STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 4, 2014

RAMADHANI KAREEM, JUMAA MUBARAK


 
LEO ni Ijumaa ya kwanza ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mwezi ambao waumini wa Kiislam wameamriwa kufungwa swaumu ikiwa ni utekezaji wa Nguzo ya Nne kati ya Tano za Dini ya Kiislam.
Waumini wanaomuogopa Allah Subhanna Wataala pamoja na kuuhofia Moto Siku ya Hesabu wanaendelea na swaumu wakiingia siku ya 7 na wengine 6 Allah Aalam!
Kama miongoni mwa waumini, nilikuwa nakukiumbushia waliopo kwenye mfungo kuitekeleza ibada hiyo kama nasaha yangu kwao ili kufanikisha lengo la swaumu kama Mwenyezi Mungu anavyosema kwenye Suratul Bakarah (2-183-5) kuwa 'Enyi Mlioamini mmefadhilishiwa funga na Ramadhani kama waliofaridhishiwa waliokuwapo kabla yenu ili kuwa Wacha Mungu'.
Muhimu mfungaji licha ya kujikurubisha kwa kutenda mambo mema ambayo hata katika miezi ingine imehimizwa, kuwahurumiwa wasio na uwezo na kujikithirisha kusoma Kur'an na kufanya Ibadat mbalimbali, lakini pia ni vyema kuchunga swaumu zao.
WAUMINI wa Kiislam wapo kwenye Mfungo wa Mwezi Ni wajibu wa mwenye kufunga kumhimidi Mwenyezi Mungu kwa sifa zake alizojihimidi Mwenyewe, kwa kuwa kamuafikisha kufanya hiyo Siyyam na kuihiifadhi Swaum yake ili asiitie uchafu na kuiumbua weupe wake kwa maasi, na aepuke yale ambayo Mtume,  swalla-Llahu alayhi waa aaliyhi wasallaam, aliyesema katika Hadithi, ‘Matano humfungulisha mwenye kufunga: uwongo, na usengenyaji, na mtindo wa kubeba maneno na kuyapeleka baina ya watu ili kuwafitinisha, na yamini ya uwongo na mtazamo wenye matamanio.’ 
Mambo matano hayo yampasa muumini ajikinge nayo, na ayaepuke na aiihifadhi Swaum yake isikumbwe nayo.

La kwanza: Uwongo. Asiwe mwenye kutumia uwongo kwenye maneno yake na katika habari zake na katika kukataa kwake na katika jawabu yake, hasa hasa uwongo juu ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

La pili: Usengenyaji – ghiiba – ni kule kuwataja ndugu zako Waisilamu kwa yale wasio yapenda hata ukiwa mkweli. Anapenda mmoja wenu, kula nyamamfu ya nduguye? Na ghiiba – kusengenya ni kati ya madhambi makubwa – kabaa-ir – lakini kwenye mwezi wa Ramadhani, hilo huwa shadidi zaidi kwa vile linabatilisha thawabu za swaumu. 


La tatu: Tena kuna namiima. Na nammaam ni yule mwenye kuchochea fitina baina ya ndugu, na hilo vile vile ni miongoni mwa maasi makubwa kabisa kupita yote. Na kwenye funga ni shadidi zaidi.


La nne: Tena kuna yamini ya uwongo, hiyo hubatilisha thawabu za mwenye kufunga kwa sababu kaonyesha dharau kwa cheo cha Mola na kamtaja pahali pasipo pa haki.


La tano: Tena mtazamo wa matamanio. Yaani ni mtazamo kwa mtu asiyekuwa mahram kwa jicho la kumtaka. Wingi ulioje wa mtazamo huu na wingi ulioje wa mtazamo huu katika zama zetu hizi. Nakuunyamazia hayo si jambo lenye kuhimidiwa  (kutajwa kwa wema).

