASWA QUEENS KUPAMBA BONANZA LA MSONDO KESHO JUMAMOSI

TIMU za soka na netiboli ya waandishi wa habari za michezo nchini, Taswa FC na Taswa Queens kesho Jumamosi zitapamba katika bonanza la muziki la bendi ya Msondo Ngoma kwa kupambana na timu za veterans za Bandari wanaume na wanawake.
Mchezo huo umepangwa kufanyika kwenye uwanja wa TCC, Chang’ombe kuanzia saa 8.00 mchana na maandalizi yake yamekamilika kwa mujibu wa mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary. 
Majuto alisema kuwa mechi hizo zinatarajiwa kuwa ngumu na za kusisimua kutokana na rekodi ya timu zote mbili.
Majuto alisema Taswa FC na Taswa Queens hazijawahi kupoteza mechi yoyote mwaka uliopita na kuweza kutwaa vikombe mara mbili mkoani Arusha na hivi karibuni waliweza kuzichapa timu ya wanamuziki wa Twanga Pepeta, Kombaini ya Leaders Club na shirika la maendeleo ya mafuta (TPDC).
Alisema kuwa timu zake zitakuwa zinacheza kwa mara ya kwanza mwaka huu kwenye uwanja wa TCC na hivyo mashabiki watarajie kupata burudani safi ya mpira na muziki kutoka kwa bendi ya Msondo Ngoma ambayo itatambulisha nyimbo zake mpya ambazo zitakuwa zinatambulishwa kwa mara ya kwanza.
“Tutaanza kutoa burudani kwa mashabiki na baadaye kuamia kwa Msondo Ngoma, tunatarajia kuwapa burudani safi ambayo itakuwa ya kwanza mwaka huu, mbali ya mechi yetu, timu ya Mass itapambana na Farion, ambapo timu ya maveterani wa Temeke inayojiita kwa jina la Kamazamani itapambana na timu ya Tall, “ alisema Majuto.
Wakati huo huo; bendi ya Msondo ngoma na Twanga Pepeta, jumapili zitatumbuiza jukwaa moja kwenye ukumbi wa CCM Kata 14, Temeke. Burudani hiyo itakuwa ya kwanza mwaka huu kwa wakazi wa Temeke na vitongoji vyake kwa bendi hizo kupiga pamoja. Twanga itaonyesha shoo na nyimbo zake mpya.

Ushindani wa namba Simba wamkuna Ali Badru


USHINDANI wa kugombea namba kwa wachezaji wa Simba umemkosha mshambuliaji mpya wa klabu hiyo, Ali Badru, akisema utaisaidia timu yao kuwa kali zaidi kwenye duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoanza kesho.
Akizungumza na MICHARAZO, Badru alisema mpaka sasa ndani ya Simba hakuna mwenye uhakika wa namba, kitu ambacho kinawafanya wachezaji wasilale ili kupigania kupata nafasi chini ya kocha Zdravko Logarusic anayeinoa timu hiyo.
Badru aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo akitokea nchini Misri, alisema kama mchezaji anayejitambua, anafurahia hali ya ushindani wa kugombea namba baina yake na wachezaji wenzake akiamini ni nafasi ya kuonyesha uwezo aliojaliwa.
"Kwa kweli nafurahishwa na ushindani wa namba uliopo Simba, unatufanya wachezaji wote kuwa macho na kuongeza bidii ili kuwaridhisha makocha na hali hii inasaidia kuongeza viwango vyetu," anasema.
Badru anayeichezea timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes), alimmwagia sifa kocha Logarusic kwamba ni 'bonge' la kocha kuwahi kumfundisha soka na kuitabiria Simba kufika mbali chini ya mtaalam huyo kutoka Croatia.
"Siyo siri nimefundishwa na makocha mbalimbali, lakini kati yao sijaona kama Loga, huyu jamaa ni bonge la kocha na kama atadumu na klabu naamini Simba itafika mbali, anajua kazi yake na anahamasisha sana wachezaji kujituma," alisema.
Simba iliyomaliza duru la kwanza la ligi chini ya kocha aliyetimuliwa Abdallah Kibadeni na kushika nafasi ya nne, itaanza kibarua cha duru la pili siku ya Jumapili kwa kuikaribisha Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Taifa.
Katika pambano lao la awali lililochezwa kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya mabao 2-2.

