STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 24, 2014

TASWA FC, TASWA QUEENS KUPAMBA BONANZA LA MSONDO KESHO JUMAMOSI

TIMU za soka na netiboli ya waandishi wa habari za michezo nchini, Taswa FC na Taswa Queens kesho Jumamosi zitapamba katika bonanza la muziki la bendi ya Msondo Ngoma kwa kupambana na timu za veterans za Bandari wanaume na wanawake.
Mchezo huo umepangwa kufanyika kwenye uwanja wa TCC, Chang’ombe kuanzia saa 8.00 mchana na maandalizi yake yamekamilika kwa mujibu wa mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary. 
Majuto alisema kuwa mechi hizo zinatarajiwa kuwa ngumu na za kusisimua kutokana na rekodi ya timu zote mbili.
Majuto alisema Taswa FC na Taswa Queens hazijawahi kupoteza mechi yoyote mwaka uliopita na kuweza kutwaa vikombe mara mbili mkoani Arusha na hivi karibuni waliweza kuzichapa timu ya wanamuziki wa Twanga Pepeta, Kombaini ya Leaders Club na shirika la maendeleo ya mafuta (TPDC).
Alisema kuwa timu zake zitakuwa zinacheza kwa mara ya kwanza mwaka huu kwenye uwanja wa TCC na hivyo mashabiki watarajie kupata burudani safi ya mpira na muziki kutoka kwa bendi ya Msondo Ngoma ambayo itatambulisha nyimbo zake mpya ambazo zitakuwa zinatambulishwa kwa mara ya kwanza.
“Tutaanza kutoa burudani kwa mashabiki na baadaye kuamia kwa Msondo Ngoma, tunatarajia kuwapa burudani safi ambayo itakuwa ya kwanza mwaka huu, mbali ya mechi yetu, timu ya Mass itapambana na Farion, ambapo timu ya maveterani wa Temeke inayojiita kwa jina la Kamazamani itapambana na timu ya Tall, “ alisema Majuto.
Wakati huo huo; bendi ya Msondo ngoma na Twanga Pepeta, jumapili zitatumbuiza jukwaa moja kwenye ukumbi wa CCM Kata 14, Temeke. Burudani hiyo itakuwa ya kwanza mwaka huu kwa wakazi wa Temeke na vitongoji vyake kwa bendi hizo kupiga pamoja. Twanga itaonyesha shoo na nyimbo zake mpya.

No comments:

Post a Comment