Kila pahala unapogeukia utawakuta mabinti wenye kukosa hayaa. Na imekuwa wanawake wengi wamelivua jilbab la hayaa na amekuwa kijana ambaye hajanawirika (kwa nuru ya ilmu yenye kumpambanulia kwamba mtazamo ule ni sumu ya imani yake) lengo la mtazamo huu. Katika miezi isiyokuwa ya Ramadhani mtazamo huo huwa mshale kati ya mishale ya ibilisi. Na katika mwezi wa Ramadhani, zaidi ya hayo yalotangulia, mtazamo huo hubadilisha ujira wa Swaumu.

Jitahidini enyi ndugu zangu, msiwe wenye kukodoa macho kwa asiokuwa mahram, ambaye haikujuzieni nyinyi kuwaangalia. Na jikingeni na hayo kama mnavyoweza. Unaloachiwa katika hayo ni kile kinachosadifu mtazamo wako wa mwanzo. Ukiwa wakati unakwenda na hapo kuna mabibi na jicho lako limetua juu yao, basi mtazamo huo wa mwanzo hauna ubaya. Lakini tena usikodoe jicho baada ya hapo. Kwa sababu ule mtazamo wenye hatari, ambao unautegemea kuenea yale mazuri ya yule bibi, ndiyo wenye kubatilisha Swaumu.
Jumaa Mubarak, Ramadhani Kareeem! Allah atuwezeshe kuwa ni wenye kuzingatia Inshallah!

Salvatory Ntebe amfananisha Oloba na Arsene Wenger

Ntebe alipokuwa akiwajibika uwanjani akiwa na Mtibwa
BEKI mpya wa timu ya Ruvu Shooting, Salvatory Ntebe amemmwagia sifa kocha wa timu hiyo Mkenya Tom Olaba akimfananisha na kocha wa Arsenal, Arsene Wenger.
Ntebe aliyetua Ruvu akitokea Mtibwa alisema kwa jinsi Olaba alivyo mahiri katika ufundishaji na kuwa mlezi kwa wachezaji anamfananisha na Wenger anavyowaleta wachezaji Arsenal.
Beki huyo wa kati alisema Olaba anajua kukaa na wachezaji na kuwasaidia kama watoto wake, mbali na uwezo mkubwa wa kufundisha soka kitu kinachompa faraja kubwa kuwa naye.
'Mashabiki watarajie mambo mazuri maana nimekuja kwa kocha bora na mlezi ninayemfananisha na Arsene Wenger. Kocha huyu ni Wenger wa Afrika Mashariki," alisema.
Ntebe aliwahi kunolewa na Oloba wakati kocha huyo akiifundisha Mtibwa Sugar kabla ya kurejea kwao Kenya na wanakutana tena Ruvu Shooting baada ya kusajiliwa hivi karibuni kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Beki huyo ni miongoni mwa wachezaji wapya waliosajiliwa na Oloba kwa msimu ujao wakitokea Mtibwa, wengine ni Yusuf Nguya, Juma Mpakala na nyota wa zamani wa Mtibwa aliyekuwa akicheza soka la kulipwa Burundi, Chagu Chagula.