HUU NDIYO UKWELI KUHUSU USAJILI WA OKWI YANGA










Hati ya Usajili wa Emmanuel Okwi kama inavyoeneka kwneye system ya CAF
Uongozi wa klabu ya Young Africans umeamua kuweka hadharani ukweli kuhusiana na usajili wa mshambuliaji wake wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi ambaye kamati ya maadili na hadhi za wachezaji imemzuia kuichezea Young Africana mpaka watakapopata uthibitisho kutoka FIFA.
Young Africans ilikamlisha usajili wa mshambuliaji huyo tangu Disemba 15 mwaka 2013, na kupata hati ya uhamisho wake wa kimataifa (ITC) ambayo iliwasilishwa TFF pamoja na fomu mama za usajili wa Ligi Kuu ya Vodacom.
Baada ya kukamilisha zoezi hilo TFF ilipitisha jina lake kwa kutupatia leseni no: 921225001 ambayo inamruhusu mchezaji kuichezea Young Africans na kisha kulituma CAF Disemba 31, 2013 kwa ajili ya mashindano ya Klabu Bingwa barani Afrika  ambapo CAF nao walimuidhinisha kuwa mchezaji halali wa Young Africans kwa mashindano hayo. 
Cha kustaajabisha siku mbili kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya Vodacom Kamati ya Maadili na hadhi za wachezaji wakamzuia mchezaji huyo kuichezea Young Africans ilihali akiwa ameshaidhinishwa na TFF na CAF kuwa mchezaji halali wa Young Africans.
Swali?? walikuwa wapi Kamati ya Maadili na Hadhi za Wachezaji kujiridhisha juu ya usajili ambao ulishakamilika tangu Disemba 15 2013? 
Wanakuja kutoa maamuzi hayo mwezi mmoja na nusu baada ya dirisha la usajili kufungwa, ikiwa ni siku mbili kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom??
YOUNG AFRICANS

Juma Jabu kuwakosa Yanga kesho Taifa

Juma Jabu enzi akiwa Simba
BEKI wa zamani wa Simba na Coastal Union aliyetua Ashanti United, Juma Jabu 'Jay Jay', amesikitika kuwakosa mabingwa watetezi Yanga wanaorejea leo kutoka Uturuki katika mechi yao ya la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayochezwa kesho.
Beki huyo wa pembeni hatacheza mechi hiyo itakayochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutokana na kutingwa na majukumu yake ya masomo kwani kwa sasa mchezaji huyo anasoma katika Chuo cha DSI.
Akizungumza na MICHARAZO, Jabu alisema alikuwa na hamu kubwa ya kuivaa Yanga katika mechi hiyo, lakini amelazimika kuomba ruksa kwa 'mabosi' wake ili kujiandaa na mitihani.
Jabu alisema kwa sasa anasomea masomo ya 'Clearing and Forwading' katika chuo hicho na hivyo kipindi hiki yupo katika mitihani, japo mechi ijayo ambayo Ashanti itaikaribisha Mgambo JKT uwanja wa Chamazi, atakuwepo.
"Nasikitika sitaweza kucheza mechi ya Jumamosi dhidi ya Yanga kwa sasa nipo kwenye mitihani, lakini mechi ijayo dhidi ya Mgambo naamini nitaanza kuitumikia rasmi klabu yangu ya Ashanti niliyorejea tena," alisema.
Jabu, alisema anaamini wachezaji wenzake chini ya kocha mpya Abdallah Kibadeni, wataiduwaza Yanga waliokuwa wakijifua Uturuki kwa karibu wiki mbili kwa kuipa kipigo ili kulipa kisasi cha mabao 5-1 walichopewa katika mechi ya kwanza ya msimu huu.
Beki huyo aliyeichezea Ashanti United iliposhiriki Ligi Kuu kwa mara ya kwanza mwaka 2004-2007, ni miongoni mwa wachezaji 15 walioongezwa kwenye kikosi cha Ashanti kwenye usajili wa dirisha dogo.

