STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 4, 2014

CHUJI ATUA AZAM, MCAMEOON AMKUBALI

BAADA ya kutangazwa kuachwa na Yanga, kiungo nyota wa zamani wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Athumani Iddi ‘Chuji’ amedaiwa kusajiliwa na mabingwa wa kandanda nchini, Azam kwa mkataba wa muda mfupi na tayari ameanza kujifua mazoezini na wenzake.
Hata hivyo bado uongozi wa Azam haujathibitisha taarifa hizo, ingawa kocha wa Azam Mcameroon amenukuliwa akimwagia sifa Chuji kwa jinsi alivyoshuhudia vitu vyake kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea Chamazi, Dar es Salaam.
Kocha huyo alisema ameridhika na kiwango cha Chuji na kutokana na uzoefu alionao ataisaidia Azam katika msimu ujao na mashindano ya kimataifa watakayoshiriki.
Hata hivyo viongozi wa Azama wamekuwa wagumu kutjhibitisha taarifa hizo kwa madai mwenye maamuzi ya mwisho juu ya Chuji ni kocha ambaye ni wazi ameridhia mkali huyo aliyewahi kuichezea Simba na Polisi Dodioma kuitumikia timu hiyo msimu ujao na Ligi ya Mabingwa Afrika.

No comments:

Post a Comment