Abdi Banda asilimia 100 Simba



IMETHIBITIKA kuwa, beki wa kushoto wa Coastal Union Abdi Banda atakipiga Msimbazi na siyo Jangwani tena kama ilivyokuwa ikiripotiwa baada ya Simba kuonyesha dhamira zote za kumnyakua kinda hilo.
Banda anayeichezea pia timu ya taifa ya vijana U20 aliyeng'ara katika msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliyopita, alikuwa akitajwa kuviziwa na vigogo wa Simba na Yanga kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.
Hata hivyo Meneja wa mchezaji huyo, Abdul Bosnia aliliambia MICHARAZO mapema kuwa walikuwa wakisubiri kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa Simba ili viiongozi wapya wamalizane naye kuhusu mchezaji huyo aliyekuwa akiwindwa pia na klabu za Ligi Kuu ya Kenya.
Bosnia alisema aliufahamisha uongozi wa Simba kwamba Banda bado ana mkataba na Coastal Union hivyo wakazungumze na viongozi wenzao wakishamalizana waje mezani kumaliza mambo.
"Simba ndiyo inayoonyesha dalili za kumtaka Banda na niliwajulisha kwamba mchezaji bado ana mkataba na Coastal na kuwataka wakazungumze na wenzao wakimalizana waje kwangu," alisema.
Alisema hata hivyo viongozi hao walimfahamisha kuwa watafanya jambo hilo, ila wanamalizia kwanza uchaguzi wao uliofanyika  Juni 29, ndipo waje kuzungumza naye.
"Walinifahamisha kuwa walikuwa wakisubiri wamalize kwanza uchaguzi wao kisha waje kuzungumza nasi na hizi ni dalili za wazi za kumtaka Banda kuliko ilivyo kwa Yanga ambao wamekaa kimya mpaka sasa," alisema.
Bosnia alisema yeye kama meneja wa Banda hana tatizo lolote juu ya mchezaji huyo kutua klabu gani, muhimu zinazomtaka zimalizane kwanza na Coastal kwani ndiyo inayommiliki kwa sasa.
Simba inamtaka Banda ili kumpunguzia majukumu Issa Rashid 'Baba Ubaya', wakati Yanga ilitajwa kumtaka beki huyo ili kumpa nafuu Oscar Joshua kufuatia taarifa za kutaka kumtema David Luhende.

Coastal Union yazidi kuzoa nyota wapya

 

Aliyekuwa beki wa kulia wa timu ya Rhino Rangers ya Tabora, Amani Juma kulia akisaini mkataba wa kipindi cha miaka miwili kuitumika timu hiyo katika msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kushoto ni katibu
Mkuu wa Coastal Union Kassim El Siagi.???????????????????????????????Aliyekuwa beki wa kati wa timu ya Mgambo Shooting ya Tanga,Bakari Mtama akisaini mkataba wa kuijunga na timu ya Coastal Union ya Tanga jana wanaoshuhudia katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mguto wa kwanza kulia ni Katibu wa Coastal Union,Kassim El Siagi na wa pili kushoto ni mjumbe wa kamati ya usajili wa klabu hiyo, Salim Amiri.
???????????????????????????????Mshambuliaji Mpya wa timu ya Coastal Union,Husein Sued akisaini mkataba wa mwaka mmoja wa kujiunga na timu hiyo yenye makazi yake barabara ya kumi na moja jijini wanashuhudia katikati ni Katibu wa Coastal Union,Kassim El Siagi na wa kwanza kulia ni Meneja wa timu hiyo, Akida Machai.

NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
BEKI wa Kulia wa timu ya Coastal Union,Amani Juma amesema atahakikisha
anashirikiana na wenzake ili kuweza kuipa mafanikio timu hiyo katika
michuano ya Ligi kuu Tanzania bara lengo likiwa kuiwezesha kuchukua
kombe hilo na kuweza kushiriki mashindano makubwa.

Juma ambaye alisajiliwa na Coastal Union kwa mkataba wa miaka miwili
alisema ni wajibu wake kujituma na kupambana vilivyo kuiwezesha timuhiyo kufikia malengo yao waliojiwekea msimu ujao ya kumaliza ligi hiyo
 wakiwa mabingwa.
Alisema katika kutimiza suala hilo wachezaji waliosajiliwa na timu hiyo hawana budi kushikamana na kuwa kitu kimoja kwa kuhakikisha wanafanya vizuri kwenye mechi zao za nyumbani na ugenini wakati ligi
 hiyo itakapoanza.

Aidha aliwashukuru viongozi wa klabu hiyo kwa kuthamini mchango wake
kwa kumpa ridhaa ya kuichezea timu hiyo katika kipindi hicho na kuahidi kupambana kufa na kupona kwa ajili ya kufikia mafanikio
 yatokanayo na soka hilo.

Katika hatua nyingine wachezaji wote waliosajiliwa na timu hiyo
 wanatakiwa kuwasili mkoani Tanga Kesho(leo) kwa ajili ya kuanza
 maandalizi ya kuelekea msimu mpya bila kukosa kwani watakaochelewa kuwasili watachukuliwa hatua za kinidhamu.