Hii ndiyo orodha kamili ya watu mashuhuru wanaodaiwa kuwa Freemason



Here comes 2014 official list finally exposed  and so few list out of 300 Official board committee sponsoring them is also here for 2014 see the list below for the special committee: full list:
*CURRENT MONARCH AND SUPREME LEADER OF THE NWO:
Queen Elizabeth II
Abdullah II of Jordan

Kerry John 
Forbes 
Abramovich Roman 
Arkadyevich King,
Mervyn Ackermann,
Josef Kinnock,
Glenys Adeane,
Edward Kissinger,
Henry Agius,
Marcus Ambrose 

Paul Knight,
Malcolm 

Ahtisaari 
Martti Oliva 
Kalevi Koon
William H. II 


Akerson
Daniel Krugman,
Paul Albert II of Belgium

Kufuor
John Alexander – Crown Prince of Yugoslavia

Lajolo Giovanni 
Alexandra (Princess) – The Honourable Lady Ogilvy Lake Anthony 
Alphonse Louis – Duke of Anjou
Lambert Richard
Amato Giuliano
Lamy Pascal 
Anderson Carl
A. Landau,
 Jean-Pierre Andreotti,
 Giulio Laurence,
Timothy James 

Hamilton Andrew (Prince) – Duke of YorkLeigh-Pemberton James
Anne – Princess Royal
Leka Crown Prince of Albania 
Anstee Nick
Leonard Mark 
Ash Timothy 
Garton Levene,
Peter Baron Levene of Portsoken 

Astor William Waldorf – 4th Viscount AstorLeviev,
Lev August,
Ernst – Prince of Hanover

Levitt, Arthur Aven,
PyotrLevy, Michael – 

Baron Levy Balkenende,

NOW LIST OF THE LATEST WORLD CELEBRITIES IN THE ILLUMINATI FOR 2014
There hasn't been much people on the list for 2014, but its finally exposed from our source that two popular football players "BALE" and "LIONEL MESSI" and others are already on the list.

Aalyiah - Illuminati
Adele - Illuminati
Alicia Keys - Illuminati
Angelina Jolie - Illuminati
Avril Lavigne - Illuminati
Barack Obama - Illuminati
BALE(football player)- illuminati
Barcelona FC- Illuminati
Beyonce Knowles - Illuminati
Blue Ivy - Illuminati
Bob Dylan - Illuminati
Bob Marley - Illuminati
Bono (from U2) - Illuminati
Britney spears - Illuminati
Cash Money/Young Money Records - Illuminati
Celine Dion - Illuminati
Chris Brown - Illuminati
Ciara - Illuminati
Cristiano Ronaldo - Illuminati
Cypress hill - Illuminati
Darren Brown - Illuminati
David bowie - Illuminati
Disturbed - Illuminati

Dr. Dre - Illuminati
Drake - Illuminati
Eminem - Illuminati
George W. Bush Sr. & Jr. - Illuminati
George Washing (was a Freemasonry) - Illuminati
Gordon Brown - Illuminati
Hugo Weaving - Illuminati
Hulk Hogan - Illuminati
Jay-Z - Illuminati
Jennifer Hudson - Illuminati
Jennifer Lopez - Illuminati
Jim Carey - Illuminati
Jimi Hendrix - Illuminati
John Cena - Illuminati
cm punk - Illuminati
John Travolta - Illuminati
Justin Bieber - Illuminati
Kanye West - Illuminati
Katty Parry - Illuminati
Keith Urban - Illuminati
Ke$ha - Illuminati
Kevin Nash - Illuminati
Kid Cudi - Illuminati
Kim Kardashian - Illuminati
Kobe Bryant - Illuminati
Kris Angel - Illuminat
Kyle Monogue - Illuminati
Lady Gaga - Illuminati
L'arc en Ciel - Illuminati
Laruku from Japan - Illuminati
Lebron James - Illuminati
Lil Wayne - Illuminati
Linkin Park - Illuminati
Liverpool FC - Illuminati
Lionel Mess- Illuminati
Madonna - Illuminati
Manchester UTD - Illuminati
Marilyn Manson - Illuminati
Michael Jackson (Former member turned against Illuminati) 

Miley Cyrus - Illuminati
Nas - Illuminati
Natalie Portman - Illuminati
Nelson Mandela - Illuminati
Ne-Yo - Illuminati
Nicki Minaj - Illuminati
Notorious B.I.G - Illuminati
One Direction - Illuminati
P. Diddy (aka Puff Daddy) - Illuminati
Paul Mccartney - Illuminati
Paul Mkenna - Illuminati
Queen Elizabeth (& entire royal family) - Illuminati
Randy Orton - Illuminati
Real Betis - Illuminati
Rihanna - Illuminati
Scott Hall - Illuminati
Sean Waltmen - Illuminati
Selena Perez - Illuminati
Serena Williams - Illuminati
Taylor Alison Swift - Illuminati
T pain - Illuminati
The Dudley Boys - Illuminati
The Mizz - Illuminati
The Pretty Reckless (Taylor Momsen!) The White Stripes - Illuminati
Tom Cruise - Illuminati
Tony Blair - Illuminati
Tupac Shakur (but then turned against them as well) Vitas (Russian Male Singer) - Illuminati
Warren Buffet - Illuminati
Whitney Houston (former member with claims of being murdered by Illuminati) 

Willow Smith (quoted as "Next Illuminati Star") 
Wiz Khalifa - Illuminati
YeahYeahYeahs - Illuminati
Yelawolf - Illuminati 
THE CHOICE

Rais wa TPBO, Ustaadh Yasin 'aula' Afrika Mashariki na Kati


RAIS wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Limited) Yasin Abdallah 'Ustaadh' (pichani) ameteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa la Afrika Mashariki na Kati (ECAPBA).
Kwa mujibu wa taarifa ya Rais wa ECAPBA ambaye pia ni Rais wa IBF-USBA, Onesmo Ngowi uteuzi umefanywa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo la ECAPBA kilichofanyika Januari 4 mwaka huu jijini Kigali, Rwanda kilichofanya mabadiliko ya kujaza nafasi za uongozi wa shirikisho lao.
Ngowi alisema Ustaadh amechukua nafasi  kuchukua nafasi ya Celestino Mindra kutoka Uganda aliyekuwa Rais wa Baraza la Ngumi za Kulipwa za nchi hiyo (UPBC).
Mbali na Ustaadh wengine walioteuliwa kwenye kikao hicho ni Simon Kategole wa Uganda, aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa ECAPBA kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Shaaban Ogolla wa Kenya ambaye yuko masomoni nchini Marekani.
Pia Daudi Chikwanje wa Malawi anachukua nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa ECAPBA, huku Nelson Sapi wa Zambia ameteuliwa kuwa Naibu Mweka Hazina wa ECAPBA akimsaidia Nemes Kavishe wa Tanzania.
Boniface Wambura wa Tanzania amebaki katika nafasi yake ya Afisa Habari wa ECAPBA wakati wajumbe wanne wameongezwa kwenye Kamati ya Utendaji ambao ni kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Malawi na Ethiopia pamoja na Roman Chuwa wa Arusha.
Aidha, ECAPBF imemshukuru Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Gaudence Lyimo kwa kukubali kuwa mlezi wake na kuipatia ofisi katika Manispaa ya jiji la Arusha kikiwa ndicho Chombo cha michezo kinachounganisha vijana cha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
"Katika malengo yake, ECAPBA itafanya kazi kwa karibu sana na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) ili iweze kuwa chachu ya utekelezaji wa maamuzi ya Jumuiya katika ukanda wa Afrika ya Mashariki na Kati," taarifa hiyo ya Ngowi inasema na kuongeza.
"Kwa kutambua kuwa, Jumuiya ya Afrika ya Mashariku ni chombo cha uchumi cha kuunganisha nguvu za watu wa Afrika ya Mashariki, ECAPBA imedhamiria kuyafanyia utekelezaji maamuzi yote yanayohusu maendeleo ya vijana pamoja na ushirikiano wa utamaduni na michezo wa EAC. Aidha, ECAPBA imedhamiria kuleta chachu katika kujenga nguvu na kutengeneza ajira kwa vijana wa Afrika ya Mashariki na Kati."